Tupo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida kwa kamanda Mkoa Linus Vincent Sinzumwa, kusubiri Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika na Dr. Kitila Mkumbo kuhojiwa kuhusu fujo zilizotokea Kijiji cha Ndago, Wilaya ya Iramba wiki iliyopita. Hata hivyo baada ya viongozi hawa kufika mapema kadiri ya muda walioambiwa na RPC huyo, Polisi wameshindwa kuanza mahojiano na viongozi hawa kwa kile kilichosemwa kuwa ni kuwasubiri Makamishna na Makachero kutoka makao makuu ya jeshi la Polisi toka Dar es Salaam. Jana jioni Mtuhumiwa muhimu ambaye alitambulishwa kwa jina moja la Msamaria, Pamoja na mwingine ambaye anajulikana kama Tito, ambao wanahusiswa au kutajwa sana kuwa ndio waliosababisha fujo kubwa zilizopelekea kifo cha mtu mmoja, bado vijana hawa walionekana wakirandaranda nje hata Polisi hawajawakamata, ukiachilia mbali wale ambao kwa sasa tunaweza kusema ndio waliokodishwa toka Dar kuletwa Singida na CCM. Viongozi wa CCM bado wanahaha kuwawekea dhamana hao vijana wa Dar es Salaam, walihojiwa na kusema eti ni wafanyabiashara: Jana ilishindikana, sijui kama leo inawezekana vijana waliosababisha ndugu kuuana kwa fujo walizosababisha. Ndugu zao wapo Dar, lakini wao wakatoka kuja huku kwa ujira kwa nia ya kuua. Ndio kazi ya Katibu wa Uchumi na fedha. Pesa za CCM NDO MATUMIZI YAKE HAYA? TUENDELEE KUULIZA UHUSIANO ULIOPO KATI YA CCM NA VIJANA SABA WALOSABABISHA FUJO MKUTANO WA CHADEMA AMBAO NI:Abdala Mbwana Kingwande, (Mndengereko), ana Miaka 36, Mwislamu, Mfanyabiashara na Mkaazi wa Segerea Dar es Salaam. wa Pili Ni Nasri Salehe (Mnyamwezi), ana umri 28, Mwislamu, anakaa karikaoo, na ni mfanyabiashara. Wa tatu ni Laizimu Njama, ni MMakua, ana miaka 42, Mwislamu, anatokea Tandika/Temeke Dar es salaam. wa Nne ni Mohamedi Abdalaa, Mluguru, ana miaka 34, Mwislamu, anakaa Kibamba Dar es Salaam, wa Tano ni Rudoviki Muganyizi, Mhaya, ana miaka 32, Mkristo, Ni Injinia. Wa Sita ni Justini Sangu, Mfipa, ana miaka 40, Mkristo anakaa Dar na ni mfanya biashara. wa Saba ni Salumu Ali Rashidi, ni Mmwela, ana miaka 26, Mwislamu, ni Mkaazi wa Tandika Jijijini Dar. Nitaendelea kuwajuza yanayojiri, ngoja tuwasubiri hao wa makao makuu kama wanakuja na kipya ambacho wa Singida waliokuwa kwenye eneo la tukio hawakijui.