VIPEPEO WEUSI
SEASON 2 – FROM ZURICH WITH RULES
EPISODE 02
Simu ya Cheupe bado ilikuwa inaita bila kupokelewa kwa karibia mara ya tano sasa niliyojaribu kupiga. Sikujua bado ni kwa sababu gani simu ilikuwa haipokelewi japo moyoni bado nilikuwa na hisia mbaya kuhusu kilichokuwa kinaendelea, lakini niliendelea kujipa moyo kwamba kila kitu kiko sawa.
Nikainua tena simu na kubofya kumpigia Issack,
“Niaje kichwa?” Issack alinisalimu mara tu baada ya kupokea simu
“Poa poa… uko wapi?”
“Ofisi kwangu.”
“naomba uende forest home ukamcheki shemeji yako..!”
“kuna tatizo kwani?”
“sijajua ila simu yake haipokelewi tangu mchana…”
“Poa mkuu dakika sifuri tu nakupa jibu..!”
“Thanks!”
Nikakata simu.
Nilikuwa naongea na simu huku nimesimama kwenye dirisha la chumba changu cha hotel naangalia nje kwenye bwawa la kuogelea.
Chumba changu cha hoteli kilikuwa kiko katika usawa ambao kutoka dirishani uklikuwa unaweza kabisa kuona sawia bwawa la kuogelea na mgahawa ulio pembeni yake. Nilikuwa nimegundua kwamba wale mabinti wawili, yule wa kizungu na mwenzake mwenye muonekano kama mnyarwanda walikuwa wanapenda kutumia muda wao bwawani pale au kwenye mgahawa kila siku muda wa asubuhi na jioni. Lakini ajabu ni kwamba leo sikuweza kuwaona na wala hakukuwa na dalili yeyeote ya uwepo wao.
Nilikaa kwa dakika kumi nzima dirishani nikichungulia labda wangeweza kutokea muda wowote lakini hakukuwa na mafaniko yoyote yale.
Ghafla nikasikia mlango unagongwa.
“nani?” nikauliza kwa tahadhali.
“Muhudumu.!” Sauti ikanijibu upande wa mlango.
Nikafungua mlango haraka.
“habari za jioni.!” Muhudumu wa kike alinisalimu akiwa amesimama mbele ya mlango wangu baada kufungua.
“poa kabisa..”
“kuna mzigo wako huu umeachwa pale mapokezi..!” muhudumu alinieleza huku ananipatia bahasha.
“ni nani ameuleta?” nikauliza nikiwa napokea bahasha na kuanza kuifungua.
“hakuacha jina… alisema ni mzigo wako unautegemea kwa hiyo utaelewa.!”
“asante sana!” nikashukuru huku naanza kufungua bahasha.
Nilifungua bahasha kwa haraka na ndani yake kulikuwa na kipande cha karatasi cha ukubwa wa wastani. Nilipoitazama karatasi hii ambayo ilikuwa na maneno kadhaa laki ni kwa haraka sana jicho langu lilitua kwenye neno “December 19”.
“Dada.! Samahanii..” nilimuita muhudumu ambaye tayari alikuwa amefika hatua kadhaa kutoka mlangoni akiwa anaondoka.
“bila samahani..!” alinijibu huku anarejea tena pale mlangozi kwangu.
Kunajambo nilikuwa nataka kumuuliza lakini kwa namna ambayo nilimsoma haiba yake kwa haraka nilijua kabisa hawezi kunieleza kwa kuzingatia maadili yake ya kazi. Wanasema kwenye udhia penyeza rupia. Ndicho nilichokifanya, nikaingiza mkono mfukoni na kutoa noti kadhaa za fedha, nikachomoa noti mbili za elfu kumi kumi na nyingine nikazirudisha tena mfukoni.
“samahani nilikuwa sijakushukuru..!” niliongea huku namkabidhi zile noti mbili za shilingi elfu kumi kumi.
“Usijali.! Asante sana kaka..” alipokea huku anatabasamu karibu meno yote yako nje.
“kuna jambo nahitaji unisaidie kidogo kama hutojali..!”
