Visa gani pombe ilikufanyia hutasahau?

Visa gani pombe ilikufanyia hutasahau?

Yaani nataka nijitahidi sana safari hii niache moja kwa moja, huwa nakaa tena narudi. Mkuu nimewahi kuzuiliwa kuboard ndege pale DSM uwanja wa Julius Nyerere tena natakiwa Mbeya kikazi. Nilipiga pombe baa moja pale ubungo riverside ilikuwa inaitwa Zambezi, nakuja kushtuka saa 12 alfajiri mfukoni sina hata nauli ya kunipeleka nina simu tu ya kitochi. Ikabidi nitoe line nimpe bodaboda ile simu anipeleke airport, nafika airport nazuiliwa kuingia. Nilirudi hadi riverside kwa miguu. Nina njaa na kiu balaa ilibidi niombe maji ya kunywa kwenye kituo kimoja cha mafuta. Nilitafuta hela nikapanda IT mchana.
Huu utumwa kaka
 
Nawapa mkasa mwingine wa pombe, nikiwa peke yangu familia wameenda likizo ya christmas, nilikunywa pombe siku tatu bila kula ndani namtuma bodaboda tu, wife anapiga simu nashindwa hata kuichukua kwenye sofa nimelala chini kwa carpeti, anamtuma mtu hata sijafunga mlango hali mbaya hatari kuamka siwezi, nikabebwa siku tatu hospital nimewekewa drip natetemeka kama simu iko vibration.

Nilipotoka nikaenda kuchukua k-vant ndogo kuweka mwili sawa. Si mikasa ya kufurahisha lakini naikumbuka sana.
 
Nawapa mkasa mwingine wa pombe, nikiwa peke yangu familia wameenda likizo ya christmas, nilikunywa pombe siku tatu bila kula ndani namtuma bodaboda tu, wife anapiga simu nashindwa hata kuichukua kwenye sofa nimelala chini kwa carpeti, anamtuma mtu hata sijafunga mlango hali mbaya hatari kuamka siwezi, nikabebwa siku tatu hospital nimewekewa drip natetemeka kama simu iko vibration. Nilipotoka nikaenda kuchukua k-vant ndogo kuweka mwili sawa. Si mikasa ya kufurahisha lakini naikumbuka sana.
Dah mamamaee nakuombea

Nilikua na hali ya kufanana na yako

Nilipoichukia nikafanikiwa kuacha

Nakuombea
 
Ukweli ni kwamba pombe ina raha yake sema nikikumbuka yale majanga, heshima niliyopoteza, kupoteza mtu niliyempenda basi napata nguvu ya kusonga
Majanga na madhara iliyoniletea mimi si haba, mengine wacha nibaki nayo. Ningeweza kuwa nakunywa hata vibia vitatu nikaenda kulala ingekuwa sawa. Ila siku hizi bia zilikuwa hazipiti kabisa kooni ni vitu vikali tu.

Nikifikisha hata mwezi nitaanza kuona mwanga
 
Majanga na madhara iliyoniletea mimi si haba, mengine wacha nibaki nayo. Ningeweza kuwa nakunywa hata vibia vitatu nikaenda kulala ingekuwa sawa. Ila siku hizi bia zilikuwa hazipiti kabisa kooni ni vitu vikali tu. Nikifikisha hata mwezi nitaanza kuona mwanga
Duh
 
na mimi niliwahi kufanikiwa kuacha kwa miaka michache, nilivyorudi ndo hali ikawa tete kwelikweli, najitahidi kukaa nayo mbali kuanzia juzi.
Kidogo tufanane mkuu pombe zilinitesa Sana,Kuna kipindi nilipiga valeur kubwa moja na vant ndogo na virikuu viwili!
Halafu asubuhi Nina kazi ya kupokea watalii nilijikuta asubuhi nimelala chini kwenye tiles milango ipo wazi,redio full mziki,taa zinawaka,Sina hata Mia mfukoni na simu

Uzuri geto hapakuibiwa chochote manake ninafuga mbwa wakali

Sijadhurika popote,sikumbuki nilifikaje Niko hangover hatari,tumbo linakwangua balaa,siwezi hata kushika glass ya maji

Nilivyokuwa fala nikajikokota mpaka dukani kwa mangi anipe kvant nizimue niende job!

Hapo ndio niliharibu!!
Nilivyozimua ile vant nilidata mazima 🤣

Kilichoniokoa mule ndani ni juice za machungwa na tangawizi

Nililala geto sio chini ya siku 3 nikaapa sinywi tena

Ila haikupita mwezi nikalisapraiz ini tena
 
Kidogo tufanane mkuu pombe zilinitesa Sana,Kuna kipindi nilipiga valeur kubwa moja na vant ndogo na virikuu viwili!
Halafu asubuhi Nina kazi ya kupokea watalii nilijikuta asubuhi nimelala chini kwenye tiles milango ipo wazi,redio full mziki,taa zinawaka,Sina hata Mia mfukoni na simu

Uzuri geto hapakuibiwa chochote manake ninafuga mbwa wakali

Sijadhurika popote,sikumbuki nilifikaje Niko hangover hatari,tumbo linakwangua balaa,siwezi hata kushika glass ya maji

Nilivyokuwa fala nikajikokota mpaka dukani kwa mangi anipe kvant nizimue niende job!

Hapo ndio niliharibu!!
Nilivyozimua ile vant nilidata mazima 🤣

Kilichoniokoa mule ndani ni juice za machungwa na tangawizi

Nililala geto sio chini ya siku 3 nikaapa sinywi tena

Ila haikupita mwezi nikalisapraiz ini tena
Kuna watu wakiona walevi wanakuwa hawajui changamoto wanazapitia na jinsi wanavyojitahidi kuacha.

Niliwahi kwenda kwa mganga miaka mingi iliyopita dawa niliyopewa nashindwa hata kuisema nilikaa miezi mitatu tu nikarudi. Naamini nitaicha jumla
 
Kuna watu wakiona walevi wanakuwa hawajui changamoto wanazapitia na jinsi wanavyojitahidi kuacha. Niliwahi kwenda kwa mganga miaka mingi iliyopita dawa niliyopewa nashindwa hata kuisema nilikaa miezi mitatu tu nikarudi. Naamini nitaicha jumla
Mimi kwa kweli siwezi sema nimeacha ila nimefanikiwa kwa asilimia kubwa kuepukana na negativity zinazoletwa na pombe!

Nimefanikiwa kuindesha pombe nakunywa nikitaka,nakunywa kwa kiwango nachojua kesho nitakua Safi kiafya na kisalio
Hilo ndio niliofanikiwa ila kuacha nimeshindwa
Wife alishaninywesha mpaka maziwa ya nguruwe lakini wapi,kakesha na maombi sijui redio safina lakini wapi

Nilichogundua pombe haina madhara, madhara yanakuja pale mnywaji anaposhindwa kuimiliki pombe

Sasa hivi Nina uwezo nikiamua nakaa hata miezi sigusi na unakuta Niko viwanja na washkaji wanakula mitungi

Siku nimeamua nimeamua na nikinywa sitaki kesho zinitese
 
Kuna watu wakiona walevi wanakuwa hawajui changamoto wanazapitia na jinsi wanavyojitahidi kuacha. Niliwahi kwenda kwa mganga miaka mingi iliyopita dawa niliyopewa nashindwa hata kuisema nilikaa miezi mitatu tu nikarudi. Naamini nitaicha jumla
Dawa gan mkuu
 
Back
Top Bottom