binti kiziwi
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 8,902
- 22,287
Angalia video ya For you(mdogo mdogo) ya q chilla
Angalia my no one remix Diamond
Angalia Wanjera dimpoz
Angalia nana Diamond
Angalka Mwana king Kiba
Kuna kichupa cha mdee nk
Hakuna cha ferari wala nini mkuu
Narudia tena the video is good lakini sio kwa viwango tunavyotarajia kutoka kwa Kiba kutokana na ushindani ulivyo sasa
Kichupi hiki hiki kama kilivyo kingetoka na audio pamoja tusingeona kama video hii ni nzuri ya kawaida, tungeiona kali sana kutokana na ukali audio
Cheketua ni bonge moja la songi limekaa ku dance dance flani
Kinachoharibu video zikichelewa ni zile video unofficial zinazowekwa youtube
Nyingi ya video za cheketua unofficial jamaa wanacheza kweli kweli sababu wimbo unachezeka, watu wanaanza kutengeneza itakua hivi hivi watu wanacheza sana
Sasa ikija kutoka tofauti ndio tunayo yaona
Hwaangalii tena uzuri sababu tu hawajakuta waliyotarajia
Mi naona video ni nzuri ila imekosa kitu kinachoongeza excitement (Taharuki), yaani haitii mshawasha wa kuiangalia tena na tena. Sijui imepooza au tatizo ninini? Ieleweke tu kuwa mtu akirudia rudia kuangalia video hajaenda pale kushangaa ferari, lamborgine wala magorofa. Huwa kuna kitu cha tofauti kinachoshawishi kuendelea kuangalia video. Wachezaji pia wamepooza yaani tabu tu. Ila video SIO MBAYA hata kidogo.
Kingine wazungu wanasema AS YOU SOW, SO SHALL YOU REAP, (kama ni kweli mashabiki wa kiba ndo walokuwa wanamponda diamond, sishangai mashabiki wa diamond wakimponda Alikiba) Ikumbukwe kuwa mashabiki tunatofautiana uwezo wa kuelewa, kuna wale low mind, kwao ni kupondaaaa tuuuu ndo wanachokijua. Tuvumiliane tu Si mashabiki sie hahahaaaaa
As long as kuna mashabiki zake wameipenda basi sawa, hakuna tatizo kabisa teh teh.