Vipepeo Weusi: Mkakati Namba 0034 (Simulizi)

Kwakweli itabidi The bold aongeze scene kali za mahaba...
Hakuna namna sasa
Aaaaaaaah Nifah eeeh zisiwe nyingi,hii simulizi ni ya ki intelijensia,isipokua nimefurah msimulizi The bold amejaribu kuwaweka wahusika wengi VIJANA na changamoto zao za kileo za kimaisha kuanzia ajira na changamoto zake, mapenzi, na umuhim wa networks.
Mi nna simulizi inayoelezea masuala ya dawa za kulevya,UJANGILI,AJALI ZA BARABARANI, rushwa,ukimwi,MAPENZI,migomo vyuoni na harakat za vijana kwenye mapambano ya maisha.
Huwez zungumzia vijana wa kileo bila mapenz, social networks
 
Ilipoishia Episode 4



Ray kwa kusaidiwa na rafiki yake Issack anafanikiwa kudukua bank statement ya shirika la Alice Cartz foundation na kugundua miamala kadhaa ya fedha nyingi kutoka kampuni ya kitanzania ya Ndeshema Safaris kwenda kwenye shirika hilo. Anaamua kwenda gerezani kuonana na mmiliki wa kampuni ya Ndeshema Safaris Eric Kaburu ambaye anamshangaza kwa kumtaja maijina yake kiufasaha ikimaanisha kuwa anamfahamu vizuri.

Aliporudi Dar na akiwa anaelekea Tegeta nyumbani kwa mpenzi wake Cheupe anatekwa na watu wanojitambulisha kuwa ni Maafisa wa Usalama wa Taifa.

Endelea….





EPISODE 5



Ndani ya gari niliwekwa katika siti ya nyuma na yule jamaa aliyenipandisha kwenye gari akakaa siti ya mbele kwenye usukani na kuendesha gari.
Kule nyuma nilikowekwa siti ya pembeni yangu alikuwepo mdada wa makamo anayeelekea kwenye umama ambaye kwa makadirio hawezi kuvuka miaka 34. amevalia suti ya kike ya rangi ya bluu. Alikuwa mwembamba, mrefu na sura yake ilikuwa nyembamba kama ya Kinyarwanda, au tuseme ya Kitusi kwa ufasaha zaidi.

Hakunisemesha chochote na mimi sikusema chochote. Nilibaki naduwaa tu kuangalia kile kilichokuwa kinaendelea.

Magari yote yakaendeshwa kwa kufuatana kuelekea barabara inayoelekea sinza. Tukiwa tunakaribia maeneo ya sinza, simu ya mkononi ya yule dada aliyekaa pembeni yangu ikaita.

"Hello.!" Yule dada akapokea simu na nikagundua lafudhi ya kifaransa katika utamshi wake.

"Oui… ok… ok... d'accord.!" Yule dada akawa anamuitikia tu anayeongea naye kwenye simu huku anachanganya maneno ya kingereza na kifaransa kisha akakata simu.

"..il que nous allions directement à la maison.." Yule dada akaongea kifaransa haraka haraka akimwambia dereva.

"..est-il là?" Dereva akamuuliza

"..oui.!" dada akamjibu

Baada ya kuwasikia maongezi yao ndipo hapa nikaafikiana na hisia zangu kwamba yule dada ni Mnyarwanda. Aliikicharaza kifaransa kwa ufasaha kabisa. Uzuri nakifahamu kifaransa kwa kiasi. Yule dada alipokata simu alikuwa amemueleza dereva kuwa huyo mtu aliyekuwa anaongea naye ataka tuelekee moja kwa moha "nyumbani". Na dereva alikuwa amemuuliza kama huyo mtu amefika tayari hapo nyumbani (huyo aliyekuwa anaongea naye) na yule dada akamjibu kuwa amefika.

Nikabaki na maswali kichwani. Yule jamaa wa mbele anayeendesha gari anakifahanu vizuri tu kiswahili na anaonekana ni mtanzania na kipindi wananichukua alijitambulisha kwangu kama Afisa wa Usalama wa Taifa na niliamini moyoni mwangu kweli walikuwa ni Usalama wa Taifa kutokana na haiba zao.
Jambo nililokuwa sielewi ni huyu dada mnyarwanda anausikaje na hawa Usalama wa Taifa maana anaonekana ni kama "mwenzao".

