Hmaster
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 346
- 86
Kwanza kabisa napenda kuanza kwa kuwapa pongezi kwa kazi kubwa mnayoifanya kusini mwa nchi yetu kwa sababu kwa kufanya hivyo tunaendelea kujihakikishia kushika dola hapo 2015.
Pamoja na pongezi hizo ningependa kujua msimamo wa CHADEMA kuhusu rangi za bendera ya chama kipya cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE (ADC) kufanana sana na za bendera ya CHADEMA.
Nakumbuka sana wakati chama hicho kinapata usajili wa muda hata msajili wa vyama vya siasa nchini mh. Tendwa aliliona na alilitolea ufafanuzi na kusema kwamba anasubiri kama ataletewa malalamiko na chama chochote alishughurikie kwa mujibu wa sheria.
Wakati usajili unafanyika vikao vya bunge vilikuwa vinaendelea na hivyo nilitegemea kwamba vitakapokwisha lingeshughurikiwa lakini hadi leo wahusika wakuu wakiwa ktk movement kusini sijasikia chochote kuhusu hilo.
Wasiwasi wangu ni endapo chama hicho kitapata usajili wa kudumu wakiwa na bendera hiyo kwamba inaweza katika nyakati za uchaguzi kuwachanganya wapiga kura na hasa wale ambao mara nyingi huangalia rangi za bendera tu na kufannya maamuzi.
NINGEFURAHI KAMA NINGEPATA UFAFANUZI JUU YA HILI; People's Power!
Pamoja na pongezi hizo ningependa kujua msimamo wa CHADEMA kuhusu rangi za bendera ya chama kipya cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE (ADC) kufanana sana na za bendera ya CHADEMA.
Nakumbuka sana wakati chama hicho kinapata usajili wa muda hata msajili wa vyama vya siasa nchini mh. Tendwa aliliona na alilitolea ufafanuzi na kusema kwamba anasubiri kama ataletewa malalamiko na chama chochote alishughurikie kwa mujibu wa sheria.
Wakati usajili unafanyika vikao vya bunge vilikuwa vinaendelea na hivyo nilitegemea kwamba vitakapokwisha lingeshughurikiwa lakini hadi leo wahusika wakuu wakiwa ktk movement kusini sijasikia chochote kuhusu hilo.
Wasiwasi wangu ni endapo chama hicho kitapata usajili wa kudumu wakiwa na bendera hiyo kwamba inaweza katika nyakati za uchaguzi kuwachanganya wapiga kura na hasa wale ambao mara nyingi huangalia rangi za bendera tu na kufannya maamuzi.
NINGEFURAHI KAMA NINGEPATA UFAFANUZI JUU YA HILI; People's Power!