Viongozi wakuu wa nchi mnatuchanganya Wananchi tunaomba mjiuzulu nafasi zenu

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,675
40,926
Wakati Rais Magufuli akiwa madarakani tuliwaona mkiandamana nae kila mahali katika ufunguzi wa miradi mbalimbali.

Na wakati mkiandamana naye mlipata nafasi ya kutoa neno na katika kufanya hivyo mliisifia miradi na kutuambia kuwa iko sawa kabisa, tuliwaamini kwakua nyie ndio mliyobeba dhamana yetu kwa nafasi mlizopo.

Vilevile wakati CAG anatoa ripoti zake, hatukuwahi ambiwa kuwa hiyo miradi haifai bali tumekua tukisikia tu kuwa kila kitu kipo sawa. Sasa ghafla baada ya Dr. Magufuli kututoka tunaona kauli tofauti na zile za awali toka kwa watu wale wale.

Binafsi naamini kabisa kwa nafasi zao watu hao walikuwa wasaidizi na kwa namna flani washauri wa Rais kwa mambo mbali mbali, watuambie ni mambo mangapi katika haya tunayoyaona walimshauri Rais vibaya.

Je, majukumu ya CAG ni pamoja na kurecommend umuhimu wa mradi au yanaishia kwenye mahesabu tu?

Ndio kusema kwamba CAG amejitwika majukumu yasiyokuwa yake?

Au kama hayo ndio majukumu yake kwanini ripoti yake ya mwaka jana haikuwa na mambo kama haya, nia ya CAG hasa ni nini?

Mimi nawashauri kama raia mwaminifu ili wasiendelee kutuchanganya kwa kauli ambazo naona kama hazina tija sana kwa kulikuza taifa letu wajiuzulu au Rais awasaidie.

Binafsi naona ni vyema tukajikita kwenye kufanya kazi kuliko kuambiana yaliyopita na ili hayo yafanyike waliopo wajiuzulu nafasi zao.

Rais ateue watu wapya watakaoendana na vision yake.
 
"Binafsi naona ni vyema tukajikita kwenye kufanya kazi kuliko kuambiana yaliyopita na ili hayo yafanyike waliopo wajiuzulu nafasi zao." wacha tujue kwa undani uozo ili tusiharibikiwe tena.
 
CAG hasemi madudu yaliyopita bali huo ni utaratibu uliopo katika kuipa dira nchi na muelekeo ulio sahihi,CAG ni sawa na kioo kinachomulika uchafu ivyo kusema ivyo ni lazima ili kujua tupo wapi kama nchi na wapi tunaelekea.

Kuhusu kwa nn RAIS hakushauriwa ,ww mwenyewe unajua RAIS alikua mtu wa aina gani refer case ya CAG aliyepita JUMA ASSAD....kwahiyo siyo kosa la hao washauri bali ni kiongozi aliyekuepo madarakani.
 
Je, majukumu ya CAG ni pamoja na kurecommend umuhimu wa mradi au yanaishia kwenye mahesabu tu?

Ndio kusema kwamba CAG amejitwika majukumu yasiyokuwa yake?
Ni kazi ya Auditor kukagua hesabu na kutoa independent opinions.

Kwahiyo hapa kwenye football tunasema ametembea na "chaki" , sema kama mwezi huu utaisha bila waliohusika ama kuresign au kuwajibishwa basi ni vyema hiyo report tusiwe tunapewa yaani ni aibu kubwa kwakweli kwasababu tuliamini kila kitu kilikuwa sawa.
 
CAG hasemi madudu yaliyopita bali huo ni utaratibu uliopo katika kuipa dira nchi na muelekeo ulio sahihi,CAG ni sawa na kioo kinachomulika uchafu ivyo kusema ivyo ni lazima ili kujua tupo wapi kama nchi na wapi tunaelekea.....kuhusu kwa nn RAIS hakushauriwa ,ww mwenyewe unajua RAIS alikua mtu wa aina gani refer case ya CAG aliyepita JUMA ASSAD....kwahiyo siyo kosa la hao washauri bali ni kiongozi aliyekuepo madarakani.
Hapana akina Ndugai waliwafukuza akina Mbowe, Lema n.k ambao walikuwa wanasema ukweli, hawa ni wanafiki wakubwa.
 
Waachie ngazi? Are you serious! Kuna kula hapo, mikataba itaangaliwa upya! Wataachia ngazi mpaka waanze kutapika $$$$$$$$. Eti wanatutumikia, I can’t even understand wanapokula viapo vya maadili. Wamemuua JPM ili turudi tulikozoea Alikuwa mgonjwa for 4 weeks, tukaambiwa yuko hai. Kumbe yuko kwa mzena in palliative care.alikuwa saa 12, tukatsngziwa saa 5 usiku, 5 hours what were they doing.
 
Ni kazi ya Auditor kukagua hesabu na kutoa independent opinions.

Kwahiyo hapa kwenye football tunasema ametembea na "chaki" , sema kama mwezi huu utaisha bila waliohusika ama kuresign au kuwajibishwa basi ni vyema hiyo report tusiwe tunapewa yaani ni aibu kubwa kwakweli kwasababu tuliamini kila kitu kilikuwa sawa.
Hawa wapumbavu ndiyo maana wanatuita wanyonge wanapiga pesa na hatuna cha kuwafanya.
 
Waachie ngazi? Are you serious! Kuna kula hapo, mikataba itaangaliwa upya! Wataachia ngazi mpaka waanze kutapika $$$$$$$$. Eti wanatutumikia, I can’t even understand wanapokula viapo vya maadili. Wamemuua JPM oil turudi lile tulikoze. Alikuwa mgonjwa for 4 weeks, tukaambiwa yuko hai. Kumbe yuko kwa mzena in palliative care.alikuwa saa 12, tukatsngziwa saa 5 isolines. 5 hours what were they doing.
Hawa wapumbavu inatakiwa tuandamane tuwakatae mara moja.
 
Waachie ngazi? Are you serious! Kuna kula hapo, mikataba itaangaliwa upya! Wataachia ngazi mpaka waanze kutapika $$$$$$$$. Eti wanatutumikia, I can’t even understand wanapokula viapo vya maadili. Wamemuua JPM oil turudi lile tulikoze. Alikuwa mgonjwa for 4 weeks, tukaambiwa yuko hai. Kumbe yuko kwa mzena in palliative care.alikuwa saa 12, tukatsngziwa saa 5 isolines. 5 hours what were they doing.
Mzee wa Mwime Nyasubi wanasemaje?
 
Hivi aliyepita alikuwa anashaurika? Msiwalaumu tu washauri. Jiulizeni kama mshauriwa alikuwa tayari kushauriwa. Ila mimi nakumbuka alitwambia kuwa ukimshauri ndio umeharibu kabisa.
 
Hivi aliyepita alikuwa anashaurika? Msiwalaumu tu washauri. Jiulizeni kama mshauriwa alikuwa tayari kushauriwa. Ila mimi nakumbuka alitwambia kuwa ukimshauri ndio umeharibu kabisa.
Kwa maelezo ya spika jana naunga mkono hoja.
 
Wajiuzulu nani na nani?!!!
Viongozi wote wanaohold public ofice,

Wampe nafasi Rais ateue watu wapya hao wapya hata wakiongea italeta maana kuliko wale wale kuja na kauli tofauti na za awali.

Mkuu utajisikiaje mfano akija DPP akasema ni kweli kulikua na kesi za kubumba wakati ni yeye hapo awali ndio aliona zinafaa kupelekwa mahakamani?? Think.
 
Ni kazi ya Auditor kukagua hesabu na kutoa independent opinions.

Kwahiyo hapa kwenye football tunasema ametembea na "chaki" , sema kama mwezi huu utaisha bila waliohusika ama kuresign au kuwajibishwa basi ni vyema hiyo report tusiwe tunapewa yaani ni aibu kubwa kwakweli kwasababu tuliamini kila kitu kilikuwa sawa.
Mkuu ni wewe kweli.
 
Back
Top Bottom