Hapo kwenye RED sijui kwa ufahamu wangu hilo neno linamaanisha nini? inamaanisha hakuwa kiongozi bali alikuwa kwa hiyo kusema vigogo sio sahihi nikiwa namaanisha kwa sasa kuna viongozi wengine ila wao walikuwa hapo siku za nyuma.Na Severin Blasio, Morogoro
ALIYEKUWA Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mkoani Morogoro, Bw. Abeli Ruanda pamoja na Mwenyekiti wa chama hicho wilayani Morogoro Bw. Rajabu Ally Kiselengo, wametangaza rasmi kuhamia CCM.
Wakizungumzia na gazeti hili kwa nyakati tofauti, viongozi hao walidai kujiunga upinzani kwa bahati mbaya kama abilia awapo barabarani ambapo linapotekea gari lenye umbo na rangi nzuri hulazimika kuingia ukiamini ni chombo imara wakati mashine yake ni mbovu na haiwezi kuwafikisha popote.
Mbali na kuipongeza CCM kwa uimara wake, viongozi hao walisema vyama vya upinzani havina sera ya kuwakomboa Watanzania bali viongozi wake wanataka kujinufaisha.
Chanzo: Gazeti la Majira, Dec 4, 2012
Hiyo habari ina upotoshaji mkubwa sana.Kwa hiyo unapinga vigogo wa Chadema Morogoro hawajahamia CCM?
Mkuu hakuna utaratibu wowote wa kisheria unaoelekeza kufuatwa mtu unapotaka Kuhama chama ili kuhamia chama kingine. Hivyo mtu aliyehama chama, kadi ya uanachama haina kazi tena, yaani inakuwa ni takataka tu.Naomba kuuliza.
- Hivi kadi za vyama hurejeshwa kwenye vyama alikotoka mtu, au hukabidhiwa kwenye chama kingine ambako mtu amehamia?
- Kadi ya uanachama ni mali ya mtu au mali ya chama?
- Huyo mwanachama aliipataje, alipewa bure au aliinunua?
- Kama halipii ada za chama ni sahihi kumtambua kuwa ni mwanachama wako hai? Nafikiri hapa umtambue tu kuwa aliwahi kuwa mwanachama.
- Mwanachama mmoja akiondoka ni issue sana kuziba pengo lake? Hakuna wanachama wengine?
wewe si ndio msemaje wa CDM? Kanusha basi na utoe habari hiyo bila ushabiki.
wile wa malecela naona umekuja kivingine bada ya kula ban
Hiyo habari ina upotoshaji mkubwa sana.
Huyo Abel Luanda sio kiongozi wa Chadema kwa wakati huu anapohamia CCM.
Miezi mitatu iliyopita wakati wa Operation za M4C Morogoro alijiuzuru baada ya kusikia unafukuzwa (baada ya kugundulika ni mamluki ndani ya Chadema na alikuwa mstari wa mbele Kukwamisha M4C morogoro), na nafasi yake akakaimu mtu mwingine.
Habari zake ziliandikwa humu JF tena kwa Kina sana.