Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,879
Afrika huenda ikawa kitovu kipya cha mlipuko wa virusi vya corona, Shirika la Afya duniani WHO limeonya.
Kumekuwa na ongezeko kubwa la visa vya ugonjwa huo wiki iliopita.
Kumekuwa na zaidi ya visa 1000 na zaidi ya maambukizi 18,000 kote barani Afrika kufikia sasa , ijapokuwa viwango hivyo viko chini zaidi ya vile vinavyoonekana katika baadhi ya mataifa ya Ulaya na Marekani.
Shirika la Afya Duniani WHO linasema kwamba virusi hivyo vinaonekana kusambaa katika maeneo ya mashambani.
Pia limesema kwamba bara hilo halina ,mashine za kutosha za kuwasaidi wagonjwa kupumua ili kukabiliana na mlipuko huo.
Mkurugunzi wa shirika hilo barani Afrika Dkt Matchidizo Moeti, aliambia BBC kwamba shirika hilo limeshuhudia kuenea kwa virusi hivyo kutoka miji mikuu hadi mashambani katika mataifa ya Afrika Kusini, Nigeria, Ivory Coast , Cameroon na Ghana.
Amesema kwamba kwa sasa wanaangazia kuzuia badala ya kutibu virusi hivyo kwasababu mataifa ya Afrika hayana uwezo kuwatibu wagonjwa wengi wa virusi vya corona.
''Tunataka kupunguza kiwango cha watu ambao wanafikia kiwango cha kuhitaji mashine za kuwasaidia kupumua katika chumba cha wagonjwa maututi , kwasababu tunajua kwamba vifaa hivi ni vichache kwa kiwango chochote miongoni mwa mataifa mengi ya Afrika'', alisema.
Nataka kusema kwamba suala la mashine za kusaidia watu kupumua ni mojawapo ya changamoto kubwa ambazo mataifa hayo yanakabiliana nayo.
Kwa wagonjwa walio katika hali mabaya zaidi wakiugua ugonjwa wa corona, upatikanaji wa mashine za kuwasaidia kupumua kunaweza kuwa changamoto kubwa
Mashine hizo zinasaidia mapafu kupumua na kutoa hewa chafu ya kaboni mwilini wakati mtu ni mgonjwa sana hali ya kwamba hawezi kujisadia kupumua.
Mojawapo ya vifo vilivyorekodiwa kutokana na virusi vya corona barani Afrika ni mwandishi wa Zimbabwe Zororo Makamba mwezi Machi.
Baraza la mji mji mkuu wa Harare limesema kwamba halina vipumuzi kumtibu na kuna hofu kwamba ugonjwa huo unaweza kusambaa haraka katika maeneo ya watu wengi ambapo mtu hawezi kufuata agizo la kutokaribiana na watu wengine ambapo wengi hawana uwezo wa kupata maji safi na sabuni.
Ramani ya Coronavirus: Kasi ya kusambaa kwa virusi 17 Aprili 2020
Maelezo haya yanatokana na data za mara kwa mara kutoka Chuo kikuu cha Johns Hopkins na huenda yasiangazie hali halisi ya mambo yalivyo katika kila nchi.
BBC
Kumekuwa na ongezeko kubwa la visa vya ugonjwa huo wiki iliopita.
Kumekuwa na zaidi ya visa 1000 na zaidi ya maambukizi 18,000 kote barani Afrika kufikia sasa , ijapokuwa viwango hivyo viko chini zaidi ya vile vinavyoonekana katika baadhi ya mataifa ya Ulaya na Marekani.
Shirika la Afya Duniani WHO linasema kwamba virusi hivyo vinaonekana kusambaa katika maeneo ya mashambani.
Pia limesema kwamba bara hilo halina ,mashine za kutosha za kuwasaidi wagonjwa kupumua ili kukabiliana na mlipuko huo.
Mkurugunzi wa shirika hilo barani Afrika Dkt Matchidizo Moeti, aliambia BBC kwamba shirika hilo limeshuhudia kuenea kwa virusi hivyo kutoka miji mikuu hadi mashambani katika mataifa ya Afrika Kusini, Nigeria, Ivory Coast , Cameroon na Ghana.
Amesema kwamba kwa sasa wanaangazia kuzuia badala ya kutibu virusi hivyo kwasababu mataifa ya Afrika hayana uwezo kuwatibu wagonjwa wengi wa virusi vya corona.
''Tunataka kupunguza kiwango cha watu ambao wanafikia kiwango cha kuhitaji mashine za kuwasaidia kupumua katika chumba cha wagonjwa maututi , kwasababu tunajua kwamba vifaa hivi ni vichache kwa kiwango chochote miongoni mwa mataifa mengi ya Afrika'', alisema.
Nataka kusema kwamba suala la mashine za kusaidia watu kupumua ni mojawapo ya changamoto kubwa ambazo mataifa hayo yanakabiliana nayo.
Kwa wagonjwa walio katika hali mabaya zaidi wakiugua ugonjwa wa corona, upatikanaji wa mashine za kuwasaidia kupumua kunaweza kuwa changamoto kubwa
Mashine hizo zinasaidia mapafu kupumua na kutoa hewa chafu ya kaboni mwilini wakati mtu ni mgonjwa sana hali ya kwamba hawezi kujisadia kupumua.
Mojawapo ya vifo vilivyorekodiwa kutokana na virusi vya corona barani Afrika ni mwandishi wa Zimbabwe Zororo Makamba mwezi Machi.
Baraza la mji mji mkuu wa Harare limesema kwamba halina vipumuzi kumtibu na kuna hofu kwamba ugonjwa huo unaweza kusambaa haraka katika maeneo ya watu wengi ambapo mtu hawezi kufuata agizo la kutokaribiana na watu wengine ambapo wengi hawana uwezo wa kupata maji safi na sabuni.
Ramani ya Coronavirus: Kasi ya kusambaa kwa virusi 17 Aprili 2020
Maelezo haya yanatokana na data za mara kwa mara kutoka Chuo kikuu cha Johns Hopkins na huenda yasiangazie hali halisi ya mambo yalivyo katika kila nchi.
BBC