Zeal of God
JF-Expert Member
- Jun 12, 2022
- 569
- 879
Nimeona kwenye taarifa ya habari ITV vipondozi vinatekezwa na mamlaka husika.
Ninavyojua mtu hawezi kuweka bidhaa kwenye duka lake ikiwa haina soko, tena bidhaa ambayo ni hatari kwake akikutwa na serikali.
Vipodozi hivi vinanunuliwa sana na watu ndio maana vinajazwa kwenye maduka.
Leo tumevitekeza ila kesho mtu anaenda dukani kuulizia, na atahakikisha anavipata.
Tunaweza kudili na wauzaji tukasahau wanunuaji ambao wanaifanya biashara ya vipodozi iendelee kukua.
Wananchi wanapaswa kupewa elimu, mtu akishajua madhara ya vipodozi ataacha kununua. Akiacha kununua muuzaji hataleta bidhaa hatarishi kwenye duka lake.
Tusipotoa elimu tutaendelea kupambana na tatizo juu juu, lakini wananchi wataendelea kuathirika.
Elimu itolewe kwa kina kupitia vyombo vya habari kama yalivyo matangazo mengine.
Ninavyojua mtu hawezi kuweka bidhaa kwenye duka lake ikiwa haina soko, tena bidhaa ambayo ni hatari kwake akikutwa na serikali.
Vipodozi hivi vinanunuliwa sana na watu ndio maana vinajazwa kwenye maduka.
Leo tumevitekeza ila kesho mtu anaenda dukani kuulizia, na atahakikisha anavipata.
Tunaweza kudili na wauzaji tukasahau wanunuaji ambao wanaifanya biashara ya vipodozi iendelee kukua.
Wananchi wanapaswa kupewa elimu, mtu akishajua madhara ya vipodozi ataacha kununua. Akiacha kununua muuzaji hataleta bidhaa hatarishi kwenye duka lake.
Tusipotoa elimu tutaendelea kupambana na tatizo juu juu, lakini wananchi wataendelea kuathirika.
Elimu itolewe kwa kina kupitia vyombo vya habari kama yalivyo matangazo mengine.