Nakumbuka siku moja naenda kazini daladala za Kibaha kutokea Ubungo- 2010.
Ilikuwa ni vile vi-hice, mdada mmoja alikaa mbele yetu tulimkuta kwenye gari, tukafika Maili moja yule dada ikawa ndo mwisho wake wa safari akanyanyuka kushuka, alikuwa mrefu kiasi ikabidi ainame kidogo ili apite akashuke, aisee sketi zipu ilishuka kidogo na sketi yenyewe alikuwa hajafunga lock yake, tulichikiona ni pant imechoka na shanga nyingi. tulikaa na jamaa mmoja lile tukio lilituhuzunisha sana, hadi tukashika midomo kwa butwaa, cha kushangaza wanawake wenzake walicheka vibaya sana.
Ilinipa fundisho sana, nilipooa, nilihakikisha mke wangu hapati fedheha kama ile, nahakikisha anachokivaa kinakuwa perfect kabla ya kutoka nyumbani, nakifanya hicho toka 2016 mpaka leo na sitaacha, hata nikiwa nimesafiri sipo nyumbani lazima nimkumbushe.