@Faizafoxy bado yupo au alijitoa
Sina uakika haswa ni yupi mmojawapo anaejiita FaizaFoxy, lakini nahisi yupo.
Vitendo Saccos haijafanikiwa kabisa kuendelea kwa kukosa uongozi na zaidi ni kwa kanuni na shria za ushirika ambazo zunalazimisha kuwe na riba. Sisi tukashindwa kutilia mkazo kwa hilo kwani vitabu vya dini zetu vinatukataza kula riba. Pia . Ilikuwa ni one man show na jambo kubwa na zito kama hilo lilikuwa linahitaji watu wazoefu wenye mawazo chanya wa kuliendesha. Ni wazo jema sana
Mbadala wake sasa tunafanya kazi na biashara za kijamii, zambapo faida yote inayopatikana au niseme itayopatikana inarudi kuhudumia jamii. Ikisimamiwa na mimi binafsi na walioajiriwa tu, hatupo kama kikundi cha ushirika.
Tuna mipango mizuri sana, tumeianzisha na inaendelea vizuri.
1) Tumeanza na Madrassa ya Qur'an
2) Tumefanikiwa kubadili na kujenga msikiti kwenye banda ambalo hapo awali (wakati wa Vitendo Saccos) lilikuwa ni uwekezaji wa banda la Video, kuonesha mipira na movies.
3) Tumefanikiwa kuanzisha kijiji kinaitwa Village Abraar, ambapo mtu anaweza kujinunulia viwanja kwa gharama nafuu na malipo kidogo kidogo bila riba.
4) Tumefanikiwa kuanzisha darasa la ufundi wa kuunda vifaa vya ujezi na ujenzi kwa vitendo (practical). Linaendeshwa kwa pesa tunazouza viwanja na ha wanafunzi wanajifunza bure kabisa, bila malipo aina yoyote.
5)(Tumefanikiwa kuanzisha mpango wa Abraar Nyumba kwa Wote. Ambao ni wa kipekee duniani. Unaanza kujenga kwa kuanzia na kujiunga kwenye mpango huu kwa Shillingi 2,500 tu. Hakuna riba hakuna interest.
6) Pia tumeanzisha mpango wa Sadaka huanzia Nyumbani. Ambao umelenga sadaka zetu zianze kuelekezwa kwa watoto zetu na wake zetu nyumbani kwa kuwawekezea kwenye kuwajengea kwa kuanzia kuwalimbikizia Shillingi 2,500 tu/
Kumbuka kuwa Shillingi 2,500 zinakununulia "jiwe la msingi" la kuanza ujenzi. Inakuwa umeshajijenga kisaikolijoia kuwa umeanza ujenzi. Na sisi hapa Abraar tunakuwa tumeshapata mteja.
Abraar hakuna longo longo, kila kitu kimenyooka. Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi 0625249605 Abdul Ghafur.
@Faizafoxy bado yupo au alijitoa