Video nyingine ya uwindaji haramu Tanzania

Video nyingine ya uwindaji haramu Tanzania

Baada ya Mchg Msigwa kuanika huu ushenzi magazeti ya Rostam Azizz Mtanzania yalikuja na story ya ajabu ya kutetea ushenzi wa Green Miles kwamba wanaonewa na makampuni ya kimarekani.tena yakatumbukiza na udini ni bahati mbaya Rais wetu na vyombo vya ulinzi na yusalama vimelala pengine vinasubiri hali ikiwa mbaya ndio utasikia vinachukua hatua.

Ungesoma na gazeti la Jamuhuri ungeona jinsi hawa waandishi wetu wanavyojua kuendesha kesi na kutoa hukumu magazetini. Green miles ni wazi kabisa wamevunja sheria za kutosha za uwindaji na wanyama pori kwa ujumla. Wameonewa hawajaonewa ijulikane mahakamani, lakini mpaka sasa sijaona idara ya wanyama pori ikiwapeleka green mile mahakamani. Na hawa waandishi wetu wako kimya wanaandika habari za kuegemea upande mmoja kama wao sio watz. cc Manyerere Jackton
 
Last edited by a moderator:
Hawa wakuda walitakiwa washitakiwe aisei...! Siyo kufutiwa leseni haitoshi.
 
Ungesoma na gazeti la Jamuhuri ungeona jinsi hawa waandishi wetu wanavyojua kuendesha kesi na kutoa hukumu magazetini. Green miles ni wazi kabisa wamevunja sheria za kutosha za uwindaji na wanyama pori kwa ujumla. Wameonewa hawajaonewa ijulikane mahakamani, lakini mpaka sasa sijaona idara ya wanyama pori ikiwapeleka green mile mahakamani. Na hawa waandishi wetu wako kimya wanaandika habari za kuegemea upande mmoja kama wao sio watz. cc Manyerere Jackton

Acha kupotosha. Huoni madudu yote ya upendeleo wa wazi aliofanya Nyalandu kwa Wamarekani ambao nia yao ni kumiliki kitalu cha Green Miles kwenye Jamhuri la leo? Hujasoma kuhusu ubabe Wamarekani hawa wanaowafanyia washindani wenye vitalu vya uwindaji wanavyovitaka? Hata hao Wamarekani inawezekana kabisa wanafanya hivohivyo na pengine zaidi ya hao Green Miles.
 
Duuuh hadi kware? Waaauuu taifa hili? Jman nyama zote hizi zilizotundikwa wanakula saa ngapi? Huu ni ulaf wa mali zetu!
 
Acha kupotosha. Huoni madudu yote ya upendeleo wa wazi aliofanya Nyalandu kwa Wamarekani ambao nia yao ni kumiliki kitalu cha Green Miles kwenye Jamhuri la leo? Hujasoma kuhusu ubabe Wamarekani hawa wanaowafanyia washindani wenye vitalu vya uwindaji wanavyovitaka? Hata hao Wamarekani inawezekana kabisa wanafanya hivohivyo na pengine zaidi ya hao Green Miles.

Inawezekana kabisa green miles wameonewa hilo sijapinga, point yangu ni hii isingekuwa bora zaidi kwa waandishi wetu kuishinikiza serikali kuchukua hatua zaidi? Green miles ipelekwe mahakamani baada ya uchunguzi kufanyika waje na ushahidi wao kuonyesha kilichofanyika ni kinyume na sheria na hiyo kampuni ya wamarekani ichunguzwe pia wakipatikana wamevunja sheria nao wachukuliwe hatua.

Haisaidii hata kidogo kuandika kurasa kadhaa kwenye magazeti bila kuchukua hatua zaidi. Wengi wanasema ni upepo utapita. Ukitaka kuja very few pay attention to such matters look at this thread very few bothered to read it let alone say something. Hebu jiulize ni wangapi watakuwa wamesoma hilo gazeti. Watanzania wamepata faida gani.
 
kwani muwindaji anaruhusiwa kupiga wanyama wangapi?

The Company violated the Wildlife Conservation Act (No. 5 of 2009), following numerous irregularities in their hunting activities.

Some of the irregularities committed by the company include, allowing their visitors to hunt wild animals prohibited in the hunting licences contrary to section 19(1)(2) of the Act; visitors playing with young zebras contrary to section 19(1); allowing their visitors to chase and shoot the wildlife animals (Section 56 (1) (a) 1) and hunting under age wild animals (56 (1)).