“jambo gani kaka?” aliuliza kwa wasi wasi. Kawa akili ya haraka haraka niliweza kumsoma kuwa alikuwa anahisi labda nataka kuongea masuala ya mapenzi.
Ilibidi niende kwenye hoja yangu haraka ili kuepusha hisia niliyomuona ameanza kuipata kichwani.
“kuna wageni wenu wawili mabinti.. mmoja ni mzungu na mwenzake mweusi… unaweza kujua kama wapo au wameshaondoka?” nilimuuliza kwa reja reja tu bila kuwa na uso ‘serious’. Nia yangu nilikuwa nataka apate hisia labda nilikuwa namtaka kimapenzi mmojawapo wa hao ninao waulizia.
“mmmh! Ngoja nicheki nitakuja kukushtua.” Yule muhudumu alijibu huku anatabasamu.
“pamoja na hilo naomba uangalie na kunipatia majina yao kamili waliyo andikisha hapa, wanakotoka na taarifa nyingine ambazo wameandikisha.!”
Nilipoongea haya nilimuona uso wake unabadilika kutoka kwenye tabasamu na kuwa uso wa ‘kazi’. Nadhani sasa alijua kuwa sikuwa na nia ya kimapenzi juu ya haoa mabao nawaulizia bali lilikuwa suala lingine kabisa ambalo linaweza kuwa muhimu au la hatari. Sikutaka hisia hii ikue ndani ya kichwa chake, kwa hiyo ilinibidi nifanye kitu haraka ili kumlainisha tena. Nikaingiza tena mkono mfukoni na kutoa noti nyingine mbili za elfu kumi kumi.
“hii utaongezea hapo ya vocha.!” Nikamshikisha mkononi huku amenikazia macho bila kuangalia pale mkononi ninako mpa fedha kama vile alikuwa hataki. Ilibidi nimfunue kiganja cha mkono, niweke hela alafu nimkunje tena kiganja.
Tuliangaliana kwa sekunde kadhaa kisha akageuka na kuondoka pasipo kusema kitu chochote kile. Moyoni nilikuwa naomba dua kimya kimya afanye kile ambacho nimemuomba, anisaidie kupata taarifa za wale mabinti wawili, mzungu na mwenzake mweusi. Nikafunga mlango na kuingia tena ndani chumbani.
Macho yangu yalikuwa yametua tena kwenye simu ambayo niliiacha kitandani, niliangalia kama kuna meseji au walau simu iliyopigwa, na sio simu tu bali simu kutoka kwa mkewangu Cheupe. Bado hakukuwa na chochote.
Nikainua simu na kupiga tena namba ya Cheupe. Safari hii ilikuwa haipatikani kabisa. Moyo ulinienda mbio zaidi nikimuomba Mungu nipate jibu la haraka kutoka kwa Godi niliyemtuma aende nyumbani.
Nikarejea tena kusoma ujumbe ulioandikwakwenye kile kijikaratasi kilicholetwa kwenye bahasha na muhudumu. Nikakisoma tena na tena kuhakikisha kuwa nilichokuwa nakielewa kilikuwa ni sahihi na hakukuwa na chochote ambacho kilikuwa kinanipita. Ujumbe wenyewe ulikuwa ni mfupi tu lakini kama nilikuwa nimeuelewa kwa usahihi ulikuwa na maana kubwa sana.
“DECEMBER 19
7712/LH. A+. A+
CITIBANK. ZURICH.”
Nilielewa huu ujumbe ulikuwa na maana gani, lakini kilichoniumiza kichwa nilikuwa najiuliza ni nani aliacha mapokezi na kutaka uletetwe kwangu? Kwa asilimia kubwa sana nilihisi kwamba ni wale mabinti wawili ndio waliokuwa wananifanyia huu mchezo. Lengo lao na dhamira yao haswa bado sikuijua. Nikasogea tenba dirishani na kuanza kuchungulia bwawani na kwenye mgahawa moyoni nikiwa na tumaini dogo labda nitawaona tena wale mabinti. Nilisimama pale dirishani kwa takribani dakika kumi kichwa kikiwa kinawaka moto haswa nisijue ni wazo lipi nilipe nafasi ya kulichakata kwenye ubongo.