Nikiwa katika kuwaza huko tayari tukawa tumetokea Mwenge na tulipofika kwenye makutano ya barabara wakaendesha magari yote matatu kuifuata Old Bagamoyo Road. Moyo ukanipasuka. Nikaanza kuwaza moyoni "napelekwa mabwepande". Jasho likaanza kunivuja kwa mbali. Nikaanza kukumbuka kuhusu sakata la yule daktari kupelekwa Mabwepande kufanyiwa "usafi wa kinywa" na "usafi wa kucha". Nikahisi hicho ndicho kilikuwa mbele yangu. Joto la mwili likapanda kweli kweli jasho likanitoka haswa.

Tulipo fika maeneo ya Lugalo nikageuka kumtazama yule dada. Kumbe muda wote huu ananiangalia tu jinsi ninavyopaniki. Nilivyomuangalia tu na macho yetu kukutana akatabasamu. Nilikereka kweli kweli, nilitamani nimtemee mate. Alionekana kuinjoi jinsi nilivyo paniki.

"..où m'emme-vous?" (mnanipeleka wapi) nikamuuliza kwa kifaransa changu cha kuunga unga.

Yule dada akatabasamu tena na kunijibu kwa mkato tu, "..domicile!" (Nyumbani).

Nikajiinamia. Nikahisi naanza kuchanganyikiwa. Nyumbani??, nikajiuliza. Nyumbani wapi wanaponipeleka? Nyumbani kwetu Mwembe Chai, nyumbani kwetu Morogoro, huku nyumbani wapi wanaponipeleka? Au wanamaanisha "nyumbani kwangu kwa milele". Daammn it! Nikijisikia hasira na kuchanganyikiwa kila mara neno "Mabwepande" lilipokatiza kichwani mwangu.

Tulipoofika maeneo ya Mbezi Beach Jogoo magari yote yakakata kulia kutoka barabara kuu kufuata njia ya vumbi.
Nikajikuta nimeshikwa na mshangao wa ajabu. Presha ikashuka, lakini mshangao nilioupata ulikaribia kunipandisha tena presha. Ni kama vile mtu ameingiza mkono mfukoni ukitarajia atoe kisu na kukudhuru badala yake anatoa pipi.

Nikageuka na kumuangalia yule dada pembeni yangu kwa butwaa. Akatabasamu tu. Nahisi alikuwa anajua kinachoendelea akilini mwangu.
Mshangao niliokuwa nao ilibakia kidogo tu nimuulize "hatuendi Mabwepande?".
Presha na hasira zikashuka kiasi. Walau nilijua siendi kufanyiwa "usafi wa kinywa na kucha". Walau moyo ulipoa, lakini bado nilikuwa najiuliza wananipeleka wapi.

Gari zote zikaendeshwa mpaka mbele kidogo kuna barabara nyingine ndogo inaingia kulia kwenda kanisa la Agape, tukaicha hiyo tukanyoosha mpaka mbele kidogo. Mitaa hii ilikuwa na utulivu sana, labda kwa vile wanaishi watu wa kipato cha juu. Maana mda wote huu sikunbuki kama tulimpita mtu yeyote barabarani. Tulikuwa tunapita tu majumba ya kifahari yenye mageti makubwa.

Mbele kidogo tukakuta barabara nyingine inaingia kushoto. Tukaifuata hiyo barabara mpaka tulipotokea mbele ya nyumba moja kubwa. Nayo ilikuwa ya kifahari kama nyumba nyinginezo pale mtaani. Ilikuwa kubwa na uzio mkubwa wa ukuta. Geti likafunguka. Nadhani lilitunia rimoti au sijui teknolojia gani ya siku hizi maana sikuona mtu kufungua.

