Jamani inaeleweka hata kabla ya kuanza kazi kwamba Nchimbi alipaswa kuwa amefukuzwa. Tazama katibu wa kamati ya Nchimbi alikuwa ni afisa wa polisi, yaani wanaotuhumiwa kwa mauaji, sasa hapo unategemea nini?? Ukisoma ile taarifa utaona kuna maeneo mengi tu hata kiswahili wamekosea, hapa naona hata wajumbe wengine wa kamati hawakupata kuisoma na kuirekebisha. La ajabu, wote wamesaini tar 09 October 2012 ikimaanisha kwamba huenda wajumbe walikutana tu pahala fulani nakusema lete tutie saini hata pasipokuipitia.
Anayeendelea kufurahia serikali ya namna hii kuendelea madarakani ana ufinyu wa kuona katika ubongo wake! Si kwamba inasikitisha tu, lakini pia inatia aibu kwa nchi na taifa!