Other mistakes included, allowing children less than 16 years of age to take part in hunting animals (Section 43 (20 (a) and visitors scaring the animals while hunting (Section 19 (1) and (2).

Ministry revokes hunting licences | In2EastAfrica – East African news, Headlines, Business, Tourism, Sports, Health, Entertainment, Education
 
Hivi karibuni Peter Msigwa aliweka hadharani video inayoonyesha wahusika wa Kampuni ya Uwindaji ya Green Miles Safaris Limited, wakitenda uhalifu wa wazi dhidi ya wanyama, wakikiuka sheria za Tanzania na kimataifa katika uwindaji.

Juzi Ijumaa tarehe 12 Agosti 2014, Motherboard wametoa video nyingine ikionyesha uharamia dhidi ya wayanma uliokuwa unafanywa na Green Miles Safaris Limited. Inadaiwa kuwa video ni sehemu ya video ndefu ya karibu masaa mawili inayoonyesha wakiwaua wanyama wakiwa kwenye gari, wakikimbiza na wanyama wachanga kwa gari, kuruhusu watoto wadogo kuwapiga risasi wanyama na kukamata mnyama mdogo na kuanza kumteza huku kichanga kikipiga kelele na kujaribu kukimbia bila mafanikio.

Utakachoona ni kama vile wawindaji hao wanawinda ndani ya uani wao bila wasiwasi wowote. Motherboard imejaribu kuwasiliana na Nyalandu na Msigwa lakini hawaku-respond, lakini mwakilishi wa Green Mile alisema kuwa serikali na Dallas Safari Club ndiyo wa kulaumiwa kwa unyanyasaji huu wa wanyama.

Green Mile Safari Co Ltd wanashangaa kwa nini unyanyasaji huo ulitokea mbele ya maafisa wa serikali. Wanadai kinachoitwa unyanyasaji wa wanyama kama kinavyoonekana kwenye video hapo chini ni mpango wa wapinzani wao kutoka Marekani kwamba hawashangai kwa kwa Nyalandu kuwasifu Dallas Safari Club baada ya kuwaadhibu Green Mile safari Ltd: Leaked Animal Abuse Video Shows Everything That's Wrong with Big Game Hunting | Motherboard






Tanzania haina mwenyewe,wanyama wetu wataisha hata wanyama wadogo wanauwawa ,watoto wanapewa rifle na kupiga ndege,wizara ya maliasili imelala na kuw biashara ya viongozi wetu
 
Last edited by a moderator:
Ungesoma na gazeti la Jamuhuri ungeona jinsi hawa waandishi wetu wanavyojua kuendesha kesi na kutoa hukumu magazetini. Green miles ni wazi kabisa wamevunja sheria za kutosha za uwindaji na wanyama pori kwa ujumla. Wameonewa hawajaonewa ijulikane mahakamani, lakini mpaka sasa sijaona idara ya wanyama pori ikiwapeleka green mile mahakamani. Na hawa waandishi wetu wako kimya wanaandika habari za kuegemea upande mmoja kama wao sio watz. cc Manyerere Jackton
Sheria ya wanyamapori ya 2009 iko wazi kuhusu upelelezi wa suala kama hili na kulifikisha mahakamani kama kutakuwa na ushaidi wa kutosha. Idara ya Wanyamapori ina wanasheria wenye uwezo wa kuchukua hatua hizi za kisheria. Kwanza itumie video hizo kama ushahidi wa mazingira "circumnstancial evidence" . Pili kuna watuhumiwa wakuu wawili ambao ni Muwindishaji Bingwa "Professional Hunter" ambaye ndiye mshauri mkuu wa Muwindaji wa Kitalii na Askari Wanyamapori ambaye majukumu yake ni kusimamia sheria na kanuni za uwindaji. Wawili hawa wanafahamika kwa uongizi wa Idara ya Wanyamapori. Kwa hiyo hakuna ugumu wa kupeleka suala hili mbele ya sheria. Inawezekana Idara inalifanyia kazi lakini ukimya wake umeanza kutoa tafsiri potovu hata kufikia TAHOA kutoa kwenye nagazeti tamko ambalo halikutegemewa dhidi ya wanachama mwenzao au mmoja wao katika tasnia ya uwindaji wa kitalii. Tamko hili lina utata na kuashiria mgawanyiko katika tasini ya uwindaji wa kitalii ambako upande mmoja unachochea moto. Suluhu na kwa heshima ya Idara ya Wanyamapori ni kulipeleka mbele ya mahakama ili haki itendeke kwa misingi ya katiba na sheria ya nchi.
 