Tukaingia ndani na wakapaki magari. Mda wote huu nilikuwa sijamuona Afisa au maafisa waliokuwa kwenye ile Land Cruiser nyeusi. Waliponichukua pale magomeni popobawa ni maafisa waliokuwa kwenye land cruiser ya kijivu iliyonizibia njia mbele ndio walishuka kwenye gari na mmoja aliyevaa suti kunichukua mpaka kwenye gari yao na yule alivaa suruali na shati akaendesha gari yangu. Ile land cruiser nyeusi hakushuka Afisa yeyeto ulitufuata tu kwa nyuma.

Tulipopaki hapa ndani ya hii nyumba ndio nikaona Afisa aliyekuwemo kwenye ile land cruiser nyeusi. Alishuka kijana mdogo tu wa makamo yangu. Kwa muonekano tu alikuwa hazidi miaka 29. Kwa kumkadiria haraka haraka nilihisi atakuwa na miaka 28 au 29.
Alikuwa amevalia suruali na jinzi ya bluu iliyopauka kidogo na na raba nyeupe. Juu alikuwa amevaa sweta yenye mistari mistari.

Nikamuangalia kisha nikajisemea kimoyo moyo "hawa ndio mafala wanaotugongea mademu zetu vyuoni, wanajifanya 'wajasiriamali' kumbe wazee wa kitengo".
Uzuri niliyasema hayo kimoyo moyo, nikamkata tu kijicho cha hasira kisha nikaangalia mlangoni tulikokuwa tunaelekea.

Yule dada akafungua mlango tukaingia ndani. Nilipokanyaga tu ndani kitu cha kwanza nilichokiona na kunishtua nusura nizimie haikuwa sebule kubwa ya kifahari, haikuwa seti za sofa zilizopangiliwa vizuri pale sebuleni, na wala haikuwa meza kubwa ya kioo katikati ya sebule.
Kitu cha kwanza nilichokiona na kunishitua mpaka karibu roho iruke, alikuwa ni Baba Bite. Alikuwa amevalia suti nyeusi na amekaa kwenye sofa la watu wawili na laptop mapajani.

Mshtuko nilioupata ilinibidi nisimame pale nilipokuwa ili nisiweze kudondoka. Maana mapigo ya moyo yalienda mbio kiasi kwamba ningepiga hatua moja tu ningeweza kudondoka. Nikabaki nimesimama tu namkodolea macho.

"Karibu sana Ray!" Baba bite akanisalimia kwa tabasamu na kusimama.

Kwa kipindi chote ambacho niliishi nae kule Morogoro Mazimbu siku zote Baba Bite alikuwa ni mtu mwenye furaha, lakini leo hii nilimuona na muonekano tofauti kabisa ambao sikuwahi kumuona nao kabla. Baba Bite niliyemuona leo alikuwa relaxed, alikuwa comfortable na alikuwa ana jiamini haswaa.

Nikatembea na kwenda kukaa kwenye sofa mojawapo ya watu wanne. Yule jamaa tuliyekuja naye aliyevakia suti nyeusi ambaye ndiye alikuwa anaendesha gari niliyokuwemo mimi akaja kukaa pembeni yangu. Baadae nilikuja kujua jina lake anaitwa Fredy.

Yule Afisa kijana wa makamo yangu ambaye baadae alikuja kutambulishwa anaitwa Hassani pamoja na yule Afisa aliyeendesha gari yangu ambaye baadae nikamfahamu anaitwa Mbena wakakaa kwenye sofa ya watu watatu.
Yule dada wa kitusi ambaye nilivyokuja kutambulishwa baadae jina lake sikuweza kulishika kichwani kutokana na lilivyokuwa gumu akaenda kukaa pale alipokaa Baba Bite lakini hakukaa kwenye sofa kabisa bali alikaa juu kwenye sehemu ya kuwekea mikono.

Zilipita karibia dakika tatu toka wote tuketi hakuna mtu aliyeongea chochote, nilikuwa nimekodoa macho tu kwa Baba Bite.

"Habari yako Ray" Baba Bite akavunja ukimya uliokuwa umetawala.

"Wewe Baba Bite ni Usalama wa Taifa??" Nikamuuliza kwa mshangao.

"Well, hilo ni swali au? Nadhani umeshaligundua hilo toka jana uliponishtukiza na maswali yako ya mtego" Baba Bite akanijibu huku anatabasamu. Nilichukia jinsi alivyokuwa relaxed ukinzingatia mimi nilikuwa katika paniki na mshangao mkubwa.

"Is that right? Ndio maana sikuwahi kukutata 'dukani kwako' hata siku moja. Ndio maana ulikuwa na taarifa ya kifo cha waziri kabla taarifa kufika kwenye media. Na ndio maana kwa miezi minane tuliyoishi pamoja ulijenga ukaribu na mimi. Kwa fikra za haraka haraka naamini muda wote huo ulikuwa unanichunguza! Swali language ni why? Kwanini Afisa wa Usalama wa Taifa upoteze miezi yote hiyo kunichunguza?" Nikamuuliza swali nikiwa katika hali ya utulivu. Taharuki na mshangao wangu vilikuwa vimeshaisha na sasa nilijisikia hali ya utulivu ndani ya nafsi.

"Well, hiyo naamimi ndio sababu kwanini wote tuko hapa! Why? Kwanini tukuchunguze? Ray, jibu lake ni jepesi tu.. Tunahitaji kujua uhusika wako kwenye kitu kinachoitwa The Board!!" Akaongea huku uso umebadilika ukiwa seruous kweli kweli hasa alipouliza swali la uhusika wangi kwenye The Board.

"Sifahamu chochote kuhusu The Board" nikamjibu kwa kujiamini. Sikutaka kutoa taarifa nisizokuwa na uhakika nazo kirahisi rahisi namna hiyo.

"Ray, nakuuliza kwa ustaarabu na kibinadamu kwa kuwa ni kijana ninayekufahamu! Nisingependa kutumia nguvu kupata hizo taarifa kutoka kwako" Baba Bite akaongea usoni akionyesha dhahiri ameanza kupatwa na hasira.

Mara simu ya mkoni ya yule dada wa kitusi ikaita. Wote tukanyamaza na nikaona wote wamegeuka kumuangalia yeye. Akapokea na kuweka sikioni.

"Hello!" Akaongea kwa lafudhi yake ya kinyarwanda.
"oui.. oui!" akamuitikia aliyekuwa anaongea naye kisha akakata simu na kuwatazama wenzake.
"le ministre est arrivé" (Waziri amewasili) akawaambia wenzake na kunyanyuka na kutoka nje.

Nikajiuliza kichwani, Waziri?? Waziri anakuja kwenye hiki kikao? Nikaacha nione kitakacho fuata!

Pia niligundua kuwa yule Dada anakielewa kiswahili ila hawezi kukizungumza kwani muda wote tunaongea alikuwa anafuatilia kwa makini na hakuna aliyekuwa anamtafasiria.

Dakika moja baadae akarejea akiwa ameongozana na Mhe. Charles Wangwe, Waziri wa Mambo ya Ndani.

Kama kawaida yake Mhe. Wangwe alikuwa amevalia suti nyeusi na shingoni amejifunga 'scarf' yenye rangi za bendera ya Taifa.
Alipoingia tu wote tukajikuta tumesimama mpaka mimi mwenyewe nikijikuta tu nimesimama. Mheshimiwa Wangwe ni moja kati ya viongozi wa nchi ninaowashimu sana na kuwahusudu, pia ni moja kati ya watu ninao waangalia kama mfano wa kuwaiga. Yes, nilikuwa natofautiana na baadhi ya misimamo yake hasa hasa kujipambanua kwake kwa itikadi za kichama, lakini alikuwa ananikosha kweli kweli kutokana na uzalendo wake na utendaji wake ambao binafsi nauona umetukuka.

Akatusalimia wote kisha akanifuata nilipokaa na kunipa mkono, "habari yako kijana" akanishika mkono.
"Nzuri tu, shikamoo Muheshimiwa" nikasalimia kwa bashasha nikifurahi kwa sekunde kadhaa nikisahau kuwa niko kwenye matatizo makubwa.

"Sijui nimechelewa? Mmefikia wapi" akauliza akiwa anakaa mahali ambapo Hassani yule Afisa kijana aliinuka na kumpisha.

"Hapana hujachelewa Muheshimiwa ndio tulikuwa tunaanza na Ray hapa anatueleza kuwa hafahamu chochote kuhusu The Board" akaongea Baba Bite huku anatabasamu.

Waziri Wangwe akatabasamu na kutoa kicheko fulani hivi kifupi kama 'anacheka kwa dharau' hivi lakini kwa sauti ndogo.

"Dogo mambo vipi" akaniangalia na kuniliza.
"Safi muheshiwa shikamoo" nikajikuta nimemuakia tena, damn it!

"Nadhani umesikia kuhusu kifo cha waziri wa nishati? Si ndio? Na tunafahamu kuwa kwa mara kadhaa umekuwa unakutana na mtu ambaye tuna hakika ni wakala wa The Board na jana tu ulienda gerezani kuonana Eric Kaburu gerezani! Sasa kabla hatuja kuunganisha kama moja ya watuhumiwa ni vizuri ukatupa maelezo ya kuridhisha" akaongea Waziri Wangwe kwa msisitizo na kwa mamlaka.

Nikajifikiria moyoni niwaeleze au niendelee kukataa? Nikahisi kuwa yaweza kuwa kosa kubwa kuongea hata kile kidogo ninachokifahamu kuhusu The Board. Lakini kwa upande mwingine nikakumbuka jinsi ambavyo mimi mwenyewe kwa siku mbili zilizopita jinsi nilovyoanza kuwa na mashaka makubwa kuhusu The Board. Na pia nikajipa moyo, kwanini niwafiche taarifa watu wa serikali na kuwalinda watu ambao Nina mashaka nao? Bora nimwage mchele tu.!

"OK! Nitaeleza kile ninachokifahamu" nikamwambia Waziri Wangwe.

Nikaanza kuwaeleza stori yote kuanzia ile miaka mitatu iliyopita. Jinsi nilivyopokea simu kwenye bahasha Morogoro ofisini. Jinsi walivyokuja nyumbani Mwembe Chai, jinsi nilivyopelekwa PPF House, jinsi walivyo nitoa damu na kuchukua alama za vidole. Nikawaeleza pia jinsi walivyonipeleka kwenye kikao chao Mikocheni B… Nilipowaeleza kuhusu kikao cha Mikocheni B niakona wameshtuka kidogo.

"Unataka kusema kuwa ulihudhuria kikao chao, unakumbuka wahudhuriaji walikuwa akina nani?" Baba Bite akaniuliza kwa shauku kubwa..

"Hapana sifahamu wahudhuriaji walikuwa akina nani, niliwekwa tu kwenye chumba fulani nikimsubiri Dr. Shirima." Nikamjibu huku nikificha kumwambia ukweli kuwa niliwang'amua wahudhuriaji wawili wa kikao usiku ule, Mbunge Zephania Zuberi na Mzee Bernard Shayo. Nikajisemea moyoni kuwa sio busara kuweka karata zangu zote mezani kwa wakati mmoja.

"Ok! Unakumbula hiyo nyumba ilikuwa wapi?" Akauliza Baba Bite huku kila mmoja wao akichukua peni na karatasi kuanza kuandika.

Nikawaelekeza mahali nyumba ilipo kule Mikocheni B. Baada ya kuwapa maelekezo hayo wakapeana ishara fulani hivi na nikawaona yule dada wa kitusi na yule Afisa aliyeiywa Mbena wakinyanyuka na kuondoka. Nikaamini wanafuatilia hiyo nyumba niliyowaelekeza.

"Enhe endelea" Baba Bite akanikumbusha kuwamalizia maelezo yangu.

Nikawaeleza kuhusu vikao vyangu na Dr. Shirima na nilipofikia kuwaeleza kuhusu vikao vyangu viwili vya mwisho, kile ambacho Dr. Shirima alinipa maelekezo kuhusu vijana wa kuwachagua kwenye programu ya Sote Hub kwa mwaka huu na pia kikao cha wiki mbili zilizopita ambapo alinipa maelezo ya kuwaombea tenda vijana hao, nilipowapa maelezo haya umakini wao uliongezeka nikagundua kuwa walikuwa hawajui suala hili. Hivyo wakaniuliza majina ya vijana hao nilioambiwa niwapitishe, majina ya kampuni zao na tender nilizowaombea. Nikawatajia na wakaandika kwenye makabrasha yao.

