Vimbano, vimini bungeni vyamkera naibu spika

jamani, nadhani wamasai watusaidia, mbona wao wanavaa hawasemwi???????? vikuku poa tu hilo ni pambo tu, na wenye miguu uwongo, inavutia
 
mnawawaona hawa maana ya vikuku vya miguuni ni kwamba hawajaolewa hivyo wakiumeni rukusa wako huruila kwa mke wa mtu sio kabisa inahashiria kuwa kidumu ni muhimu sanaaaaa
 

hawa wamevaa bomba tu....tatizo hivyo vishanga vya mguuni....niliwai sikia ufaransa ukivaa hvyo unamaanisha wewe ni msagaji...but sijaifanyia utafiti sana...kama kuna mtu anazodata kamili anipe...........

inamaanisha pia yuko tayari mbele na nyuma!!
 
Wednesday, 13 April 2011 20:50

Israel Mgussi, Dodoma

IDADI kubwa ya wanawake vijana,wanavaa mavazi yanayopingana na maadili ya Bunge, jambo linalowafanya baadhi yao kuzuiwa kuingia mara tu wanapofika katika milango mikuu ya kuingilia bungeni.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, baada ya wabunge wa kike vijana kulalamika kuwa wanazuiwa na walinzi kuingia bungeni, kwa sababu ya mavazi yanayopingana na maadili ya Mtanzania na picha halisi ya Bunge.Hatua ya walinzi kuwazuia wabunge hao, iliwafanya waazimie kuwasilisha kilio chao kwa Naibu spika wakidhani kuwa wanaonewa.

Baadaye habari hizo zilimfikia Ndugai ambaye alizitolea maelezo kabla ya kuahirisha Bunge.Ndugai alisema, baadhi ya wabunge hasa wanawake, wamekuwa na tabia ya kuvaa mavazi yanayopingana na utamaduni na maadili mema ya Mtanzania.Kwa mujibu wa Naibu spika,baadhi ya mavazi hayo yanaonyesha maungo ya miili ya wabunge hao na mengine ni mafupi mno.

"Kuna tatizo la mavazi, wabunge wengi wamekuwa wakisumbuliwa pale wanapofika getini wakitakiwa warudi wakabadilishe mavazi, sina tatizo la wabunge wa kiume, mavazi yao yanajulikana na hayajatupa taabu, hatuna tatizo na wabunge wanawake wakinamama hawa mavazi yao yamekuwa ya heshima," alisema Ndugai.

"Tatizo ni kwa wabunge wanawake vijana, hawa wengi wao wamekuwa wakivaa nguo fupi, zinazobana na zinazoonyesha maungo yao ya mwili, hii imekuwa ikitupa taabu sana,"alisema Ndugai.

Alisema kanuni za Bunge zimetaja mavazi yanayostahili kuvaliwa na mbunge anapouwa katika shughuli za chombo hicho cha kutunga sheria."Niseme kuwa msione kama mnaonewa pale mtakaporudishwa pale getini,hizo ni kanuni na kwa kweli si vizuri kuvaa mavazi ambayo yatawafedhehesha wenzako na wewe mwenyewe pia,"alisema Ndugai.
 
wengi wa wabunge wa jinsi hiyo hawana mchango pale bungeni zaidi ya kwenda kujitangaza kibiashara.
Kama watu wapo kuzomea wenzao unategemea akili zao zinafikiria nini?
 
Labda tatizo ni kuwa na Wabunge wengi wa Kuteuliwa mara nyingi hawachangii hoja zozote ni Umaridadi
 
Kapendeza mwenyewe

HOW AMUSING! The Prime Minister, Mr Mizengo Pinda (right), enjoys a light moment with Kawe MP (CHADEMA), Ms Halima Mdee (centre) and Minister of State in the Prime Minister's Office (Regional Administration and Local Government), Mr George Mkuchika, at Bunge grounds in Dodoma on Wednesday. (Photo by PMO)
 
wengi wa wabunge wa jinsi hiyo hawana mchango pale bungeni zaidi ya kwenda kujitangaza kibiashara.
Kama watu wapo kuzomea wenzao unategemea akili zao zinafikiria nini?

Ngono tu, mbona hawaongelei la machangu kuhamia Dodoma na kufumwa wakiwa na wakubwa? Ulitegemea wanaume wavae kata-K? Nguo fupi no! Ufisadi na kulala bungeni Yes!
 
Kuna picha za hivyo vimini?

na vikuku navyo

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MIGUU ya wabunge wanawake iliyoshiba na kupambwa na cheni maarufu kwa jina la ‘vikuku’ ni miongoni mwa mambo yaliyokuwa vivutio katika mkusanyiko wa wabunge wakati wa kuapishwa mjini Dodoma, Amani limesheheni data.

