- Source #1
- View Source #1
- Tunachokijua
- Wadau wa JamiiCheck kupitia mitandao ya kijamii na jukwaa la JamiiCheck.com wamebainisha uhalisia wa video inayowaonesha watoto wakicheza na kimbunga. Wengi wameeleza kuwa video hiyo ina viashiria kuwa si video halisi bali imetengenezwa kwa kutumia Teknolojia ya Akili Unde (AI).
Baadhi ya Majibu ya wadau
my_country254 (Mdau wa JamiiCheck Instagram)
Dotto Shaaban (Mdau wa JamiiCheck Facebook)Hiyo ni AI, angalia huyo mtoto mwenye begi jeusi amerushwa mara mbili
chama_dulla_feb20 (Mdau wa JamiiCheck Instagram)AI, maana huyo dogo wa mwisho inaonekana begi lake limerushwa lakini yeye akatoka tena na begi! Wakati wote wana mabegi yao, je lile lililorushwa nje ni la nani!?
Kuna huyo mwenye suruali nyekundu kaingia kwenye upepo katoka ana suruali ya jeans
Ufuatiliaji wa JamiiCheck umejiridhisha kuwa video hiyo inayosambaa kupitia mitandao ya kijamii na kudaiwa kuwa ni ya tukio kutoka nchini India, imetengenezwa kwa Teknolojia ya Akili Unde (AI). Kwa kutumia nyenzo ya kidigitali ya kubaini maudhui ya AI ya Hive Moderation imetengenezwa kwa teknolojia hiyo kwa zaidi ya 99.4%.