Baada ya hapo nikawaeleza kuhusu nilivyogundua namna ambavyo Ndeshema Safaris wanatoa msaada kwa Alice Cartz Foundation na hatimaye nikawaeleza kuhusu kumtembelea Eric Kaburi gerezani Morogoro na kitu alicho nijibu. Nikamaliza.

"Aiseeee!" Waziri Wangwe akashusha pumzi, "asante sana kijana kwa taarifa hii" akaongea huku anaendelea kuandika kwenye notebook yake.

"Umetuongezea vitu kadhaa ambavyo tulikuwa hatuvifahamu kuhusu The Board lakini pia la muhimu nadhani maelezo yako yanathibitisha ripoti ambazo alikuwa anatupa Justin (baba bite) kwamba wewe sio mwanachama wa The Board bali itakuwa wanakutumia tu" akaongeza Waziri Wangwe.

"Sijakuelewa Mheshiwa" nikamuuliza kwa uso wa alama ya kuuliza.

"Well, takribani mwaka mmoja umepita toka tugundue juu ya vikao vyako na Dr. Shirima ambaye tunamfahamu muda mrefu kuwa wakala wa The Board. Ndipo miezi minane iliyopita Justin akahamia mahali unapoishi kwa ajili ya kuchimba taarifa zako na baada kama ya miezi minne kwenye ripoti zake akatueleza kuwa wewe sio mwanachama wa The Board bali labda utakuwa unatumika tu so ni vizuri tusikuchukulie kama adui bali tukugeuze kuwa asset!" Akaongea Waziri Wangwe akimalizia kuandika kwenye notebook na kuniangalia usoni.

"Asset? Una maana gani kuwa niwe asset?" Nikauliza ingawa moyoni nilishakijua anachokimaanisha.

"Tunataka utusaidie kuichinguza The Board na tunaihitaji kufanya hivyo haraka sana!" Akaongea tena Waziri Wangwe.

"Kabla sijakubali au kukata hilo, sidhani kama The Board wataniamini tena, kwanza nimedukua akaunti ambayo nina amini wanahusika nayo, nimeenda kumuona Kaburu gerezani na niko hapa naongea na nyinyi watu wa serikali! Sidhani kama wataniamini tena" nikaongea kwa msisitizo kabisa nikiwakatisha tamaa kuhusu hoja waliyoiibua.

"Kuhusu sisi kukutana na wewe hawafahamu na hawawezi kufahamu tumejitahidi kuwa makini! Kuhusu kudukua taarifa za akaunti na kwenda kumuona Kaburu hawawezi kukutema kwenye mipango yao kwasababu hiyo! Naamini Dr. Shirima atakuita na kukukemea uache kufukunyua na mipango yenu itaendelea! Hawawezi kukutema kiraisi hivyo, naamini kutokana na kukuficha mambo yao wanexpect kijana mwenye utashi kama wewe ufukunyue mambo kuwafahamu" akaongea Waziri Wangwe akiwa na uhakika kabisa na kujiamini.

"Ok! Ok, kabla sijaanza kufikiria kuhusu hilo suala la kuwachunguza mnaweza kunieleza walau kidogo hawa The Board ni watu gani hasa maana nahisi mnawafahamu zaidi kuliko mimi"

"Ray sidhani kama kuna umuhimu wa kukupa taarifa ya namna hiyo"

"Mheshimiwa Waziri, kwa heshima zote kabisa naomba kukuambia kwamba nimewapa taarifa zote mnazohitaji na bado mnanitaka nianze kuwachunguza hao watu! Sasa nasema hivi, siwezi kuanza kuchunguza watu ambao siwafahamu na wala sifahamu ubaya wao! Kwa miaka mitatu hao The Board wanamtuma dokta kunipa maelekezo Fanya hiki fanya kile, lakini wameniweka gizani kuhusu shugjuli zao na unaweza kuona jinsi zilivyoniingiza kwenye majanga! Sasa na nyinyi mnataka kunituma kazi zenu na mnakuja na mtindo ule ule wa kutaka kuniweka gizani! sasa nasemaje, eidha niachieni niende nyumbani, au niswekeni rumande kama mtuhumiwa kama mlivyonitishia awali lakini nawahakikishia siwezi kufanya hicho mnachokitaka pasipo kunipa maelezo ya kutosha!!" Nikafoka kwa hasira nikimuangalia Waziri Wangwe.