Katika viwanja vya Bunge, mapema wiki iliyopita, wabunge wanawake kadhaa walionekana wakiwa wamejipamba na vikuku, hali iliyowafanya baadhi ya waheshimiwa wanaume kuikodolea macho miguu yao na kuijadili.

Wakikatiza mbele ya macho yake, Mbunge mmoja wa Chadema kutoka mkoani Mwanza ambaye Amani linamhifadhi jina alisikika akisema: “Miguu hiyo bwana, kama mwanamke hana mguu wa bia hawezi kuvaa kikuku.”

Mwenzake, kutoka CCM Unguja, Zanzibar akadakia: “Kwanza kitampwaya. Maana kikuku chataka mguu hasa.”
Amani lilibahatika kuongea na mbunge mmoja miongoni mwa waliokuwa wametinga urembo huo ambaye sharti lake la kwanza alisema si lazima kutumia jina lake gazetini kwa sasa, na alikuwa na haya ya kusema:

“Kusema kweli kikuku ni urembo wa mwanamke kama ulivyo urembo mwingine, mfano bangili, hereni, cheni ya shingoni na vikorombwezo kibao, unajua mwanamke kujipamba, au siyo?”

Akaongeza: “Lakini si wanawake wote wanaovaa vikuku, kama ilivyo kwa cheni shingoni au bangili mkononi, sifa mojawapo ya kuvaa kikuku ni kuwa na mguu mnene kiasi.”

Utafiti wa kina uliofanywa na Amani umejua kwamba, ni kweli wanawake wanaovaa vikuku ni wale waliojaliwa miguu yenye maumbile maarufu kama ‘mguu wa bia’ ambapo huvaa ndani ya viatu vya kutumbukiza na vyenye visigino virefu.

Mbali na wabunge wavaa vikuku, lakini pia waheshimiwa wengine wanawake ‘walioneshana’ umahiri wa kujipamba kwa suti za nguvu huku wakibeba mikoba yenye rangi sawa na suti hizo, hali iliyowafanya waonekane warembo zaidi kuliko wakati wa kampeni za ubunge zilizokwenda kwa takriban miezi miwili na nusu, katika Uchaguzi Mkuu wa 2010.
 
Ndio Tabu ya kujaza watu na kuwalipa hela nyingi bila Chochote wanachochangia!! Fikiria Mtu Unapata over 12,000,000 Kwa mwezi na Huna chochote Cha maana unachofanya, Si utafikiria kuvaa Gold Hadi Kwenye Makalio, Achilia Mbali Miguuni!! Wingi wa Bure bila Manufaa!! Shame on this Country
 

Wakivua nguo tutaona mengi:love:
 
tena nasema asilimia kubwa ya wavaa vimini bungeni ni wale ambao hawana ndoa wanataka kuiba waume za watu matingatinga yanazoa dunia nzima tuna cv zao tena waache mara moja.halafu mbona inajulika mwanamke anayevaa cheni mguuni ni msagaji na mwaume anaevaa hereni ni shoga.
 
Hii ni kwa kusisitiza kama una mke ama mchumba mbunge yuko dodoma endelen kuwahimiza waache kufanya bunge letu tukufu kama danguro la Sinza afrikasana
Si mbaya kujiheshimu hatakama ulivua nguo kupata ubunge na sidhan kama waliokutumia wataendelea kukutumia tena wakiwa bungen ..embu jiheshimun madada zetu jaman mnatutia aibu kubwa huu ni upuuzi

Imefika wakati bunge letu lisiwe bunge la umalaya bali la kushugulikia shida za wananchi..nawapongeza walioona hili ni wachache sana wenye uwezo wa kulalamikia..unaweza ona wabunge wengine walikuwa wakifurahishwa na hali hii chafu ya kuvaa nguo nusu uchi..nani anauitaji uchi wako...kama upo na unataka utumike kwa nini usiende lasvegas watu wakautumia na wewe kufaidika tena zaidi ya posho za bungen

Huu wakati wa uwazi na ukweli kama mliwavulia nguo mafisadi mkaingia haya sasa wameanza kufukuzwa sijui mtakimbilia wapi..nawaasa mabibi na madada zetu jiheshimun..unalalamika ujaolewa utaolewa na nani akuna anaekimbilia milupo sikuhizi kupata presha ya maisha watu wanataka raha za milele na sio mateso mnayoyatafuta mtaishia kukaa uchi na mtatumika vilivyo na hii ni aibu yaani hata mwaka wa PILI aujafika mna kashfa za kukaa nusu uchi Lohhhh

Mama Yetu Makinda usikubali kukaa na wachafu kama hao tafadhali mkishindwa kabisa tuiten tutachape bakora kwa mnaokumbuka kuna kundi la waislamu walikuwa wakija pale afrikasana sinza na kuwakimbiza wale wauza uchi mpaka kukawa na heshima ilifika wakati unaenda kula na mkeo unaonekana umelambaa Zigo kumbe wapi uko na wako milele

Kila la Kheri Bunge Jipya la Bashasha

Wakati huo huo kundi la madada walioondoka kwa ajili ya kwenda kuwauzia uchi wabunge limefurahi kkitendo cha Naibu spika kuwakataza wanawake kuvaa nusu uchi na kufikia kuwakosesha biashara
wakizunguzumza kwa kufurahi wanasema unajua kaka tunakodishaga basi la shabiby zaidi ya mawili kwa ajiili ya kwenda kuwatimizia wabunge wenu wasiteseke baada ya kuwamiss wanaowapenda sasa hii midada iko humuhumu na inakula hela nyingi tu bado inangangana kubanana na sie wachovu siju vipi...hawana hata huruma hawa angalia wanavaa vikuku sijui wanashida gan...pamoja na hivyo wamekiri wabunge wengi wa kike wazuri na wanazuia biashara zao kwa kuwa wabungewengi wamekuwa wakichukuana weneyewe kwa wenyewe ukilinganisha na bunge la zamani..wakalalamika sana bunge la sasa limejaa vijana wengi..enzi za mababu zetu waliowafukuza we acha tu tulifaidi mbaya unarudi si chini ya M1.5 Mpaka linaisha ....wale wazee inabidi wafanye utaratibu wa kuwarudisha nanukuu..

Hata hivyo Binafsi nawashauri waaachane na biashara hiyo kwa kuwa vijana wengi wa sasa awajui maana ya CONDOM na hivyo kuwataaharisha maisha yao..n kweli wanasema mababu wameondolewa lakini wale mababu walikuwa waoga sio bunge la sasa wako masahrobaro kibao wao ngozi kwa ngozi sidhan kama watawaacha na kwa kufanya hivi wanaongeza idadi ya wabunge wagonjwa na hivyo kufanya maisha ya wabunge kuwa magumu kumaliza miaka yao 5 ukiacha wale wanaoondoka kwa ngwengwe mean kwa kupulizwa...na mwisho watu kuishia kuzika MAGOGO AMA MIGOMBA BADALA YA WATU

ASSALAAHM ALHEIKUM WABUNGE WAPYA
 
Israel Mgussi, Dodoma
IDADI kubwa ya wanawake vijana,wanavaa mavazi yanayopingana na maadili ya Bunge, jambo linalowafanya baadhi yao kuzuiwa kuingia mara tu wanapofika katika milango mikuu ya kuingilia bungeni.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, baada ya wabunge wa kike vijana kulalamika kuwa wanazuiwa na walinzi kuingia bungeni, kwa sababu ya mavazi yanayopingana na maadili ya Mtanzania na picha halisi ya Bunge.Hatua ya walinzi kuwazuia wabunge hao, iliwafanya waazimie kuwasilisha kilio chao kwa Naibu spika wakidhani kuwa wanaonewa.

Baadaye habari hizo zilimfikia Ndugai ambaye alizitolea maelezo kabla ya kuahirisha Bunge.Ndugai alisema, baadhi ya wabunge hasa wanawake, wamekuwa na tabia ya kuvaa mavazi yanayopingana na utamaduni na maadili mema ya Mtanzania.Kwa mujibu wa Naibu spika,baadhi ya mavazi hayo yanaonyesha maungo ya miili ya wabunge hao na mengine ni mafupi mno.

"Kuna tatizo la mavazi, wabunge wengi wamekuwa wakisumbuliwa pale wanapofika getini wakitakiwa warudi wakabadilishe mavazi, sina tatizo la wabunge wa kiume, mavazi yao yanajulikana na hayajatupa taabu, hatuna tatizo na wabunge wanawake wakinamama hawa mavazi yao yamekuwa ya heshima," alisema Ndugai.

"Tatizo ni kwa wabunge wanawake vijana, hawa wengi wao wamekuwa wakivaa nguo fupi, zinazobana na zinazoonyesha maungo yao ya mwili, hii imekuwa ikitupa taabu sana,"alisema Ndugai.

Alisema kanuni za Bunge zimetaja mavazi yanayostahili kuvaliwa na mbunge anapouwa katika shughuli za chombo hicho cha kutunga sheria."Niseme kuwa msione kama mnaonewa pale mtakaporudishwa pale getini,hizo ni kanuni na kwa kweli si vizuri kuvaa mavazi ambayo yatawafedhehesha wenzako na wewe mwenyewe pia,"alisema Ndugai.

Source: Gazeti la habari za kiswahili la kila siku Tanzania, linaongoza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…