Vikwazo 5 vinavyomsubiri Ofisini Rais Bola Tinubu wa Nigeria

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
1685172290708.png

Mei 29, 2023, Taifa la #Nigeria, lenye utajiri wa Dola Bilioni 441 GDP na idadi kubwa ya Watu Barani #Afrika (Milioni 223), litashuhudia kuapishwa kwa Rais Mpya, #BolaTinubu na Makamu wake #KashimShettima

Pamoja na ukubwa wa Uchumi wake, bado Nchi hiyo imekosa utulivu katika maeneo mengi ikiwemo hali ya Usalama, mfumuko mkubwa wa bei na gharama kubwa za maisha, hali inayochangia kuzorota kwa Uchumi wake

Matarajio ya wengi hata wale ambao hawakumpigia Kura, watataka kuona mabadiliko ya mapema ya hali hizo. Hapa chini kuna baadhi ya vikwazo vikubwa vinavyomusbiri ofisini Rais Tinubu

MAMBO 5 YANAYOMSUBIRI OFISINI RAIS MPYA WA NIGERIA

1. Ruzuku ya Mafuta: Licha ya kuwa kati ya Nchi zinazozalisha Mafuta kwa wingi, Nigeria imekuwa ikikumbwa na uhaba wa Mafuta. Bola Tinubu ameahidi kuifuta Ruzuku hiyo, hali inayotajwa kuwa itasababisha kupanda zaidi kwa bei ya Mafuta

2. Uungwaji Mkono: Licha ya kushinda nafasi ya Urais kwa 37% ya Kura, Tinubu atakuwa na kibarua kigumu cha kuliunganisha Taifa hilo linalooneka kugawanyika kutokana na mambo Ukabila pamoja na Vijana wengi kutomuunga mkono

3. Kuimarisha Uchumi: Mtihani mwingine uko kwenye eneo la Uchumi ambapo takwimu zinaonesha Mtu 1 kati ya 3 Nchini humo hana Ajira, Mfumuko wa Bei umefikia 22%, Watu Milioni 96 wanaishi chini ya Mstari wa Umasikini

4. Hali Mbaya ya Usalama: Kwa muda mrefu taifa hilo limekuwa likisumbuliwa na Matukio ya Utekaji, Mauaji na Mashambulio ya Kigaidi. Hata hivyo, Tinubu aliahidi kuwa akishinda atatumia Vikosi Maalumu kupambana na vitendo hivyo

5. Afya Yake Kutetereka: Kiongozi huyo amekuwa akitajwa kutokuwa sawa Kiafya ikiwa ni pamoja kusambaa kwa picha zinaoonesha akitembea na Mfuko Maalumu wa kuhifadhia haja ndogo na kusafiri Nje ya Nchi mara kwa mara kwaajili ya Matibabu

============
 
Hivi utajiri wote huo kwanini aendelee kuwa kwenye system
Huwa hawana aibu wala Soni
Haja ndogo haina break na hela zote hizo si bora akae tu hospital kuliko kuhangaika?
Hotuba yake ya kwanza wala haeleweki alikuwa anaongea nini

Nigeria ujanja mwingi na kuna maharamia kibao
Hiyo nchi sijui ina laana gani

Eti kisa ukae Lagos unaamua kuishi juu ya maji machafu yaliyooza kwa vinyesi na mikojo pamoja na kila aina ya uchafu

Hapo panaitwa Makoko, binadamu wanaishi kama mifugo
Screenshot_20230527_085044_Google.jpg
 
Duh! Mbona mzee sana 🤣. Wa Nigeria wameyakanyaga. The new Nigerian president is old pro max 🤣.
Kwa afya yake atatumia muda mrefu kujiuguza kuliko kuongoza........

Ila ndio wenye nchi hao, ngumu sana kwa kizazi kipya kupata madaraka makubwa huku Africa.
 
Back
Top Bottom