Vijana punguzeni dharau kwa Mwalimu Bashiru

Linguistic

JF-Expert Member
Mar 16, 2021
3,671
8,237
Nimekuwa Nikiona Vijana Wengi Wakituma picha za Mwalimu Bashiru Na Kuandika Maneno Ya Dharau na Kejeli juu yake.

Tupunguze dhihaka na Dharau Kwa Mwalimu Bashiru, Wakati Bashiru Akiwa SG Wa CCM Wala Hakuwa Mtu Wa Majigambo Kama Watangulizi Wake.

Aliwahi kuwakemea hadharani Viongozi Vijana Kama Nape, Makonda, Hapi Kwamba Wakajifunze Siasa na Uongozi Lakini leo Vijana Tena Wa CCM Mnatuma Picha Mkimdhiaki na Dharau Juu.

Vijana Msipomheshimu Mwalimu Bashiru Kwa Cheo Chake Cha Ukatibu Mkuu Mstaafu au Cheo Cha Ubunge Wake, Basi Mheshimuni Hata Umri Wake
 
Nimekuwa Nikiona Vijana Wengi Wakituma picha za Mwalimu Bashiru Na Kuandika Maneno Ya Dharau na Kejeli juu yake...
Siku zote ukiusimamia ukweli hautakusaliti!
Hata kama watu waovu wakikuchukia ukiwa mamlakani.

Watu wema na wengi, watakuthamini hata unapokuwa nje ya mamlaka.

Nadhani alikiuka misingi hii, usiwalaumu vijana wa ccm ni msingi huu unamuadhibu
 
Pamoja na mapungufu ambayo mengi yalitengenezwa na hayati kupeleka watendaji kutokufikiria athari za wanayotamka. Dr Bashiru ni asset kubwa sana kwa siasa za Tanzania endapo kama ataweza kurekebisha kauli zake za kibabe.

If CCM real needs reforms hawa na mzee Mndolwa wanatosha sana kuleta mabadiliko . Akili kubwa sana.
 
Alikosea ile kauli yake kwamba tutatumia dola kubaki madarakani,

Ameonekaga kigeugeu kwa sababu ya njaa , Mana amekuwa na mtazo tofauti wakati yupo CUF na alipopata wazifa CCM.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijui political science ya wapi inasema kwenye demokrasia vyombo vya dola vinatumika kubakisha chama cha siasa madarakani!
 
Back
Top Bottom