Vile mashauzi yalivyoniumbua

Amen mtumishi mwenzetu

Ubarikiwe pia mno kabisa.

Pengine amekufanyananisha na akina bia yetu 🤣🤣🤣
😂😂😂😂
Hivi kweli katika vitu vya kunifananisha navyo ndiyo ije kuwa Bia yetu??? Si bora tu mninyonge..!
 
Hii akili ipo

"Mwanaume akimsimamisha mwanamke njiani akili yake ya kwanza inajua unataka kumtongoza.
Mwanaume ukisimamishwa na mwanamke njiani unahisi huyu ana shida"

Katika harakati zangu huwa najizuia saana kuzungumza na mwanamke nisiyemfahamu.
Kwanini unajizuia mkuu?
 
Amezingua sana.

Angalau hata angekufananisha na 'half rey'

Of all people bia yetu kweli🤣🤣
Haahhahhahaaa..!
gademt..!
Kitendo tu cha kunifananisha na rangi yoyote ya kijani kwanza kabisa nasimama nacho kinyume.!!
 
Mtumishi mwenzetu Saint Anne anaielewa sana kijani.

Sijui ile rangi ya mboga mboga huwa anaipendea nini.
Pep naona leo umeamua kunichana baba
Usichokijua baba ni kuwa mimi nilikuwa namshabikia mtu na si chama.

Sasa hivi wote tupo kuupiga mwingi kama mama.

NB: Sina mawazo ya kuwa mwanachama wa chama chochote Tanzania
 
😂😂😂😂
Hivi kweli katika vitu vya kunifananisha navyo ndiyo ije kuwa Bia yetu??? Si bora tu mninyonge..!
😂😂😂😂😂
Nimemmiss bia yetu jamani🤣🤣🤣
Kuna siku kalinichamba
 
Nilipokuwa dukani kwa mangi bossi. Alikuja mdada mmoja katoa mkoba kisha akatoa pochi, kalipa hela kununua vitu vyake, sasa ile anarudisha pochi kwenye mkoba akaiangusha chini,
Nikamuita yeye ndio kwanza anatingisha chura yake eti ananikomoa akawahi kwenye kipasso chake.

Nilipita zangu waswanu pale nikala kitimoto kilo 2 na bia nikarudi kujaza na gesi nikarudi Home

Sipendagi mashauzi kabisa.
 
Wanaume kweli wanasumbua ila nikipita sehemu hata salamu huwa najibu japo najua wengine wanasalimi kwa sababu zao, hata barabarani mtu akinisimamisha huwa namsikiliza ndo naendelea na safari. Nilijifunza hii kwamba sio kila anaekuongelesha anataka kukutongoza wengine ni watu wema wanataka kukusaidia jambo so ni bora umsikilize halafu uamue lakini sio kumpotezea mtu.

Nilishawahi simamishwa na mkaka akaniambia zipu ya jeans iko wazi. Nikamshukuru nikafunga. Sasa ningejifanya mrembo mimi ndo mrembo sana nisimsikilize ningeumbuka vibaya sana maana nilipokua naenda kuna watu wengi.

Juzi juzi nimeenda kwenye ATM askari akaniita moyoni nikasema huyu hana lolote ila wacha tu nimsikilize, akaniambia kuwa makini dada wanaiba simu maeneo haya. Hata hakunitongoza baba wa watu nikasema ningekua wale wanawake washamba wa kuvimbia wanaume ningeibiwa angeishia kunicheka tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom