Vigogo wa CHADEMA wahamia CCM - Morogoro

Vigogo wa CHADEMA wahamia CCM - Morogoro

Slaa nae amekiri kuwa ana kadi ya ccm,tusubiri tutayasikia tu

Hata Dr Lwaitama nae amekiri ana kadi ya c.c.m ila yeye ni mwanachama mfu,kwa kua hajailipia hiyo kadi zaidi ya miaka 20,hajakipigia kura chama toka mfumo wa vyama vingi uingie Tanzania,na haoini kama C.c.m ni chama kitakachoweza kuikomboa nchi toka kwenye dimbwi la umaskini,so try to think out of the box,nini maana ya mwanachama mfu,na je kua mwanachama active wa chama unahitajika kufanya nini,kama wewe ni kijana nakusihi tu kua usiwe na mitazamo au fikra nyepesi bila kushirikisha ubongo!
 
Na Severin Blasio, Morogoro

ALIYEKUWA Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mkoani Morogoro, Bw. Abeli Ruanda pamoja na Mwenyekiti wa chama hicho wilayani Morogoro Bw. Rajabu Ally ’Kiselengo’, wametangaza rasmi kuhamia CCM.

Wakizungumzia na gazeti hili kwa nyakati tofauti, viongozi hao walidai kujiunga upinzani kwa bahati mbaya kama abilia awapo barabarani ambapo linapotekea gari lenye umbo na rangi nzuri hulazimika kuingia ukiamini ni chombo imara wakati mashine yake ni mbovu na haiwezi kuwafikisha popote.

Mbali na kuipongeza CCM kwa uimara wake, viongozi hao walisema vyama vya upinzani havina sera ya kuwakomboa Watanzania bali viongozi wake wanataka kujinufaisha.


Chanzo: Gazeti la Majira, Dec 4, 2012

Kabla ya kwenda CDM walikuwa chama gani? na kama hawakuona sera za kuwakomboa wakiwa CDM na wasisi na uwezo wao wa kusoma au uelewa loh kazi ipo.
 
Nimesikia tetesi mjini Morogoro kiongozi yoyote wa Chadema akijitoa na kutangaza, CCM wanampa kitita cha uhakika, naona ndivyo walivyofanya hawa jamaa ili watoke kimaisha. Mambo ya fedha yamewahamisha kama Kevin Yondani alivyoenda Yanga jamaa hela yote ya ufisadi wanayo wao. Azizi Abood anachangia kwenye siasa ile mbaya sasa hivi, anakata mshiko vibaya vibaya kwa sababu yeye kuongea sana hajui.

Swali ni kwamba watawapa hivyo vitita vya uhakika na wananchi wote aambao mwisho wa siku ni wapiga kura na ambao ni wengi?
 
Chama kinasambaratija hiki,siamini macho yangu.jana mjumbe wa kamati tendaji/katibu wa ilemela amebwaga manyanga,huko mbeya katibu wa wilaya wa cdm amenasa kwenye rushwa,na huku morogoro tena abiria wameshuka kwenye mkokoteni.haya yangu macho
haa mkuu yaani kisambaratike baada ya watu wawili ama watatu kutoka? Je ungekuwa unafuatilia ccm wanaotoka ambao hawatangazwi si ungesema ccm imekufa? Chama ni cha watu na si mtu mmoja. We ulisikia wapi msikiti au kanisa vimefungwa kisa waumini wamebadili dini? Inabidi tuwapongeze sana walio upinzani si kazi ndogo kwa tanzania,maana serikali ya magamba ina wanyanyasa kwa kila aina!
 
Nimesikia tetesi mjini Morogoro kiongozi yoyote wa Chadema akijitoa na kutangaza, CCM wanampa kitita cha uhakika, naona ndivyo walivyofanya hawa jamaa ili watoke kimaisha. Mambo ya fedha yamewahamisha kama Kevin Yondani alivyoenda Yanga jamaa hela yote ya ufisadi wanayo wao. Azizi Abood anachangia kwenye siasa ile mbaya sasa hivi, anakata mshiko vibaya vibaya kwa sababu yeye kuongea sana hajui.

Ni kweli, njaa inawamaliza. Leo asubuhi kwenye kipindi cha Star TV tuongee asubuhi nimemwona mmoja wa Ilemela amejivua gwanda!! Na amepongezwa na diwani wa CDM aliyevuliwa uanachama (Matata), nasikia huyu Matata ni tajiri, halafu owner wa Star TV naye zimo....unganisha dots na kufanya analysis ya tutakayoyaona kuelekea 2014/2015
 
Nimesikia tetesi mjini Morogoro kiongozi yoyote wa Chadema akijitoa na kutangaza, CCM wanampa kitita cha uhakika, naona ndivyo walivyofanya hawa jamaa ili watoke kimaisha. Mambo ya fedha yamewahamisha kama Kevin Yondani alivyoenda Yanga jamaa hela yote ya ufisadi wanayo wao. Azizi Abood anachangia kwenye siasa ile mbaya sasa hivi, anakata mshiko vibaya vibaya kwa sababu yeye kuongea sana hajui.
ni kweli mkuu unachezea waharabu koko wa moro nini? Akina abudi ni kuhonga wapinzani kwa kwenda mbele!
 
Kwa hiyo unapinga vigogo wa Chadema Morogoro hawajahamia CCM?

Ritz na Chadema ni mafuta na maji nadhani ni zaidi ya siasa, ungekuwa na uwezo wa kufuta Chadema nadhani ungeshaiondoa dhamani najua hii newz imekufurahisha sana. Unaweza ukasema ugomvi wako na Chadema chanzo ni nini?
 
Kila kiongozi anategemea kupata posho kutokana na utendaji wake. Hata Slaa (Katibu anayepata posho ya kibunge) analijua hili
walitegemea kupata posho, kwa hiyo anaona sera nzuri morogoro Abood kutoa basi kupeleka watu kwenye mazishi? njaa mbaya sana
 
Nimeona kamanda Sugu ameingiza wanachama zaidi ya 200 wapya na ni wananchi wa kawaida kabisa ambao maisha yao yamefanywa magumu na ccm.. Tunawahitaji wananchi wa kawaida kwenye kwenye ukombozi.. Sio hawa ambao walikuwa ni viongozi kabla ya kutoka ccm.. Wanapokuja hawa wanakuwa na malengo yao binafci au kutumwa ambayo mwisho wanakuja kugundua ni vigumu kupata yale waliyoyafuata wanaishia kuitisha mikutano na kutangaza kuhama kwa kashfa..
mkuu ni afadhali kupokea wanachama wa kawaida kuliko viongozi wa ccm,maana hao wamezoea pepo ndani ya ccm kuliko shida.
 
Wera wera tutawajua tu mliokuwa huku cdm mnasikilizia hela cdm,imekula kwenu rudini kwa boc wenu wa zaman mkapge mambo yenu ya ufisadi.cdm hakuna kuremba gwanda tu no majungu ,safari njema wa moro-sisi hatukuwapenda yeye aliwapenda saana..
 
mtanzania; bora umewaambia ukweli CDM mana kwao kuambiwa ukweli huo ni dhambi... siasa ni fedha hakuna mwanasiasa anayefanya kazi bure .. kila mtu anahaki ya kuhama chama sasa wameona CDM kuna matatizo si chama cha kuendelea mbele ni chama cha mtu mmoja au wawili basi wameamua kurudi CCM kwa imani kuwa ndio chama sahihi.. mbona tumeona ccm wanaenda chadema mbona hawasemi ni wachumia tumbo???.... ukweli uko wazi hao jamaa ndio walikuwa mhimili mkuu wa CDM morogoro sasa wameshatamba zao kwa babayao ....
hahaha mkuu sijakilenga chama chochote katika andiko langu....nimewalenga wanasiasa wote......Ngoja kwenye katiba mpya tutoe maoni ya kufutwa kwa ruzuku kwenye vyama vya siasa tuanze kubembelezana kushika nafasi za uongozi katika vyama vya siasa kama enzi za mwalimu :behindsofa:
 
Luanda tunamjua na sasa tumethibitisha alishirki kuchakachua kura za Juma Tembo Morogoro Kusini ambapo yeye Luanda alikuwa kampeni meneja wa Tembo,Leo Karogeris Mbunge na Mwenyekiti wa CCM mkoa anamrudisha kuwa mpiga debe wa CCM kwa njaa ya Luanda.
 
Haki ya kuhama chama ni yao hawazuiliwi na mtu... Na inakuwaje cdm inapowapokea wanachama wa ccm hawaonekani kuwa ni wachumia tumbo??? Lakini wanachama wa cdm wakienda ccm ni wachumia tumbo ,wananjaa....... Cha kutambua hakuna siasa bila pesa ... Hata dr.slaa na wote wanafanya m4c wanapata posho la sivyo tusingewaona majukwaani wakinadi sera......... Kikubwa cdm wajipange upya mana hakuna asiyejua hao jama ndo walikuwa majembe hapa moro kwa cdm........
 
Ritz na Chadema ni mafuta na maji nadhani ni zaidi ya siasa, ungekuwa na uwezo wa kufuta Chadema nadhani ungeshaiondoa dhamani najua hii newz imekufurahisha sana. Unaweza ukasema ugomvi wako na Chadema chanzo ni nini?

huyu si mtanzania halisi ... anaeneza chuki za kidini na ukabila akiwa na lengo la kuwagawa waTz ... lakini huu ujinga anaojaribu kufanya hautafanikiwa ...
 
Walikimbilia vyeo...haooo waende kwa wachumia njaa wenzao
MKUU VYEO VIPI TENA unamaanisha? si tayari walikuwa navyo huko chadema lakini wameamua kuvitema? labda utoe sababu nyingine.
 
Katika ulimwengu wa leo kama kuna kiongozi wa siasa anayeweza kusema anarudi CCM kwa moyo mmoja eti huko ndio kwenye ukombozi wa kweli basi ujue huyo ana kasoro akilini na si mkweli.
Nawahakikishia hata Mwenyekiti mwenyewe JK muwe wawili na mwambie kama anaweza kukuapia kuwa CCM ni chama cha ukombozi wa Watanzania? na uhakika kabisa atakataa kukuapia kwa vile hata yeye katika nafsi yake ya ukweli haamini hivyo. Sasa hawa wachumia tumbo ndio wa kuwasikiliza? unaweza kukuta hapo bahasha ya laki mbili tuu imefanya kazi.
 
Kwaheri zao, kuwa mpiganaji kunahitaji moyo. Acha waende CCM wakavune, CHADEMA itawasaidia kukomboa vizazi vyao kutoka kwenye mikono ya wazee wa kupeleka uswis vipesa vyao
 
It was predestined to be. Hawa ahkuwa sehemu ya mabadiliko; wamegundua kuwa hawatafit! wamefanya uchaguzi mzuri kwa ajili ya CDM!
 
Back
Top Bottom