Vikwazo vya maendeleo katika nchi yetu ni...

Sidhani kama kwa kutumia sanduku la kura kuwatimua haiwezekani. Tukiwakataa katakata kwenye sanduku la kura itawafanya hata wao wajishtukie kuiba kura. Mara nyingi kura huibwa kama idadi haijapishana sana.

Kama hilo likishindikana, basi tunaweza na sisi kuwa Orange Revolution yetu kama ilivyokuwa kule Ukraine. Kama hujui Orange Revolution ni nini jaribu ku google na utaelewa ilikuwa ni nini na faida zake zilikuwaje. Nakwambia massive civil disobedience, passive resistance, sit-ins, na migomo mingine inafanya kazi. Ilifanya kazi Marekani wakati wa civil rights, ilifanya kazi Ukraine na kwingineko duniani na nina imani itafanya kazi Tanzania. Tatizo wengi wetu hatuko tayari kulipa gharama. Tuko waoga.

Labda hilo la kufanya Orange Revolution ndilo litakalofanikisha kuiondoa CCM madarakani, lakini kuwatoa CCM madarakani kwa kutumia kura kwa maoni yangu haitawezekana kabisa. Watawanyanyasa wanachama na viongozi wa vyama vya upinzani kwa kila namna wakati wa kampeni tena kwa kutumia vyombo vya dola kama FFU, polisi na hata Wanajeshi. Pale ambapo wanajua kuna uwezekano wa kushindwa wataweka mikakati mikali sana ya wizi wa kura
 
Labda hilo la kufanya Orange Revolution ndilo litakalofanikisha kuiondoa CCM madarakani, lakini kuwatoa CCM madarakani kwa kutumia kura kwa maoni yangu haitawezekana kabisa. Watawanyanyasa wanachama na viongozi wa vyama vya upinzani kwa kila namna wakati wa kampeni tena kwa kutumia vyombo vya dola kama FFU, polisi na hata Wanajeshi. Pale ambapo wanajua kuna uwezekano wa kushindwa wataweka mikakati mikali sana ya wizi wa kura

Ndio maana nilikupa mfano wa Montgomery bus boycott wakati wa civil rights Marekani. Watu wakiamua kufanya kitu kwa umoja hakuna linaloshindikana. CCM ni fraction ndogo sana ya Watanzania wote. Tukiwagomea hawatakuwa na wa kumwongoza. We need our own Orange Revolution now.
 
Ndio maana nilikupa mfano wa Montgomery bus boycott wakati wa civil rights Marekani. Watu wakiamua kufanya kitu kwa umoja hakuna linaloshindikana. CCM ni fraction ndogo sana ya Watanzania wote. Tukiwagomea hawatakuwa na wa kumwongoza. We need our own Orange Revolution now.

Nafikiri kule Z'bar walianza kuonyesha njia ya kuipinga CCM na hata kusababisha watu kuuwawa lakini matokeo yake hayakuwa ya kuridhisha. Na viongozi wengi wa Z'bar wakati ule sasa hivi wanakula sahani moja na CCM baada ya kuwageuzia kibao wanacham awao, hapa namzungumzia Sharriff Hamad na wengine wachache, lakini bado sikubaliani na kuwalaumu Watanzania wote maana wanaopinga CCM wanaongezeka kila kukicha lakini pamoja na ongezeko hili CCM bado inashinda hata katika majimbo ambayo hawastahili kabisa kushinda.
 
This has got to be one of the most ridiculous claims ever..that we (Africans) were more developed than Europe during the 15th and 16th centuries.

Huyo Rodney wenu hoja zake zimejikita ktk kutokujionesha kuwa duni ilhali hali halisi inapingana na hoja zake. Haingii akilini eti tulikuwa tumeendelea zaidi au tulikuwa sawa kimaendeleo halafu wao (wazungu) wakaja wakatulostisha na tokea hapo hatuja recover kabisa. This makes no sense.

Wakatuletea dini na sisi tukazikumbatia. Wakatuletea so called ustaarabu na sisi tukaukumbatia. Wakatuletea lugha tukazikumbatia. Wakatuletea elimu tukaikumbatia. Wakatuletea mambo mengine lukuki (likiwemo kulana denda-french kiss) na sisi hao kichwa kichwa tutayakumbatia. Juu ya yote hayo wakaja wakatutawala kimabavu. Wakagawiana bara letu kama vile ni mali yao binafsi, na sisi tulivyo wajinga tukakaa tu tukiwatazama na kuwasubiri.