Kwa upande mmoja bado nilikuwa kwenye kitendawili cha kwa nini simu ya Cheupe ilikuwa haipokelewi na sasa hivi ilikuwa haipatikani kabisa. Upande mwingine nilikuwa najiuliza kwa nini hawa mabinti walikuwa wananifuatilia kwa siri ingawa kama nilikuwa sahihi moyoni mwangu niliamini kwamba wametumwa hapa ili kuja kuonana na mimi, lakini ajabu walikuwa hawajajitambulisha kwangu, kitu pekee walichokuwa wanakifanya ni kufuatilia nyendo zangu kwa siri kubwa.
Upande mwingine nilikuwa kwenye kitendawili cha huu ujumbe nilioletewa kwenye bahasha dakika chache zilizopita. Ujumbe wenyewe haukuwa kitendawili kwangu, bali swali lililo niumiza kichwa lilikuwa ni nani alikuwa ameleta ujumbe huo. Jibu rahisi zaidi la swali hili lilikuwa ni wale mabinti wawili. Lakini sikujua kwa nini kuna upande fulani wa moyo wangu ulikuwa unakataa jibu hili.
Nikaona hakukuwa na haja ya kuendelea kuumiza kichwa wakati kulikuwa na njia rahisi zaidi ya kupata ukweli.
Nikafunga mlango wa chumba changu na kuteremka mpaka chini mapokezi ya hoteli. Pale mapokezi niliwakuta wadada wawili lakini yule dada ambaye aliniletea bahasha juu chumbani kwangu hakuwepo tofauti na nilivyodhani kwamba atakuwa ni dada wa hapa mapokezi.
“habari zenu waerembo!”
“nzuri tu kaka!” wakaniitikia kwa pamoja kwa tbasamu.
“nililetewa bahasha juu chumbani kwangu… nilikuwa na uliza ni nani ambaye aliicha bahasha hiyo hapa na kusema iletwe kwangu?” nikawauliza.
Wale wadada walionekana kushanga kana kwamba walikuwa hawajui ni nini nilikuwa naongea.
“bahasha gani kaka?” mmoja wao akaniuliza kwa mshangao kidogo.
“bahasha nimeletewa na muhudumu mmoja kati yenu japo sio nyinyi.. ameniletea juu chumbani dakika chache zilizopita.
Nikajieleza tena huku na mimi nawashangaa wao kwa kutokujua ninchowauliza.
“kwa kweli sifahamu hicho kitu kaka.. hatujapokea bahasha yeyote hapa siku ya leo.!” Dada mmoja wapo akanijibu akiwa na uhakika na anachokiongea huku pia akiendelea kunishangaa kwa nianchoiuliza.
“una uhakika kuwa hamjapokeaa bahasha hapa siku ya leo?” nikamuuliza kwa udadisi zaidi muda huu nilianza kupata wasiwasi moyoni.
“nina uhakika kaka.. hatujapokea bahasha yeyote hapa mapokezi siku ya leo! Ni nani ambaye alikuletea hiyo bahasha?” akaniuliza.
Nikaanza kuwaelekeza muonekano wa huyo muhudumu aliyeniletea bahasha na muda gani hasa aliniletea.
“atakuwa ni Siwatu huyo!” yule muhudumu mwingine akadakia nikiwa bado naendelea kuwaelekeza muonekano wa huyo muhudumu ambaye aliniletea bahasha.
“hebu kamuite aje aeleze!” muhudumu wa kwanza yule ambaye alionekana kama kwa namna fulani alikuwa ni kiongozi wa wenzake au wanamuheshimu kwa namna fulani aliongea huku anamuagiza mwenzake ili “Siwatu” akaitwe.
Kama dakika tano baadae yule muhudumu alirejea akiwa na muhudumu mwingine ambaye ndiye alikuwa ni yule aliyeniletea bahasha juu chumbani kwangu.
“yani huyu Siwatu hata hasikii.. yani ana mambo ya kijinga sana huyu” yule muhudumu alikuwa anakuja anafoka na mwenzake ambaye sasa nilimfahamu kuwa alikuwa anaitwa Siwatu, yule ambaye aliniletea bahasha.
