Mto Songwe
JF-Expert Member
- Jul 17, 2023
- 6,408
- 13,198
Ndio inaweza onekana kauli ya kushangaza lakini ndio ukweli halisia kwa asilimia nyingi tu.
"Viongozi wetu ndio picha halisi ya jamii yetu"
Kwa asilimia kubwa viongozi wetu wanawakilisha tamaduni,malezi,tabia na fikra za watu wa jamii yetu kwa kiwango kikubwa.
Vile wafikiriavyo viongozi wetu, vile watendavyo viongozi wetu ndilo kundi kubwa la jamii yetu hufanya hivyo ni kundi dogo sana ndani ya jamii yetu lililo tofauti na tabia za wanajamii wengi ambao pia viongozi wetu wamo.
Namna walivyo viongozi wa jamii au mataifa ya wazungu ndivyo ilivyo jamii ya kizungu kufikiri,kutenda,malezi, tamaduni na mienendo.
Namna walivyo viongozi wa jamii/mataifa ya waarabu ndivyo hivyo jamii ya waarabu inavyo enenda kwa kiasi kikubwa.
Namna walivyo viongozi wa jamii au mataifa ya Asia China, Korea, Japan ndivyo walivyo watu wa jamii hiyo katika kuwaza na kutenda.
Namna walivyo viongozi wa CCM Tanzania ndivyo walivyo viongozi wa Chadema,ACT, CUF n.k na ndivyo walivyo Watanzania wengi kutenda, kunena, kufikiri, tabia, malezi, tamaduni na mfumo mzima wa kimaisha.
Vita dhidi ya hali yetu tuliyo nayo haiwezi kuwa nyepesi kwa sababu jamii yetu kubwa ipo kama walivyo wale wanao tuongoza sasa. Wenye fikra mpya,malezi tofauti, tamaduni tofauti na mfumo mzima wa maisha tofauti na jamii ni wachache sana.
"Viongozi wetu ndio picha halisi ya jamii yetu"
Kwa asilimia kubwa viongozi wetu wanawakilisha tamaduni,malezi,tabia na fikra za watu wa jamii yetu kwa kiwango kikubwa.
Vile wafikiriavyo viongozi wetu, vile watendavyo viongozi wetu ndilo kundi kubwa la jamii yetu hufanya hivyo ni kundi dogo sana ndani ya jamii yetu lililo tofauti na tabia za wanajamii wengi ambao pia viongozi wetu wamo.
Namna walivyo viongozi wa jamii au mataifa ya wazungu ndivyo ilivyo jamii ya kizungu kufikiri,kutenda,malezi, tamaduni na mienendo.
Namna walivyo viongozi wa jamii/mataifa ya waarabu ndivyo hivyo jamii ya waarabu inavyo enenda kwa kiasi kikubwa.
Namna walivyo viongozi wa jamii au mataifa ya Asia China, Korea, Japan ndivyo walivyo watu wa jamii hiyo katika kuwaza na kutenda.
Namna walivyo viongozi wa CCM Tanzania ndivyo walivyo viongozi wa Chadema,ACT, CUF n.k na ndivyo walivyo Watanzania wengi kutenda, kunena, kufikiri, tabia, malezi, tamaduni na mfumo mzima wa kimaisha.
Vita dhidi ya hali yetu tuliyo nayo haiwezi kuwa nyepesi kwa sababu jamii yetu kubwa ipo kama walivyo wale wanao tuongoza sasa. Wenye fikra mpya,malezi tofauti, tamaduni tofauti na mfumo mzima wa maisha tofauti na jamii ni wachache sana.