Tukabakia tunaangaliana machoni kwa karibia nusu dakika.

"Justin naomba files za The Board" Waziri akamuagiza Baba Bite na Baba bite akainuka na kuingia chumba kimoja wapo mle ndani na dakika mbili baadae alirudi na mafailu kama saba hivi mkononi akayaweka mezani mbele ya Waziri Wangwe.

Waziri Wangwe akachukua faili moja na kulirusha mezani mbele yangu, nikalichukua na kuanza kufungua ndani kulisoma huku namsikiliza akinipa maelezo.

"The Board, hatufahamu mengi sana kuwahusu so nitakueleza machache tunayoyafahamu mpaka sasa" akaanza kunipa maelezo Waziri Wangwe
"Mtu ambaye tunahakika kwa asilimia mia kuwa ni mwanachama wao ni Dr. Shirima, mwalimu wa Uchumi Chuo Kikuu cha Mzumbe! IHuyu anatumiwa kama mtu wa mikakati na kuwa wakala wa kuwaunganisha The Board na vibaraka wao katika sekta mbali mbali. Na kuna watu watatu wengine ambao tume wafahamu hivi karibuni kuwa ni wanachama, wa kwanza ni Bernard Shayo naamini unamfahamu vizuri ni mmiliki vyombo vya habari Vingi hapa nchini… Vituo vya televisheni, vituo vya redio, magazeti na kampuno ya kusindika maji na soda. Mtu wa pili ni mfanyabiashara maarufu sana ambaye naamini unamfahamu na alikuwa mbunge kabla ya kujiuzuru miaka michache iliyopita, Bw. Khalid Mohammed na watatu ni Askofu Eliyah Kamei wa Uzima Ministries moja ya makanisa makubwa zaidi ya kilokole hapa nchini. Kwa hiyo hawa ndio watu wannepekee ambao tuna hakika kuwa ni wanachama wa The Board lakini kwa taarifa zetu za intelijensia tunaamini kuwa The Board ina wanachama wasiopungua ishirini na tano! Lakini taarifa zao ni za siri mno ila tunapambana usiku na mchana tuweze kuwatambua wanachama wao wengine na hasa hasa tunatamani kumjua kiongozi wao ambaye hatumjui jina bado ila wenyewe wanapenda kumuita Chairman "

Sikushangaa kuyasikia majina ya Dr. Shirima na Mzee Bernard Shayo kwani hawa nilikuwa nafahamu kuwa ni wanachama wa The Board lakini nilishtuka kusikia jina la Khalid Mohammed na nilipigwa na butwaa zaidi kusikia jina Askofu Eliyah Kamei wa Uzima Ministries.

Na pia nikawaza moyoni kuwa kumbe hawajui Mbunge Zephania Zuberi ni mwanachama pia wa The Board. Nikatamani kuwaambia lakini nikaimbia tena nafsi yangu kuwa si busara kuweka mezani karata zangu zote kwa wakati mmoja. Nikanyamaza na kuendelea kusikiliza maelezo ya Waziri Wangwe.

Waziri Wangwe akaendelea na maeleza, "tanahisi kuwa The Board ilianzishwa zaidi ya miaka arobaini iliyopita! Tunaami kuwa ilianza na wanachama kumi na mbili pekee na wamekuwa wakiongeza wanachama kwa kadiri ya mahitaji ya wakati husika. Tunaamini kuwa lengo lao kuu ni kushika uchumi wa nchi na kufanya ushawishi nchi iende vipi na ili kutekeleza malengo hayo wamekuwa wakiratibu matukio mengi makubwa katika nchi kwa miaka mingi sana"
Akaongea Waziri Wangwe na kuchukua faili lingine na kunirushia mbele yangu kwenye meza. Nikalichukua na kuanza kulipitia. Juu lilikuwa limeandikwa T.B. Strategy # 008. Waziri Wangwe akaamza kunipa maelezo.