“nini tena?” yule uhudumu niliyebaki naye pale mapokezi aliuliza huku anasimama.
“hebu msikie anachokisema!” yule mwenzake aliongea tena kwa kufoka.
Walifika mpale mapokezi huku wote macho tukiwa tumemkodolea Siwatu. Siwatu mwenyewe alikuwa amejikunyata kwa woga ana angalia chini.
Sasa hivi ndio niligundua tofauti ya sare alizovaa Siwatu na sare ambazo walikuwa wamevaa wale wadada wa pale mapokezi. Siwatu alikuwa amevaa shati na suruali ya kitambaa rangi ya bluu-nyeusi. Wale dada wa pale mapokezi mmoja alivaa suruali na mwingine sketi fupi lakini zote za rangi kama ya sare za Siwatu lakini wao walivalia na mashati meupe juu.
Kwa uzoefu wangu wa kukaa mahotelini niligundua mara moja kuwa Siwatu alikuwa ni muhudumu wa masuala ya usafi vyumbani kwenye hii hoteli.
“hebu nielezeni, nini?” yule muhudumu niliyebaki naye pale mapokezi aliongea kwa sauti ya taratibu safari hii.
“samahani dada nilijisahau nikapokea mzigo kutoko nje!” Siwatu alijieleza huku ameanzgalia chini alafu anabinya binya vidole kwa uoga.
“wewe Siwatu utazoea lini kazi jamani?? Mara ngapi nakueleza usipokee mizigo huko nje… ukipewa bomu je?” dada wa pale mapokezi alifoka.
Niliwaelewa ni nini walikuwa wanakiongelea. Inaonekana kuwa aliyeleta bahasha ile hakuingia ndani ya hoteli hapa mapokezi, bali kwa namna fulani alimkabidhi mzigo Siwatu wakiwa nje ya Hoteli.
“ok! Hakuna shida ilikuwaje kwani dada’ngu?” nikauliza huku nikiwatuliza wale wenzake wasiendelee kuofoka.
“nilikuwa nadeki hapo nje kwenye korido ndio kuna mkaka akaja na gari akasimamisha akanipa ile bahasha akanieleza kuwa nikuletee chumbani kwako… nilipomuuliza nikwambie imetoka wapi, akanijibu kwamba ameandika humo ndani na wewe unajua.!” Siwatu aliongeaa huku amejiinamia chini anabinya binya vidole mikononi.
“umamkumbuka muonekano wake?” nikamuuliza tena.
“mweupe hivi alafu ana mandevu mengi amenyoa ‘timbalendi’.” Siwatu aliongea huku bado amejiinamia.
Mara moja nikaelewa ni nani alikuwa ameleta bahasha hiyo. Alikuwa ni Godfrey au Godi kama ambavyo tulipendelea kumuita. Nikajitahidi nisionyeshe mshtuko wangu.
“msijali nimeshafahamu ni nani ameleta huu mzigo… ni rafiki yangu! Msijali..” nikaongea kwa kujiamini huku nikiwatuliza wasiendelee kufokeana.
“hapana kaka… huyu hasikii… hapa hotelini yanatokea mambo mengi… mtu akileta mzigo wa mteja ili apelekewe chumbani huwa tunataka akabidhi hapa mapokezi sio kupeana kienyeji hivyo… mfano huo mzigo ukipotea tunafanyaje? Nani atawajibishwa… Siwatu hili sula lisitokee tena la sivyo namfikishia boss hii taarifa..!!” dada wa mapokezi pale akafoka.
“yani huyu mzito sana kuelewa.. wiki nzima hii bado tu haujajua maadili ya kazi yako? Mwenzake naye akaongezea.
Aliposema hili neon “wiki nzima” nilijikuta kama kuna taa fulani hivi imewaka kichwani mwangu. Kuna hisia fulani hivi nikaipata kana kwamba kuna jambo fulani hapa la zaidi natakiwa kulijua. Nahisi Siwatu naye kwa namna fulani neno hili lilikuwa limemgusa maana nikamuona amenikata jicho fulani hivi la kuibia ibia nisigundue kuwa ananiangalia.