Last edited by a moderator:
The Company violated the Wildlife Conservation Act (No. 5 of 2009), following numerous irregularities in their hunting activities.

Some of the irregularities committed by the company include, allowing their visitors to hunt wild animals prohibited in the hunting licences contrary to section 19(1)(2) of the Act; visitors playing with young zebras contrary to section 19(1); allowing their visitors to chase and shoot the wildlife animals (Section 56 (1) (a) 1) and hunting under age wild animals (56 (1)).

Other mistakes included, allowing children less than 16 years of age to take part in hunting animals (Section 43 (20 (a) and visitors scaring the animals while hunting (Section 19 (1) and (2).

Ministry revokes hunting licences | In2EastAfrica – East African news, Headlines, Business, Tourism, Sports, Health, Entertainment, Education


Kha!!!

Lakini hawa ni wawekezaji "sheria zenu haziwahusu"!
 
Hivi karibuni Peter Msigwa aliweka hadharani video inayoonyesha wahusika wa Kampuni ya Uwindaji ya Green Miles Safaris Limited, wakitenda uhalifu wa wazi dhidi ya wanyama, wakikiuka sheria za Tanzania na kimataifa katika uwindaji.

Juzi Ijumaa tarehe 12 Agosti 2014, Motherboard wametoa video nyingine ikionyesha uharamia dhidi ya wayanma uliokuwa unafanywa na Green Miles Safaris Limited. Inadaiwa kuwa video ni sehemu ya video ndefu ya karibu masaa mawili inayoonyesha wakiwaua wanyama wakiwa kwenye gari, wakikimbiza na wanyama wachanga kwa gari, kuruhusu watoto wadogo kuwapiga risasi wanyama na kukamata mnyama mdogo na kuanza kumteza huku kichanga kikipiga kelele na kujaribu kukimbia bila mafanikio.

Utakachoona ni kama vile wawindaji hao wanawinda ndani ya uani wao bila wasiwasi wowote. Motherboard imejaribu kuwasiliana na Nyalandu na Msigwa lakini hawaku-respond, lakini mwakilishi wa Green Mile alisema kuwa serikali na Dallas Safari Club ndiyo wa kulaumiwa kwa unyanyasaji huu wa wanyama.

Green Mile Safari Co Ltd wanashangaa kwa nini unyanyasaji huo ulitokea mbele ya maafisa wa serikali. Wanadai kinachoitwa unyanyasaji wa wanyama kama kinavyoonekana kwenye video hapo chini ni mpango wa wapinzani wao kutoka Marekani kwamba hawashangai kwa kwa Nyalandu kuwasifu Dallas Safari Club baada ya kuwaadhibu Green Mile safari Ltd: Leaked Animal Abuse Video Shows Everything That's Wrong with Big Game Hunting | Motherboard


Naomba unitumie kwa whatsapp namba hii +255787577755. Nina mpango wa kuishtaki hii serikali ya mashetani.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo letu Watanzania tumeishamua kujigawa makundi matatu:
1.Kundi hili linaumia na jinsi nchi yetu inavyoendelea kuwa maskini wakati kuna kila sababu ya hata kutokutegemea pesa za wafadhili! Na kundi hili hata waseme maovu mangapi watonekana kuwa wanawivu sababu hawajapata nafasi,na pia wanaonekana kuwa wachochezi.

Kundi la pili ni lile lililo watetezi wa maovu yote bila kujali kesho ya watoto na wajukuu zake itakuwa wapi,mradi tu leo ameshibisha tumbo lake kutoka kwa wenye serikali yao ambao wanadai wapinzani ni walevi na wapenda madaraka lakini leo tumewaona wanapinga Katiba ya wananchi tulioamua wabunge wakae miongo mitatu tu,lakini wanatuona watanzania ni wajinga na bado eti wanaongeza muda wa rais kukaa madarakani hawa ndiyo tunaolazimishwa kuwaamini eti hawapendi madaraka na hawa ndiyo wahongaji wakuu wa kundi hili ili wasipoteze muda kusikiliza kilio cha watanzania wenzao.

2.Kundi la mwisho ni lile bora liende chochote kwao ni sawa bila kujali kama kinawaathiri au la.

Hivyo hata hao akina Msigwa wakikesha wanasema maovu ya Wizara hiyo bado wataonekana ni wapenda madaraka.
 
Back
Top Bottom