Viongozi 500 kutoa heshima za mwisho kwa Malkia leo

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,553
Rais wa Marekani Joe Biden na Samia Suluhu wa Tanzania ni miongoni mwa viongozi waliowasili jijini London tayari kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabeth II siku ya Jumatatu.

Viongozi hao ni miongoni mwa wakuu na viongozi 500 wa kigeni wanaokuja London kwa tukio linalowakutanisha viongozi wa ulimwengu wengi zaidi kuonekana kwa pamoja kwa miongo kadhaa.

Mawaziri wakuu wa Canada, Australia na New Zealand tayari wako Uingereza.

Mzozo unazingira baadhi ya wageni waalikwa, kama vile Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed Bin Salman.

Mbali na Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau, Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese na Waziri Mkuu wa New Zealand Jacinta Ardern, viongozi wengine wa Jumuiya ya Madola wanaotarajiwa kuhudhuria ni pamoja na Waziri Mkuu wa Bangladesh Sheikh Hasina na Rais wa Sri Lanka Ranil Wickremesinghe.

India itawakilishwa na Rais Droupadi Murmu.

Viongozi walioalikwa leo watapata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho huko Westminster na kutia saini kitabu cha maombolezo.

Mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabethi II yatafanyika kesho Jumatatu Westminster Abbey, London, kabla ya mwili wake kulazwa kwenye kasri la Windsor.

BBC
 
Rais wa Marekani Joe Biden na Samia Suluhu wa Tanzania ni miongoni mwa viongozi waliowasili jijini London tayari kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabeth II siku ya Jumatatu.

Viongozi hao ni miongoni mwa wakuu na viongozi 500 wa kigeni wanaokuja London kwa tukio linalowakutanisha viongozi wa ulimwengu wengi zaidi kuonekana kwa pamoja kwa miongo kadhaa.

Mawaziri wakuu wa Canada, Australia na New Zealand tayari wako Uingereza.

Mzozo unazingira baadhi ya wageni waalikwa, kama vile Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed Bin Salman.

Mbali na Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau, Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese na Waziri Mkuu wa New Zealand Jacinta Ardern, viongozi wengine wa Jumuiya ya Madola wanaotarajiwa kuhudhuria ni pamoja na Waziri Mkuu wa Bangladesh Sheikh Hasina na Rais wa Sri Lanka Ranil Wickremesinghe.

India itawakilishwa na Rais Droupadi Murmu.

Viongozi walioalikwa leo watapata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho huko Westminster na kutia saini kitabu cha maombolezo.

Mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabethi II yatafanyika kesho Jumatatu Westminster Abbey, London, kabla ya mwili wake kulazwa kwenye kasri la Windsor.

BBC
Ungesema tu Biden atawaongoza wenzie kwenye kuzika....
 
Sawa,tuombe Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Yafaa nini ukizikwa na watu milioni mia lakini ukaipoteza roho yako? Tuombe mwisho mwema.
 
Rais wa Marekani Joe Biden na Samia Suluhu wa Tanzania ni miongoni mwa viongozi waliowasili jijini London tayari kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabeth II siku ya Jumatatu.

Viongozi hao ni miongoni mwa wakuu na viongozi 500 wa kigeni wanaokuja London kwa tukio linalowakutanisha viongozi wa ulimwengu wengi zaidi kuonekana kwa pamoja kwa miongo kadhaa.

Mawaziri wakuu wa Canada, Australia na New Zealand tayari wako Uingereza.

Mzozo unazingira baadhi ya wageni waalikwa, kama vile Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed Bin Salman.

Mbali na Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau, Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese na Waziri Mkuu wa New Zealand Jacinta Ardern, viongozi wengine wa Jumuiya ya Madola wanaotarajiwa kuhudhuria ni pamoja na Waziri Mkuu wa Bangladesh Sheikh Hasina na Rais wa Sri Lanka Ranil Wickremesinghe.

India itawakilishwa na Rais Droupadi Murmu.

Viongozi walioalikwa leo watapata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho huko Westminster na kutia saini kitabu cha maombolezo.

Mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabethi II yatafanyika kesho Jumatatu Westminster Abbey, London, kabla ya mwili wake kulazwa kwenye kasri la Windsor.

BBC

17 September 2022

RAIS SAMIA ASHIRIKI MAZISHI YA MALIKIA ELIZABETH II


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili jijini London, Uingereza kwa ajili ya kushiriki shughuli rasmi ya msiba wa Malkia Elizabeth II.

Siku ya Jumapili, viongozi mbalimbali walioalikwa akiwemo Rais Samia watatoa heshima zao za mwisho kwa Marehemu kwenye eneo la Westminster Hall ambapo pia atatia saini kitabu cha maombolezo.

Baada ya hatua hiyo Rais Samia atahudhuria hafla fupi ilioandaliwa na aliyetamkwa kuwa Mfalme Charles III ambaye amemrithi mama yake Marehemu Malkia Elizabeth II.

Hafla hiyo ambayo pia imeandaliwa na Malkia Mfariji (Queen Consort), Camilla Parker Bowles itafanyika katika Kasri ya Buckingham jijini London.

Aidha, siku ya Jumatatu, Rais Samia atahudhuria Mazishi ya Kitaifa ya Malkia Elizabeth II yatakayofanyika kwenye Kanisa la Westminster Abbey. Mwili wa Malkia Elizabeth utalazwa kwenye kasri la Windsor

Source : 17 | September | 2022 | Blogu Rasmi ya Ofisi ya Rais
 
Rais wa Marekani Joe Biden na Samia Suluhu wa Tanzania ni miongoni mwa viongozi waliowasili jijini London tayari kuhudhuria mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabeth II siku ya Jumatatu.

Viongozi hao ni miongoni mwa wakuu na viongozi 500 wa kigeni wanaokuja London kwa tukio linalowakutanisha viongozi wa ulimwengu wengi zaidi kuonekana kwa pamoja kwa miongo kadhaa.

Mawaziri wakuu wa Canada, Australia na New Zealand tayari wako Uingereza.

Mzozo unazingira baadhi ya wageni waalikwa, kama vile Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed Bin Salman.

Mbali na Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau, Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese na Waziri Mkuu wa New Zealand Jacinta Ardern, viongozi wengine wa Jumuiya ya Madola wanaotarajiwa kuhudhuria ni pamoja na Waziri Mkuu wa Bangladesh Sheikh Hasina na Rais wa Sri Lanka Ranil Wickremesinghe.

India itawakilishwa na Rais Droupadi Murmu.

Viongozi walioalikwa leo watapata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho huko Westminster na kutia saini kitabu cha maombolezo.

Mazishi ya kitaifa ya Malkia Elizabethi II yatafanyika kesho Jumatatu Westminster Abbey, London, kabla ya mwili wake kulazwa kwenye kasri la Windsor.

BBC
tuombe yasitokee yale ya LONDON HAS FALLEN
 
Back
Top Bottom