Sasa mtu eti aje na hoja ya kudai kuwa tulikuwa sawa au kuwazidi kimaendeleo mimi nitamwona kachanganyikiwa tu. Maendeleo ni pamoja na kuamka kifikra na kuwa mwerevu. Sasa ni maendeleo gani hayo tuliyokuwa nayo wakati wenzetu walikuwa werevu zaidi kutushinda sisi?
Mkuu nilimuuliza hawa wazungu volunteers wa uingereza. Alikuwa mwalimu wa biology (evolution). nilimuuliza kwanini wao (wazungu) walipata akili mapema na kuja kututawala na hatimaye kutufanya watumwa kwani wao walievolve kabla yetu na je tunalingana akili?Akanijibu hajui. How can someone justify kwamba tuliendelea kuliko wazungu.Huyo Roodney nakuunga mkono ni Mwongo.Alikuwa anavutia kamba kwake.

Kuna mgeni aliniuliza kwamba "nyie waafrica kwa nini ni wakristo au waislamu wakati yesu na mohammad ni wazungu na waarabu?Aliniuliza kwa nini mnaamini kwamba wazungu na waarabu hawawadanganyi?

Nilishindwa kujibu maake na mimi nimeaminishwa tu.

Wachina wenyewe wanadhani kwamba sisi (black) hatuendelei kwa sababu mbili moja sisi ni wavivu (kufikiri na kutenda) hatutaki kuenyeka. wameambiwa kwamba usimfanyishe kazi nyingi black ukitaka muwe marafiki. Hili nilithibitisha kwa supervisor wangu. Je sisi ni wavivu pamoja na viongozi wetu?Sababu ya pili wanadhani sisi ubongo wetu ni inferior. katika kuprove hilo kijana (mchina) ananiambia kwamba tunaweza riadha tu na football kidogo kwasababu michezo hiyo haihitaji akili sana.Ana refer olympic beijing.

Vile vile anasema maendeleo yote ya kisayansi ni weupe tu. Anakiri kwamba hata wao wako nyuma lakini wanapiga hatua. Je tuko inferior? Mimi nilishindwa ku-prove kwamba hatuko inferior kama reference yake ilivyokuwa ni maendeleo ya kiuchumi, kijamii na technologia).Ninachojua ni kwamba kuna tatizo somewhere in our thinking.Tunadhani tuko nao sawa.

Tunataka kutumia magari kama yao, nyumba kama zao, furniture kama zao kila kitu kama zao lakini hatuna hata ndoto ya kumiliki (kutengeneza).Tunaona aibu kuanza moja. Na kibaya zaidi hata kuiga hatu-encourage. Tumekata tamaa tunadhani hatuwezi na kwamba tunawakaribisha waje watuwezeshe (kuwekeza)!
 
- Maendeleo ya nchi yetu yanadumazwa na sisi wananchi, kama huamini angalia mikoa ya Kilimanjaro na Arusha, wao hawaisubiri serikali hufanya mambo yao kama watakavyo serikali huja kuwasaidia kusogea mbele tu, lakini kila kitu hufanwya na wao wenyewe bila kusubiri serikali, mchawi wetu ni sisi wananchi wenyewe!

Respect.

FMEs!
Mkuu mimi ninavyofahamu ni kwamba mikoa hiyo unayotaja iliendelea kwa sababu ilishikilia BOT na TRA (hazina zetu) na ndo maana watu wakawa na wanavuga kwenye biashara lakini wanachota tu pesa.Ajira ndo usiseme.Kwa sasa ambapo ofisi ile hawapo na mkuu akirejea tena atawatimua TRA hapo tu tutawapa miaka nyingine ishirini ndo tuamini kwamba hiyo mikoa inaendelea kwa sababu ya juhudi zao. kwa sasa bado nina doubt uhalali ya utajiri wao.
 
Nyani,

Hujanijibu swali langu, kwa nini tupoteze the art and skills of anything in just 4 generations? Yaani hapakuwa na oral stories jioni tukiwa tumekusanyika kuota moto wa mavi ya ng'ombe au Mzungu alikuwa anatulinda hata tusiongee?
 
Nyani,

Hujanijibu swali langu, kwa nini tupoteze the art and skills of anything in just 4 generations? Yaani hapakuwa na oral stories jioni tukiwa tumekusanyika kuota moto wa mavi ya ng'ombe au Mzungu alikuwa anatulinda hata tusiongee?

I don't think there was much art and skills to lose in the first place.
 
jamani... hebu nigeukie upande wa pili kuangalia mchango chanya wa mila desturi etc......... back to Values/belief systems..... ina maana jamii za kitanzania hazina tena misingi iliyoweza kusimamia maadili ambayo ni muhimu katika kuleta maendeleo?
Nadhani mfano mzuri uliopo ni wamaasai japo kwa siku za karibuni nao wameanza kuwa kama wengine wote tu.... walinzi wa Kimaasai walikuwa wanaaminika sana kwa vile bado walikuwa wanadumisha mila..... wanatii mamlaka zao za kijadi... wakikutendea kinyume ukawashtaki kwa viongozi wao mf. Laigwanang..ungeweza kupata haki bila kwenda mahakamani! Siku hizi .hawaaminiki tena .......
Belief /value systems ni muhimu kuzijua na kujua namna ya kuzitumia.....
 
Kusema tu kikwazo ni sisi wananchi
kwa ujumla ni makosa....

wananchi tanagawanyika kwenye makundi
tofauti,hasa kielimu.
 
KIKWAZO CHA MAENDELEO YA NCHI YETU NZURI YA TANZANIA, NI CCM (SISIEMU).period. sisiemu ikitoka madarakani tu, maendeleo yatakuja yenyewe, kwasababu mizizi ya uovu wote itang'olewa, na nchi itaanza kupandwa upyaaaa, sio pachika pakua fisadi inayoendelea sasahivi hii.
 
Kusema tu kikwazo ni sisi wananchi
kwa ujumla ni makosa....

wananchi tanagawanyika kwenye makundi
tofauti,hasa kielimu.

The BOSS :) Mfano mzuri wa kuonyesha kwamba tatizo la nchi nyingi za Kiafrika ni Viongozi na si Wananchi ni Zimbabwe. Nchi hiyo ilipopata uhuru 1980 ilikuwa na uchumi mzuri sana na pia iliweza kujitosheleza kwa chakula na kingine kuuza nchi za nje. Miaka michache baadaye kutokana na utawala mbovu wa Mugabe uchumi wa nchi hiyo umeanguka vibaya sana na hata haiwezi kujitosheleza kwa chakula. Wananchi wa Zimbabwe ni walewale waliweza kuifanya nchi hiyo kuwa na uchumi mzuri na pia kujitosheleza kwa chakula, kilichobadilika na kuondoka mkoloni na kuingia Viongozi wazawa ambao wamesambaratisha uchumi wa nchi hiyo vibaya sana. Hapa wa kulaumiwa kama ilivyo katika nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania si wananchi bali Viongozi mufilisi katika utendaji na kuweka mbele maslahi ya nchi zao.
 
Ni kweli kabisa jamii nyingi sana zenye tradition hata kubadilika ndio inakuwa vigumu sana, kama Tanzania na hii inakwenda mpaka kwenye siasa na kuwa na viongozi wasio taka maendelea kwa kuwa wawazi kama tanzania
 
tatizo la kwanza ni sisiemu (CCM), hayo mengine yana editiwa kama chama hiki cha ajabu chenye genge la wezi kikiondoka madarakani.
 
Jamii inaongozwa na ujumla wa mifumo na taratibu zinazoathiriwa na belief systems ( imani za kidini, mila, desturi, haki na uhuru wa kujieleza au kudai haki etc).

Nchi nyingi hasa za Kiafrika zimeshikilia sana imani ( za kidini au kimila) kama nguzo za jamii zao na kuwa na kiwango kidogo cha uhuru wa mawazo au hata kudai haki mbalimbali..nchi hizi nyingi hujikuta zina maendeleo hafifu. Nchi kama Sweden au Uholanzi ambazo hutoa uhuru mwingi kwa wananchi wake..kuna haki za watoto na wanawake za kiwango cha kutisha - zimepiga hatua kubwa kimaendeleo.....

Kwa maneno mengine... kadiri jamii inavyoshikilia mila ( traditions) ndivyo kiwango cha maendeleo kinavyokuwa chini..

Je, ina maana mila, desturi au hata imani za kidini hudumaza maendeleo?

Swali lako zuri dada yangu lina majibu ya ndiyo mengi na ya hapana mengi kutegemea mjibuji ana ufahamu gani

Si kweli kuwa mila na desturi zinadumaza maendeleo. Mila na desturi zinatokana hsa na hali ya watu wa mahali hapo, mazingira n.k , mtu anayeishi Dodoma, ni likely akawa na utamaduni tofauti na anayeishi pwani. Mila na desturi uathiriwa pia sana na hali ya hewa,, majanga n.k

Kwa mfano mila zetu wengi tulizoea kulima kwa umoja kuishi kwa umoja na kucheza ngoma vipindi vya mavuno , kutunza mazao na kuyatarisha mashamba kwa ajili ya kilimo kijacho na vizazi vijavyo.

Watu wanaoishi kwenye hali mbaya kabisa za hewa kijiografia let say, nchi za ulaya, asia na america, tabia na tamaduni zao zinaendana sana na kukabili hali hizo na kwa sababu ni ngumu mafanikio ya kukabili hizo hali yanapitia hatua nyingi sana.

Dini pia ina mchango wake wa kuleta maendeleo au kudumaza kulingana na ilivyopokelwa; here is my view in a nutshell

Geographical position

Wanaoshi kwenye tropical, where they can experience all four seasons without any problems and threats, wengi hufurahia hali hii. MAANA ndiyo hasa unakuwa kama unaishi duniani!! study zinasema watu wanaoshi kweny tropical wana furaha sana and peace of mind kulingana na watu wanishi nchi za baridi sana, jangwani au sehemu za matetemeko n.k

Na usipoufanyisha mazoezi ubongo kawaida unadumaa, we can not innovate anything kwa sababu hatuna shida ya kufanya hivyo! (hapa nasema as if hakuna influence ya mataifa ya nje)

Nchi za ulaya wana onekana wana akili kwa sababu hali ya mazingira ya nchi zao imewapelekea kuwa hivyo, taabu na dhiki walizopitia sisi kamwe hatutakuja kuzipitia


Tamaduni

Tamaduni zina nguvu sana, mila zina nguvu mno, ukaribu, ujima, au tulivyokuwa tunaishi kama waafrika, ilileta na inaleta uhusiano wa nguvu sana kati ya mtu na jamii anayoishi. Kwetu sisi mtoto ni wa jamii au jumuiya, kwa hiyo kila afanyacho mtu kina reflect jinsi gani alivyofundishwa na jamii yake; Ubora wa mtu au ubovu ulitokana na jamaa ndugu zake unless atokee mtoto unique kama Okonkwo (Things fall part) ambaye alisema anataka kutokuwa mvivu kama baba yake.

Ndiyo maana kama kabila fulani ni wavivu basi asilimia kubwa ni wote , genes zimeshaingia damuni, so kama kabila lako lilikuwa na utamaduni mbaya usioleta maendeleo basi mtakuwa hivyo hivyo. Tamaduni zinaweza kuvunjwa kutokana na externa force kama maingiliano na jamii zingine, dini , elimu n.k

Dini

Dini hazina ubaya dini kama dini; Ila mapokeo mabaya ya dini ndiyo yanaleta matatizo, dini zetu kubwa mbili zina matatizo makubwa:

waislamu-Tabia ya kuwapeleka watoto madrasa na kuhakikisha mtot anafuata uislamu
Ukristo -tabia za kupeleka watoto makanisani, kuwabatiza wakiwa watoto na kuhakikisha wanafata dini za wazazi.



Tabia hizo zote hapo juu ya dini hizi mbili ni mbaya kama zitaendelezwa vibaya! mtu akizaliwa anakuwa mtu tofauti kabisa na wewe hakuna ubaya kumpeleka mtoto msikitini au makanisani, ubaya unakuja pale tunapolazimisha, kuaminisha na kuwamezesha dini hawa watu tangu wakiwa watoto. Refer point yangu ya utamaduni, ubongo unaathiriwa zaidi na jinsi unavyolelewa , ubongo nao unakuwa kulingana na unavyopata challenge.

Kumbuka sisiemi tusiwapelke watotot maknisani au misikitini, ni vizuri kabisa , ila wakienda na wakafika umri wa kuwa huru kujifunza wajifunze, waulize, wasiambiowe kuuliza maswali ni dhambi au Mungu hapendi! kuuliza maswali ni kufuru! sasa huyu mtot nyumbani hawezi kuuliza, msikitini au makanisani hawezi kuuliza, eventually akienda shuleni hawezi kumuuliza mwalimu, ndiyo tunaambiwa confident yetu ipo chini!

Naamini mtu akizaliwa ni mtu huru kabisa na mwenye mawazo na malengo yake , parents should only guide them in good way, unaposema mtu hawezi kiuwa na tabia njema pasipo kuwa mwislamu na mkristo ni kuvunja haki za binadamu! unapomwambia mtoto unaweza kuwa na tabia nzuri na dini ni kichocheo ni vizuri pia, mzazi mlevi , jirani mzinzi na wote wana dini na watoto wanajua, likely kesho naye anafuata huko huko, MLISHAPATA KUULIZA HIVI VIONGOZI WANAOAPA KWA KUTUMIA vitabu vya dini watailinda katiba are they serious? dini leo zimegeuka ni vichaka vya kuficha wezi wote!!

Ukishaanza kumbana mtoto na kumwelekeza njia za dini kwa nguvu, basi unaharibu system nzima ya kumuwezesha ubongo wake kuuliza, kufikiri, kutawala mazingira, huyu mtu anakuwa na ubongo tegemezi kwa sababu ameshaanzishiwa kunyoshewa njia ya kuishi.We can learn this from animals, hata watoto wadogo wakinyonysa sana maziwa huwa wavivu kula chakula !!!!!

Ndio unakuta dini zote hizi watu wakiwa wakubwa huwa wengi hawazifuati, kama kuzifuata zinafuatwa kwa woga wa jamii lakini siyo kuwa watu wamezipenda kutoka moyoni. Hatujaweza kushawishi kwa SABABU na nguvu ya concepts zilizomo ndani ya hivyo vitabu.

TULICHOWEZA ni kulazimisha kutokana na nguvu zetu za uzazi. Ndiyo maana wazazi wakiona watoto wao wanataka kubadili dini wanakasirika sana kuliko mtoto akisema anataka kuwa shoga!!

Udikteta huu wa fikra za dini, julisha utamaduni tuliokuwa nao, jumlisha sehemu tuliyopo basi ndiyo unaona matatizo mengi sana ya kijamii tunayo. Na dini waliozileta walizileta kwa vipindi vibaya -waarabu walileta na kuchukuwa watumwa kwa nguvu, hivyo swala la kuwa mwislamu aidha ni kwa nguvu au kujikomba kwa waarabu,. wamisionari walileta dini juu ya mgongo wa ukoloni, japo hawakulazimisha, lakini walitumia saikolojia kulazimisha, kuwapa zawadi watu, kuwatengenganisha watu, na wengine wakakubali kuwa wakristo kwa kujikomba au kutaka zawadi, achilia mbali mabavu, wazungu waliopigana vita na mababu zetu na kuleta dini baadaye bado ni yale yale sawa na waarabu tu!

Akili huru za vijana au jamii husika uleta maendeleao huru, akili huru inatayarishwa inajengwa, japo leo hii wenzetu wana watu wachache makanisani, uhuru wao umesiaid akujua pumba na mchele, wanaoenda kanisani wanaenda kweli kweli na wanafuata dini mno, wanaoenda kwenye tabia mbaya wanazifanya kweli kweli, yaani kila mmoja yuko huru na anchokisema. Nguvu za ushawishi no bora sana kwa kuenenza dini kuliko ubabe wa aidha mzazi au utawala. Sasa kama akili haiko huru kuwaza, itakuwa tegemezi na mbaya tunarithi kutoka kizazi kimoja mpaka kingine!

Hivi watoto wa Chenge, Lowassa, Karamagi, RA kitu gani kitawazuia kuwa mafisadi? na wazazi wao still wanaenda makanisani na misikitini nako wanapokelewa vizuri kabisa!

Unaona kabisa jamii yetu haikutegemewa kuwa katika hali ya leo hii, kila mtu anawaza gari, nyumba, simu, PC kwa gharama zozote zile hata kuiba, baadaye ajionyeshe na jamii imtambue! unaona wazi kuwa mind yetu imetawaliwa zaidi na jamii na siyo mtu individually! we even not think of next generation! hakuna mipango ya miaka 100 ijayo!

Dada WoS leo tunahitaji kiongozi anayejua tabia zetu, na ambaye amekombolewa na hali hii, tumeona uvivu tunao umetokana na mazingira, pamoja na tamaduni zingine we as Tanzanian we are in a better position to rule the world! we have everything,

In principles ilitakiwa nchi tajiri kuliko zote duniani iwe Afrika!, we have everything kuanzia hali ya hewa, mali asili watu wenye manguvu, ngozi imara, miili imara n.k, ila sababu za kisaiolojia zimetufanya tuwe nyuma sana.

Hivi ndivyo ninavyofikiri
 
In principles ilitakiwa nchi tajiri kuliko zote duniani iwe Afrika!, we have everything kuanzia hali ya hewa, mali asili watu wenye manguvu, ngozi imara, miili imara n.k, ila sababu za kisaiolojia zimetufanya tuwe nyuma sana.

Kumbe Afrika ni nchi!!!
 
Kwa maneno mengine... kadiri jamii inavyoshikilia mila ( traditions) ndivyo kiwango cha maendeleo kinavyokuwa chini..

Je, ina maana mila, desturi au hata imani za kidini hudumaza maendeleo?
Jamii isiyo na mila aiwezekani kwani mila zina historia ya miundo yake mpaka tulipo ikuta sisi kizazi cha leo na zilitungwa ili ziweze kuwa mwongozo wa maisha katika hizo jamii. Na zipo karibu sana na imani, kwani imani si dini peke yake.

Wanasema mila ni part of moral guidence in a society unlike morals however they dont evolve over time that is to say miaka ya zamani kuvaa kimini au zile t-shirt za mgongo wazi kwa wadada ilikuwa tatizo na zinaweza kumpa label mbaya katika jamii. Lakini over time people have come to accept aina maana nyingine yeyote zaidi ya kuwa vazi tu na wala aina maana msichana ana nia nyingine they evolve over time.

Ukirudi kwenye mila mfano unakuta watu wana kwenda sijui kucheza ngoma za kwao msimu wa mavuno sijui ilikuwa inasaidia nini kwa sababu wazijuazo wao mababu walizo zianzisha kutokana na primitive thinking of their time, ingawa leo unakuta sababu zenyewe zimeshajulikana azina maana hila utakuta bado mijitu inan'gan'gana na hizo tamaduni za mila na desturi.

Kwa upande wangu sisi waafrika inaoneka tulikuwa mahodari wa kutunga hizi mila and we have extreme believes in them; ndio mpaka leo zinatuadhibu kuzunga zunguka na man'gombe maporini na kwenda kumuua simba for no reason kisa anataka kula n'gombe, ulienda fwata nini kwenye his natural environment. Mara kuchanjana usoni na kuogopa kukosoa wakubwa hata kama wamekosa haya yote ni against us.

Lakini all this falls back to one argument ignorance helps the survival of these silly traditions. The more we educate ourselves we learn to leave some of the traditions which are unhelpful. Mimi kwa kweli baba yangu alizaliwa kijijini lakini alikataa kamwe sisi tusitiwe na chale za macho wala kiluga akuona umuhimu wa sisi kukijua tulipokulia.

Na kwa kuwa tuna makundi mengi katika nchi zetu za afrika, each proud of their traditions it helps us elect leaders we feel are closer to us as tribesmen rather than as a citizen of that nation. Sasa ukienda huko kijijini ambapo these kind of thinking is almost extreme kwanza huwaletee na mtu wa kwao hili wamuelewe regardless of his potential. Again si ajabu asilimia kubwa ya wabunge wetu sidhani hata kama wanajua kuuliza maswali au kuleta hoja zenye kuiomba serikali ifanye kitu fulani kwa taifa zaidi ya kusema watu wangu wanahitaji hiki au fisadi kafanya hiki its all pathetic.

