Viongozi wa CHADEMA kutokumtambua Rais ni Kosa?

Democrasia

Member
Feb 1, 2008
79
3
Jamani nilikuwa naomba kujua kama kuna madhara yoyote yanayoweza kuwapata wabunge wa CHADEMA NA WANACHADEMA kwa ujumla kwa kutomtambua Raisi.
Naomba kuwasilisha
 
sio kosa maana hata wtz %72 hawamtambui na hakuna madhara.

na leo natamani wasiingie mara huyu jk atakopofika mjengoni

watoke nje na kuanza kucheza bao au karata
 
Hakuna sheria inakatiza mtu kusema kuwa hatomtambua rais. Lakini kama rais ametangazwa na tume ya uchaguzi kutokumtambua hakutakuwa na nguvu kisheria kwa sababu hakuna mahakama yeyote yenye mamlaka ya kuchuguza kuchaguliwa kwake kwa mujibu wa ibara 42(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Ibara hii iliwekwa makusudi kwani walikuwa madarakani walijua kuna wakati watahitaji kuchakachua matokeo.
 
Hao CHADEMA hovyo sana! Kama kweli hawamtambui basi sharti wasiingie bungeni na wasichukue ile hela ya posho wala pesaingine manake itakuwa kama wanachukua kutoka serikali wasioitambua!! Yule kiongozi wa upinzani bunge lililopita aliwaambia hivyo kwani wao CUF hawaku ingia baraza la wakilishi mpaka muafaka ulivyofikiwandipo wakarudi barazani na kuanza kuchukua fweza.

Namna gani hii!!!!????
 


a typical ignoramus!
 
Wabunge wa CHADEMA wametoka kwenye ukumbi wa Bunge ila wameonekana wakitazama TV (Runinga) hotuba ya JK , sasa hapo haumtambui kivipi ili hali unamsikiliza ? si ni bora ungekaa tu ukumbini ukamsikiliza vizuri Mh. Rais
 
HAHAHAH WAMEMWAIBISHA RAIS WAKO MBELE YA WAGENI WAKE....
KWANI KUANGALIA MTU AKIONGEA KWA TV NI KOSAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA:doh:
 
Katika hali iliyokuwa ya kubeza Kikwete awaambia Wapinzani kwamba hata wasipomtambua wasisahau kwamba watahitaji ushirikiano wa Serikali iliyopo madarakani ili kuweza kuleta maendeleo katika Majimbo yao na kusisitiza kuwa na Serikali hiyo yeye ndio Rais wake.

Maana yake ni kwamba itabidi wamtambue ndio wataweza kupata ushirikiano. Sounds like a blackmail!!
 
Wabunge wa CHADEMA wametoka kwenye ukumbi wa Bunge ila wameonekana wakitazama TV (Runinga) hotuba ya JK , sasa hapo haumtambui kivipi ili hali unamsikiliza ? si ni bora ungekaa tu ukumbini ukamsikiliza vizuri Mh. Rais

Karibu JF.

Hongera kwa kujiunga leo.

Bahati mbaya umeanza kwa hoja nyepesi.
 
hiyo ni ku send signal kwa serikali kuwa wali-chakachua ,hivyo hata baadaye watakuwa makini kufanya madudu kama hayo....
bravo Chadema
 
Alipaswa kujipa angalizo yeye na chama chake kwanza kabla ya kutishia 'wanaume'
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…