“basi limeisha hili jamani kuweni na amani… Siwatu usisahau ile kazi niliyokutuma uifanye sawa?” nikaongea huku naanza kutembea kuelekea mlango wa kutokanje ya hoteli.
“Sawa kaka!” siwatu akanijibu kwa heshima zote.
Nikafungua mlango na kutoka nje. Nyuma yangu nikasikia wenzake wanamuuliza, “kazi gani amekutuma?” alafu nikmsikia Siwatu anawajibu, “kuna nguo chumbani kwake anataka zipigwe pasi.”
Nikajikuta natabasamu na ucheka namna ambavyo Siwatu aliweza kutunga uongo wa haraka haraka namna ile. Kazi niliyokuwa namkumbushia kuifanya ilikuwa ni kunipatia taarifa za wale mabinti mzungu na mwenzake mnyarwanda, lakini alijiongeza akili haraka haraka na kuwaeleza wenzake kuw
kuwa nimemtuma kunipigia pasi nguo.
Bado kuna kitu fulani kichwani nilikuwa nashindwa kukichakata kuhusu Siwatu, hasa hasa baada ya mwenzake kutamka kauli ya “wiki nzima hii bado tu hauelewi kazi”… japo ilikuwa kauli ya kawaida tu lakini ilikuwa inaninyima raha ndani ya nafsi. Ina maana Siwatu amekuwa kazini pale kwa wiki moja tu? Sikuelewa ni kwanni lakini nafsi yangu ilikuwa haijatulia kuhus suala hili.
Lakini pia nilikuwa najiuliza kuhus Godi kumpa Siwatu kikaratasi kile. Godi alikuwa amepata wapi kile alichoandika. Jibu zuri ambalo lilikuja kichwani ilikuwa ni kwamba Godi alikuwa ameagizwa na mtu aniletee ile bahasha. Lakini kwanini asinipigie simu kunieleza kuwa ana mzigo wangu ili anikabidhi mwenyewe badala yake anauacha mapokezi tena bila maelezo ya kujitosheleza? Nikahisi labda atakuwa alikuwa na haraka mno.
Nikavuka barabara na kwenda mpaka upande wa pili ambapo kuna kibanda cha chips kinaangaliana na hoteli na nikakaa hapo. Nikaagiza mishikaki tupu na soda na kuanza kula taratibu huku natafakari vitendawili ambavyo vilikuwa kichwani mwangu. Kwa kiasi fulani kichwa kilikuwa kinakaribia kupasuka nikijitahidi kufikiri japo niweze kung’amua machache kati ya yale ambayo yako kichwani mwangu.
Nikiwa bado nandelea kula mishikaki yangu nikisindikiza na kinywaji, mara simu yangu ya mkononi iliita.
“Issack… nipe ripoti.” Nilipokea simu.
“Kichwa tafadhali naomba urudi Morogoro leo!” Issack aliongea kwa sauti ya woga lakini iliyo makini.
Nilijikuta moyo umepasuka, pwaaa.!
“kuna nini Issack… mke wangu na mwanagu wako salama?” niliuliza huku nimeanza kuhema kwa woga wa kupokea habari mbaya.
“Kichwa!! Naomba urudi Morogoro sasa hivi… yani hivi ninavyoongea nataka uwe unakusanya vitu vyako unaanza safari!” Issack alionngea kwa sauti ya kufoka safari hii baada ya kuona simsikilizi anachonisisiotiza.
“ok ok ok! Calm down Issack… najiandaa sasa hivi nirudi, lakini naomba unieleze walau moyo wangu utulie… mkewangu na mwanagu wako salama?”
“wako salama… tuko nao hapa mimi na Godi”
Nilihisi kama dunia imepasuka. Godi?? Godi anawezaje kuwa Morogoro muda huu? Kwa maelezo ya Siwatu japo hakutaja jina lakini ni dhahiri kuwa aliyekuwa anamuongelea alikuwa ni Godi.
