Nilikua mishemishe kukusanya oda za detergents huku na kule, ni kawaida kula chochote msako bako Kwa bako, nimeingia hapa mara nika wakuta mateja wamejaa, ni njiani tu hawana shida hao, sasa kilicho nifikirisha Teja Mmoja akatoka vidonge rangi ni kama kijani sijui rangi gani ile, lakini kavitoa Kwa Siri huku anaficha nikajiuliza kama ni vidonge vya kutibu Kwa Nini Teja avifiche? Na sizani kama ni cocaine ile no ni vidonge ila nadhani wanapata stimu, hofu kama ni vidonge kawaida Kwa nini aangalie huku na huku na kama ni drug je vinauzwa pharmacy? Na je pharmacy wanatambua Hilo? Mana Kuna mtu Alisha nambia wahuni huvuta Hadi petrol, nilishangaa sana, hivo muonekano ni vidonge kama vidonge na vina rangi na vimo kwenye kipacckage yake kama paracetamol ilivo wekwa ila vyenyewe ni vina rangi Fulani hivi, dah