Watoto wanaokufa JKT serikali inalijua hilo? Nenda kashuhudie makambi ya Tabora,Tanga nk.Hivi watoto hao walipotoka Form six walipimwa afya kwanza kabla ya kwenda JKT? Sasa haya ona sasa wanakufa.[/QUO
Wacha porojo mbona sisi hatukufa tena tumetumikia mwaka mzima,siyo nia ya JKT kuua watu kwanza si wameenda kwa hiari yao!au walifikiri jeshi ni kwenda kucheza bongo fleva?matatizo ya kizazi hiki cha DOT.COM cha kula chips na mayai ukiwapa ugali tena dona na maharage wanadai wanaharisha sasa wale nini jeshini na mlo huko ndiyo huo,hawajawahi kushika jembe hata mche wa harage au mahindi hawajawahi kuuona toka kuzaliwa,jeshini unakutana na mashamba yanayohitaji palizi yanaitwa Embakasi,serengeti kulingana na ukubwa wake na palizi ni mkono sasa kama hauna ukakamavu umelelewa legelege afya lazima ilete mgogoro tu