We have a mammoth task kuinua africa au hata nchi zetu wenyewe. Wanavyoma afrika is still primitive si dharau bali our ways of thinking proves so in large scale through our primitive traditions and reasoning labda sio humu ndani ya JF but in many other places in africa. That is we havent even looked at the culture of poverty and the ways of lives poor people tend to live we have along time battle and its going to take even longer kuendekeza people like masai and the sort.
 
Jamii inaongozwa na ujumla wa mifumo na taratibu zinazoathiriwa na belief systems ( imani za kidini, mila, desturi, haki na uhuru wa kujieleza au kudai haki etc).

Nchi nyingi hasa za Kiafrika zimeshikilia sana imani ( za kidini au kimila) kama nguzo za jamii zao na kuwa na kiwango kidogo cha uhuru wa mawazo au hata kudai haki mbalimbali..nchi hizi nyingi hujikuta zina maendeleo hafifu. Nchi kama Sweden au Uholanzi ambazo hutoa uhuru mwingi kwa wananchi wake..kuna haki za watoto na wanawake za kiwango cha kutisha - zimepiga hatua kubwa kimaendeleo.....

Kwa maneno mengine... kadiri jamii inavyoshikilia mila ( traditions) ndivyo kiwango cha maendeleo kinavyokuwa chini..

Je, ina maana mila, desturi au hata imani za kidini hudumaza maendeleo?


Kikwazo kikubwa ni ubinafsi. Viongozi wanaangalia matumbo yao, wanagombea nafasi sio kuwatumikia wananchi bali kuchukua kodi zao na mali zao kwa maslahi binafsi. Angalia Mkapa, EL , JK et al. Wanaangalia zaidi matumbo yao wanapata ngapi kwa kujineemesha siyo kuwasaidia wale waliowaweka na kuwakwamua katika matatizo yao ingawaje hivi sasa wana fweza tele ambazo wataziacha hapa duniani baada ya kufa kwao. Ndio wenye mawazo yaliyofilisika.
 
Ni porojo kwa sababu si kweli hizo ndizo zilikuwa sababu za maendeleo na kama causes of black death until the 19th century bado kulikuwa na common occurances ya vifo vya misimu in some areas.

na kama ni dini italy and spain wana huge numbers in their population ambao ni waumini, bila ya hata kusema wa israel ambao unaweza sema kwa haraka haraka about 80% of the theorist today ni wao. therefore kusema mungu ni chanzo cha failure is just bunkum.

Unaifahamu Black Death ni nini? Unajua tofauti ya Black Death na hivyo "vifo vya misimu" (whatever that means) ?

Italy na Spain wana huge numbers amongst their population, unajua positions za Italy na Spain katika nchi zilizoendelea iko wapi? If anything una prove point yangu tu, kwa sababu hata katika nchi zilizoendelea, hizi Italy na Spain ndizo zinaongoza katika dini na ndizo zinshika mkia kimaendeleo.

Halafu hata huko Italy na Spain dini zinafifia, wanapata matatizo ku recruit priests. Zamani kuwa priest ilikuwa ni njia mojawapo ya ku escape poverty, lakini siku hizi hali si mbaya sana relatively speaking hawawapati. In any case Italy kanisa ni kama utamaduni zaidi kuliko dini per se, wtu wanaenda kanisani kuangalia mapambo, stained glass, kujumuika etc zaidi kuliko kufuata dini. Ni kma social club fulani hivi.

And this brings us to another point, waafrik ku flock makanisani na misikitini inaweza kukawa kunatokna sana na umasikini na kutafuta group therapy.

Hiyo figure ya 80% of theorist duniani ni "waisraeli" umeitoa wapi? Waisraeli wako about milioni sita, for sure milioni kumi hawajafika, hata ukimfanya kila mama baba na mtoto wa kiisraeli awe muumini wa mungu na "theorist" (again, I don't know exactly what you mean by this) katika ulimwengu wa watu bilioni 6.7 hawafiki hata 0.1%. Hawa wametoaje 80% ya "theorists", umetoa wapi figure hiyo?Una hakika na unachoongea au unajisemea tu?
 
Back
Top Bottom