GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,277
- 6,673
Jana ndio tulifuata majibu hayo kwa ajili ya rafiki yangu
ambaye amechumbia binti wa kizaramo. Majibu hayo yamenisisimua
na kuniacha hoi hasa upande wa mambo ambayo tunatakiwa
kulipia. Haya ndiyo mambo yenyewe.
Kwanza tulitozwa faini kwa makosa mawili.
1. Tulipeleka barua ikiwa kwenye bahasha imefungwa kwa GUNDI
Hilo tuliambiwa ni kosa inabidi tusiifunge hiyo bahasha kwani inamaanisha
kuwa baba mzazi wa huyo binti hajatahiriwa. Duh!
2. Kwa haraka ya kutaka kuifungua mjomba wa yule rafiki yangu akaichana
kwa nyuma, nalo likawa kosa lingine eti matusi nani umemuona anatahiriwa
nyuma.
Makosa yote mawili tumelipia 25,000 kila moja siku tuliyofuata majibu ya barua.
HIZI NI BAADHI YA GHARAMA AMBAZO TUMETAKIWA KULIPA
1.Kisamvula ndevu - 25.000
2.Mkaja wa Bibi - 25,000
2.Mkaja wa Babu - 25,000
3.Kakwambia nani kama kuna mchumba 25,000
Naomba ufafanuzi kutoka kwa Wazaramo Mkaja na kisamvula ndevu ni vitu gani?
Pamoja na yote hayo nimefurahia mapokezi mazuri na ya aina yake ambayo
yananitamanisha kutafuta binti wa kizaramo.
ambaye amechumbia binti wa kizaramo. Majibu hayo yamenisisimua
na kuniacha hoi hasa upande wa mambo ambayo tunatakiwa
kulipia. Haya ndiyo mambo yenyewe.
Kwanza tulitozwa faini kwa makosa mawili.
1. Tulipeleka barua ikiwa kwenye bahasha imefungwa kwa GUNDI
Hilo tuliambiwa ni kosa inabidi tusiifunge hiyo bahasha kwani inamaanisha
kuwa baba mzazi wa huyo binti hajatahiriwa. Duh!
2. Kwa haraka ya kutaka kuifungua mjomba wa yule rafiki yangu akaichana
kwa nyuma, nalo likawa kosa lingine eti matusi nani umemuona anatahiriwa
nyuma.
Makosa yote mawili tumelipia 25,000 kila moja siku tuliyofuata majibu ya barua.
HIZI NI BAADHI YA GHARAMA AMBAZO TUMETAKIWA KULIPA
1.Kisamvula ndevu - 25.000
2.Mkaja wa Bibi - 25,000
2.Mkaja wa Babu - 25,000
3.Kakwambia nani kama kuna mchumba 25,000
Naomba ufafanuzi kutoka kwa Wazaramo Mkaja na kisamvula ndevu ni vitu gani?
Pamoja na yote hayo nimefurahia mapokezi mazuri na ya aina yake ambayo
yananitamanisha kutafuta binti wa kizaramo.