BK hivi kwa mtu kama JM anajijua fika yeye anawindwa kwa udi na uvumba kuhusu kuwalipuwa wala rushwa na madhambi mengineo kweli akurupuke tu akachukue rushwa ya 10 milioni kwa mtu alifukuzwa kazi na PM inakujia akilini kweli. JM anamlaka yapi ya kumrudisha mtu kazini alie fukuzwa kazi na PM. Huyo mhasibu alietimuliwa kazi kwani JM ndie alie sababisha ama ni uzembe wake kazini hadi ukafika kwa bosi wake PM akatimiliwa.bro jerry mtu mdogo sana kufananisha na kesi ya kombe,jerry ni mwandishi wa habari kijana tu,kwa ninavyoijua bongo mimi,sawa inaweza kuwa polisi walimbambikia lakini inaonekana hata yeye alishaingia kingi mil 10 za chapchap kijana yeyote ofisi yeyote bongo haziachi mzee,haya licha ya mambo ya rushwa vitu alivyokamatwa navyo ndio msala zaidi,na sidhani kama mtu anaweza kubambikiwa kisha kutishwa asitoe ukweli hasa kwa mwandishi wa habari,anyway story yote ni kizungumkuti tu,mi nataka na yeye atoe maelezo yake tusikie,lakini kaambiwa hatakiwi kusema chochote na kakubali,ndo mana nasema kuna mahali muro atakua kakosea na ndio maana kakaa kimya atherwise tungesikia mengine kabisa.
Hivi huwa ukikutwa na bastola unaulizwa risiti au wanatakaga kujua kama unaimiliki kihalali?? mbona mimi nazidi kuwa confused?????
mimi namiliki bastola, kihalali....nyaraka hupaswi kutembea nazo , unless uwe unakwenda mbali na mkoa wako unaoishi.Ukiwa unamiliki bastola huwa unatakiwa kutembea na copy za vibali kuthibitisha kuwa huyo sila ni yako kihalali mtu yeyeote anayetembea na bastola muda wote hivyo vitu huwa anakuwa navyo kwenye gari lake na hata wakati wa kununua hiyo bastola wanakwmbia kabisa toa copy halafu wanaithibitisha maana huwezi tembea na document orignal muda wote kuna kupoteza ama zikachaa
inakua sahihi wakati mwingine....lakini sikila mahalakila muosha huoshwa!!!!........lol
hawa police nao Jerry akutwe na pingu kwani yeye ni police ..alinunua hizo pingu za kumfungia nani??
inafikirisha.mamii in this country anything is possible!!! mi hii habari inanipa kizunguzungu, toka nimeisikia jana mpaka sasa hivi bado kuna vitu nashindwa kuunganisha, ngoja nitulie kwanza.....!!!!!!
inafikirisha.
haya sheshe ndo hilo,na jamaa kakutwa na pingu na bastola risiti hana,watu wengine unawaona kama watiifu kumbe ni majambazi na waporaji,sasa hii unaweza sema polisi walimbambikia lakini inaonekana jamaa nae kabugi mahali,naona polisi wameamua tu kumshtua kama anajisahau kama na yéye mchafu vilevile.
Ina mana hiyo bastola kaanza kuimiliki jana? kama alikuwa nayo mbona hawakumkamata nayo kabla? Mbona mpaka alipovumbua jambo no yote haya yametokea? akili kumkichwa.............
Hivi jamani......kweli inakujia akilini mtu amakutwa na bastola iko full hana risiti alafu akaachiwa kweli kwa dhamana ya kujizamini mwenyewe???? labda hizo stori wapelekwe watoto wa chekechea hata mtua asie enda darasani hatawaelewa?????