Malaria Sugu
JF-Expert Member
- Jul 7, 2009
- 2,653
- 264
Nimekusoma mkuu, kama hivyo ni vema , isije kuwa wamepewa maelekezo toka IKULU
maelekezo yaketoka pale kinondoni manyanya yalipo makao makuu yatu.
Nimekusoma mkuu, kama hivyo ni vema , isije kuwa wamepewa maelekezo toka IKULU
Mkuu Kitila Mkumbo,There are currently 51 users browsing this thread. (21 members and 30 guests)
Tunataka kumbananisha OCS na askari wake wanaotajwa kuona vurugu zikianzishwa na kikundi hicho cha kukodi lkn wasichukue hatua,so muhimu kina mnyika na watoe maelezo/ushuhuda wao namna ilivokuwa.Nina habari Mwema kashachoka kupakaziwa anataka kufanya real
]Mkuu [/COLOR]Kitila Mkumbo,
Tunakuona upo online kwenye thread. Tunaomba utupe update kinachojiri huko.
TUMBIRI (PhD, University of HULL - Hull City, UK),
tumbiri@jamiiforums.com
hapo kwenye red,kwanini umeenda kuua ndugu zako???
huoni hiyo ni laana kwa mungu??
Policeccm na filamu za kova..... Hao ccm walifuta nini mkutano wa chadema, ajabu wanabebana na viongozi wao?
Ahsante kwa taharifa....ila sijapenda ulivyotaja majina ya hao watu kwa dini na makabila yao.
Sijaona umuhimu wowote wa kutaja hivyo vitu.
Mnyika alitoke Dar. Tutumie hizi kidogo tulizonazo.Hao watu wa Dar lazima watakuwa wamekuja huko na msafara wa Mnyika, ss huoni kwamba hao ni CDM?
Hao watu wa Dar lazima watakuwa wamekuja huko na msafara wa Mnyika, ss huoni kwamba hao ni CDM?
Tupo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida kwa kamanda Mkoa Linus Vincent Sinzumwa, kusubiri Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika na Dr. Kitila Mkumbo kuhojiwa kuhusu fujo zilizotokea Kijiji cha Ndago, Wilaya ya Iramba wiki iliyopita.
Itabidi hao kwenye red waunganishwe na watuhumiwa wenzao
Usipate shida anzeni kumkamata OCD.....La sivyo mtaumbuka
Hii nimeipata humu…. NOLNIZ
Mimi ni mtumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Kiomboi, Singida katika idara ya elimu. Nilishiriki katika mikutano miwili ya CHADEMA iliyofanyika Ndago na Kinampanda na nilishiriki kupokea msafara kuanzia Mbelekese.
Ukweli ni kwamba utaratibu wa kuvuruga mikutano ya CHADEMA uliandaliwa mapema kwa kuwashirikisha OCD, Mkuu wa Wilaya na Mbunge wa Iramba Magharibi, na jambo hili tuliwaeleza viongozi wa CHADEMA kabla hawajafika Ndago. Mpango uliokuwepo na utakaokuwepo katika mikutano ya leo ni kuwaandaa vijana wasio pungua 50 wakiwa
wamelewa chakari. Wao kazi yao ni kuhakikisha kwamba viongozi wa CHADEMA hawahutubii mikutano na wakijifanya hawaelewi basi mawe yapopolewe. Jambo hili halijawafurahisha watumishi wengi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wanaopenda haki, na kuna malumbano makali yanaendelea chini kwa chini.
Sasa jana, mara msafara ulipofika Ndago na kabla mkutano haujafunguliwa wale vijana walikuwa wamekaa pembe tatu tofauti nyuma ya Mnyika, mbele kabisa karibu na barabarani na kushoto wakiwa wamejichanganya na maaskari. Lengo ilikuwa ni kumlenga mawe Mnyika moja kwa moja ili ionekana kwamba hatakiwi kabisa Iramba. Bahati nzuri aliposimama Waitara akaanza na tahadhari kali sana kwamba tunafahamu mipango yote haramu na akawaambia maaskari wanawajibika kulinda mkutano kwa sababu mkutano ni halali na una baraka zote za Jeshi la Polisi.
Moja ya wale vijana alimpigia simu Mwigulu kwamba mpango wao umeingia mkenge kwa sababu jamaa wa CHADEMA wanaujua mpango mzima. Mwigulu alimfokea yule kijana kwa ukali sana na akamwambia anataka kuona mawe yanapigwa ndani ya dakika tano vinginevyo ajiandae. Moja kwa moja yule kijana akawaambia wenzake kwa ishara na wakatoa mawe mfukoni wakaanza kurusha. Purukushani ziliendelea na vijana wa CHADEMA wakawa wanajihami na kuwalinda viongozi waliokuwepo kwa karibu kabisa.
Vurugu ziliendelea kwa takribani kati ya dk 20-30, na wananchi wengi kusambaratika. Waitara na Mnyika walionekana wakiwasiliana kwa simu na kuwalaumu polisi waliokuwepo, ambao wao walikuwa wanachekacheka tu. Ndipo utulivu ukarejea na wananchi walirudi kwa kasi ya ajabu, na mkutano ukajaa tena na Mnyika akaendelea kuhutubia. Mnyika alipokuwa anamalizia hotuba yake, ndipo landrover ya FFU ikaingia ikiwa imesheheni maaskari. Mnyika akawaambia wananchi kwamba maaskari wameingia lakini baada ya fujo kutokea na wananchi wamejilinda wenyewe.
Mkutano uliisha kwa amani, na kisha msafara ukaelekea Kinampanda palipokuwa na Mkutano mwingine. Tukiwa pale Kinampanda ndipo habari zikaanza kusambaa kwa kasi kwamba kuna kijana ameuawa. Mkutano wa Kinampanda uliisha salama na hapakuwa na kurushwa mawe. Wananchi walihudhuria kwa wingi ukizingatia pale ndipo palipo Chuo cha Ualimu cha Kinampanda. Taarifa nilizozipata baadaye ni kwamba yule kijana aliuawa ndani ya nyumba ya mtu kando kidogo na mkutano ulipokuwa unafanyika. Mtu huyo pia anatajwa kuwa kada wa CCM aliyekuwa anagombea ukatibu kata na ndiye aliyepewa fedha na Mwigulu kuratibu shughuli nzima ya fujo.
Sina uhakika kama mikutano ya leo ya CHADEMA itafanyika kwa sababu vijana wameshaanza kukamatwa na kuna hatari polisi wakazuia mikutano ya leo. Pamoja na yote haya, Mwigulu watu wanamchukia sasa hivi kwa mambo ya kihuni anayoyafanya. Hatujuwahi kuwa na Mbunge wa namna hii katika Jimbo hili".
Hao watu wa Dar lazima watakuwa wamekuja huko na msafara wa Mnyika, ss huoni kwamba hao ni CDM?
kwanini sio wale waliosababisha mauaji akina mwita na mnyika.au unataka kupindisha ukweli
Tumefika Hapa Tulipo Kwa Sababu Ya Udhaifu Wa Rais Kikwete, Kwa Uzembe Wa Bunge, Na Kwa Sababu Ya Upuuzi Wa CCM-Mnyika John Mnyika.
Kwa hili hata mimi sifuti kauli hii kwani ina ukweli usiopingika.