“umesema mko na Godi hapo?” nikauliza kwa sauti ya chini lakini iliyo thabiti.
“kichwa rudi Morogoro sasa hivi kuna situation hapa.. yes, niko na Godi, mkeo na mwanao Ayanda!” Issack akafoka tena.
Nikajikuta nimekata simu bila kujibu chochote kile. Nikakumbuka ile kauli ya yule muhudumu, “wiki nzima sasa bado tu hujaelewa kazi.” Ina maana Siwatu ana wiki moja tu tangu aanze kazi pale Dodoma Hoteli? Taa ikawaka tena kichwani mwangu. Kuna mchezo hapa ulikuwa unafanywa na huyu anayejiita Siwatu.
Sikumbuki kama nilimlipa mwenye chips au ni muda gani nilivuka barabara kurejea upande wa hoteli, ninachokumbuka ni namna ambavyo nilikuwa natembea haraka na kwa hasira kuelekea mapokezi ya hoteli.
“Siwatu yuko wapi?” niliuliza huku nahema baada ya kufika mapokezi.
“uko sawa kaka?” dada wa mapokezi mmoja wa wale niliowakuta mara ya kwanza aliniuliza kwa mshangao huku akiwa na woga kutokana na uso wangu wa hasira.
“Siwatu yuko wapi?” niliuliza tena kama sijasikia swali lake.
“ameondoka nyumbani shift yake imeisha.!!” Dada alinijibu huku amenitumbulia macho kwa woga.
“fuuucck!” tusi lilinitoka bila kujijua na haraka nikaanza kupanda ngazi kuelekea juu chumbani kwangu.
Nilielewa kuwa huyu anayejiita Siwatu hawezi kurudi tena hapa hata hiyo kesho. Alikuwa hapa kwa kazi maalumuna kazi hiyo alikuwa amesha itekeleza. Tatizo nilikuwa bado sijajua ni kazi gani hasa. Kunipatia ile bahasha? Lakini mbona kila kilichoandikwa ndani yake japo ni siri kubwa lakini havikuwa vipya kwangu. Labda tu ni kitendawili kingine cha kujiuliza ni namna gani alikuwa amepata ile taarifa maana ni watu wachache mno tunaofahamu kitu hicho. Mimi, marehemu baba yangu na Rais wa bank ya Citibank.
Sikutaka kupoteza muda zaidi, kwa usalama wangu natakiwa kuondoka hapa mkara moja kabla jambo baya halijatokea. Nilikuwa tayari nimefika mbele ya mlango wa chumba changu. Nilitoa funguo haraka haraka mfukoni na kufungua mlango.
Nilipofungua tu mlango kitu cha kwanza nilichokiona ilikuwa ni bahasha kubwa kama size ya A4 ikiwa sakafuni. Nikashituka.
Nikainama kuikota. Juu ya bahasha kulikuwa na maneno, “Kazi uliyonituma” yameandikwa kwa kalamu ya wino. Nikaanza kuifungua huku moyo unaenda mbio na kijasho chembamba kinachuruzika.
Nilipofungua ndani ya bahasha nilikuta picha ya wale mabinti wawili, mzungu na yule mnyarwanda. Pamoja na hizo picha kulikuwa na kama karatasi nne zilizochapwa maandishi mengi sana ambayo japo sikuyasoma kwa muda huo lakini yalionekana kuwahusu wale mabinti.
Kama nusu saa iliyopita nilimuomba Siwatu anipe taarifa za wale mabinti wawili ambazo waliziandikisha hapa hotelini, but this was too much. Taarifa hizi zimetoka au amezitoa sehemu fulani adhimu, hoteli abadani hawawezi kuwa na taarifa kama hizi.
Nikajikuta najiuliza swali kichwani ambalo nilipaswa kujiuliza muda wote huu, “HUYU SIWATU NI NANI? NA ANATAKA NINI?”
Mara simu yangu ya mkononi ikaita, nikatupa jicho kwenye kioo, jina lilisomeka, “ERIC KABURU”.
Mapigo ya moyo yakaongezeka maradufu. Nilihisi mpaka kizunguzungu.
Itaendelea….
THE BOLD