"Tunaamini kuwa The Board kwa kushirikiana au kutumiwa na baadhi ya nchi za nje ndio walioratibu mpango mzima wa kuondoa sera na itikadi ya ujamaa nchini"

Akachukua faili lingine na kulirusha mbele yangu, hili lilikuwa limeandikwa T.B. Starategy # 0012. Waziri Wangwe akaendelea na maelezo.

"Tunaamini kuwa The Board ndio walioratibu mkakati wa kushusha thamani ya shilingi kwa mara ya kwanza kabisa na kusababisha mgogoro wa kiuchumi nchini mpaka mzee wetu kipindi kile akaachia madaraka kutokana na umaarufu wake kisiasa kushuka kutokana na kupingana na mipango hii. Usiniulize kushuka thamani ya shilingi iliwanufaisha vipi, baadae ukipitia hiyo file utapata majibu"

Akachukua faili lingine na kulirusha mbele yangu. Hili lilikuwa limeandikwa T.B. Strategy # 0021. Waziri Wangwe akaendelea na maelezo.

"Tunaamini kuwa kstika miaka ya tisini na elfu nbili mwanzoni The Board kwa kushirikiana au kutumiwa na IMF waliratibu mkakati wa ubinafsishaji wa viwanda, mali na mashirika ya umma nchini."

Akachukua tena faili lingine na kunirushia mbele yangu. Hili lilikuwa limeandikwa T.B. Strategy # 0031. Waziri Wangwe akaendelea tena na maelezo ila safari hii yalikuwa maelezo mafupi tu. Kwasababu nilipofungua faili na kutazama ndani nikakuta maelezo lakini juu take kulikuwa na picha ya kiongozi mstaafu. Nikainua macho kumuangalia Waziri Wangwe. Naye akaongea kwa kifupi tu,

"Uchaguzi mkuu 2005, tunaamini The Board walimuingiza huyo mgombea madarakani"

Nikainama kuangakia faili na kuangalia Picha ya yule kiongozi mstaafu. "Aiseeee!" Nikajikuta nimetaka neno hilo tu.

Waziri Wangwe akachukua faili lingine lakini safari hii hakunirushia mbele yangu kwenye meza bali akiendelea kulishikilia mkononi na kuanza kunipa maelezo.

"Tunaamini kuwa kwa miaka yote hii zaidi ya arobaini toka kuanzishwa kwa The Board wamekuwa wakitekeleza mkakati mmoja baada ya mwingine, hiyo niliyokuonyesha ni mifano ya mikakati michache tu waliyoitekeleza lakini tunaamini jumla ya mikakati hiyo ambayo wameitekeleza tayari mpaka sasa iko thelathini na tatu! Na kwa sasa wako wanatekeleza mkakati wa thalathini na nne" akaongea akinionysha lile faili alilolishika mkononi mwake.

"Dogo, sasa hapa ndio naomba unisikilize kwa makini kweli kweli maana ndipo tunapohitaji utusaidie"

Nikakaa sawa sawa kwenye sofa na kutega masikio yangu kwa shauku kubwa.

"Nakusikiliza Mheshimiwa!" Nikamwambia Waziri Charles Wangwe nikiashiria niko tayari kuyasikia hayo maelezo ya mkakati wa thelathini na nne na kitu gani wanataka nisaidie kukifanya.








Itaendelea….
 
NEW EPISODE (EPISODE 5) POST # 1115



Divine... glory to yhwh Nifah BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga succinate coA hydrogenase SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea Shareef Conscious wambeke The Boss deejay Nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly The Wolf Firegironsa everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Juma chief Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi @gambada YNWA @adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody King Easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 Mazigazi KIDUDU buffalo44 winlicious RIZIKI ALLYS MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo berbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome StraTon MemPhis GhaZar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga haa mym KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Blaki Womani erasto kalinga Chrizo kichakaa man kulubule FORTALEZA poleni Mshuza2 shibumi ZE DONE gkileo umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Clkey Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici T-King gkileo mij TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Mwangungulu marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 George Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom