Vijimisemo vya zamani

Vijimisemo vya zamani

Aisee, naomba unifanunulie kuhusu huu msemo...bado sijaelewa alikuwa anamaanisha nini hapo...hawa vijana wa yamoto band...wametisha! NITASHUKURU SANA

Wametishaje wakati hata huo msemo tu umekushinda kuuelewa!!!!!
 
Gashu -mwanamke
Sister duu nonino -mwanamke
Mzula -kofia
Mbangu, njagu, pongo -polisi
Denglizi -jeans.
Mtu akiwa haeleweki machepele flan aliitwa chale wakimfananisha na yule mchekeshaji Charles Chaplin.
Mtu ambae kachanganyikiwa kidogo aliitwa kipindi cha michezo RTD waqt huo kilikuwa saa mbili kasorobo sasa badala ya kusema mbili kasoro.
 
Kulikuwa na vijimisemo enzi zile nikivikumbuka, huwa vinanipa burudani. Vijimisemo kama ''Utabana ngenge - wakimaanisha utakoma! ,du kinaa - yaani hakuna shida, dole tupu - yaani powa tu!! Unakumbuka vimisemo vipi, hebu tupia hapa tukumbushane!!

Baba Ngenge! Nafikiri ilitokana na bendi moja ya Zaire ikiitwa Bana Ngenge Bakule Bakule
 
Zamani tukiona jamaa kubwakubwa la mwili tunawaita la kuchumpa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom