Uncle bright
JF-Expert Member
- Feb 9, 2023
- 1,040
- 4,080
Hapa nazungumzia yale makabila ambayo undugu una uzito mkuwa, kuna wale ambao mambo ya undugu hayanaga uzito wala sio shida.
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo ukinyoosha mkono utaambiwa subiri kwanza wenzako (wenye mawe) wachangie
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo ukiongea utaambiwa unakatisha maongezi usubiri upewe ruhusa, muda huo wenye nazo wanaongea kwa uhuru
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo, kikao kinaweza kuendelea bila uwepo wako na ukachukuliwa una kiburi warakusema "huyo mwacheni dawa yake inachemka, ukiwa na pesa kikao kinakusubiri na ukichelewa utadhaniwa kuna dharura muhimu imekupata na bado utapewa updates.
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo hata ukitoa wazo linapewa uzito mdogo, ni kama vile basi tu wamekuruhusu kuongea kwa kukuona unaweza kuanza kulalamika hupewi nafasi, ukimaliza kutoa point utaambiwa "haya asante anaefuata", ila wazo hilo hilo likitolewa na mwenye pesa linaanza kupewa uzito
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo utapewa soda pendwa Mirinda, Na hio Mirinda mtoto wa mwenye pesa akililia atakupokonya na huruhusiwi kumzuia, Muda huo wale wenye mizigo wameandaliwa juice natural za matunda, grand malt, n.k.
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo inabidi uchague sehemu ya kukaa kwa hesabu kali sana, huwa kkuna kawaida ya michango kuchangishwa, ukikaa huko mbele ama karibu na wenye mizigo wao wakianza kuchanga milioni mbili mbili, moja, laki 8, unaefuata utakuwa wewe mwenye uwezo wa elf 50 utaishia kuaibika kwa kusema ukweli ama kugharamika kwa kuchangia kuzidi uwezo wako pengine hata kukopa,
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo ukinyoosha mkono utaambiwa subiri kwanza wenzako (wenye mawe) wachangie
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo ukiongea utaambiwa unakatisha maongezi usubiri upewe ruhusa, muda huo wenye nazo wanaongea kwa uhuru
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo, kikao kinaweza kuendelea bila uwepo wako na ukachukuliwa una kiburi warakusema "huyo mwacheni dawa yake inachemka, ukiwa na pesa kikao kinakusubiri na ukichelewa utadhaniwa kuna dharura muhimu imekupata na bado utapewa updates.
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo hata ukitoa wazo linapewa uzito mdogo, ni kama vile basi tu wamekuruhusu kuongea kwa kukuona unaweza kuanza kulalamika hupewi nafasi, ukimaliza kutoa point utaambiwa "haya asante anaefuata", ila wazo hilo hilo likitolewa na mwenye pesa linaanza kupewa uzito
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo utapewa soda pendwa Mirinda, Na hio Mirinda mtoto wa mwenye pesa akililia atakupokonya na huruhusiwi kumzuia, Muda huo wale wenye mizigo wameandaliwa juice natural za matunda, grand malt, n.k.
Usipokuwa na pesa kwenye kikao cha ukoo inabidi uchague sehemu ya kukaa kwa hesabu kali sana, huwa kkuna kawaida ya michango kuchangishwa, ukikaa huko mbele ama karibu na wenye mizigo wao wakianza kuchanga milioni mbili mbili, moja, laki 8, unaefuata utakuwa wewe mwenye uwezo wa elf 50 utaishia kuaibika kwa kusema ukweli ama kugharamika kwa kuchangia kuzidi uwezo wako pengine hata kukopa,