ALU-MASOLI
Member
- Mar 2, 2010
- 57
- 1
Sijaiona hii video may be check vizuri na uwe sure na hi link
Nilikuwa kada wa CCM kuanzia mwaka 1995 hadi kufikia mwaka 2007 niliitupa rasimi kadi ya CCM na kuchukua kadi ya CHADEMA. Lakini kuwa kwangu CHADEMA hakunifanyi niwe kipofu kiasi cha kutokuona kwamba Lema alikosa busara katika kauli yake. Jiweke kwenye viatu vya Mulongo! Na wewe ndiyo kiongozi wa mkoa halafu unaowaongoza wanakufanyia hayo! Halafu uniambie how it feels!Waliyokosa busara ni polisi na mkuu wa mkoa,pamoja na yote hakukuwa na sababu za msingi za polisi kuwatawanya wanafunzi kwa mabomu ya machozi kwani hawakumfukuza Mkuu wa mkoa wala kumtupia mawe,wala hizo chupa alizosema ametupiwa kwani wangeondoka kimya kimya bila kutupa mabomu ya machozi wasingejulikana kama ni polisi?Mchochezi wa kwanza hapa ni Mkuu wa Mkoa na Polisi.Ifike mahali watanzania KOLEO tuiite KOLEO na siyo kijiko kikubwa.Inatia hasira na uchungu.Amka Lukolo hata kama wewe ni kada mzuri kuwa realistic,wafungue macho viongozi wetu.
Yah man hii link hai someki
Nimeangalia hii Video kwa makini; bila kuegemea mrengo wowote wa kiitikadi ninachoweza kusema Mh. Lema alivuka mipaka kwenda kuhutubia wanafunzi bila kukaribishwa na uongozi wa chuo, mbaya zaidi katika kuongea nao alikuwa akiwaita "makamanda" na hivyo kufanya uwepo wake pale kuwa wa kisiasa zaidi badala ya utatuzi wa tatizo la uvamizi wa vibaka. Hata kumpigia simu Mh. Mkuu wa mkoa haukuwa wajibu wake bali wajibu wa uongozi wa chuo kuomba msaada wa polisi kusaidia kutuliza fujo. Haya ni maoni yangu huru kabisa
i have nothing to add,video inaonyesha kila kitu,ile message ya mkuu wa mkoa kwenda kwa lema itam-cost mlongo.
Kama hayo ni maoni yako HURU basi una matatizo ya kiakili. Umeambiwa Lema alifuatwa na wanafunzi kwa kuwa anaishi jirani na chuo hicho. Pia aliwarudisha wanafunzi wasiandamane hadi kwa mkuu wa mkoa ila wamsubiri mkuu wa mkoa aende chuoni, sasa hapo unataka aombe kibari cha uongozi wa chuo kuwarudisha wanafunzi waliokuwa wanaandamana. Hayo ni maoni ya KITUMWA sio huru. SERUKAMBA
Kama hayo ni maoni yako HURU basi una matatizo ya kiakili. Umeambiwa Lema alifuatwa na wanafunzi kwa kuwa anaishi jirani na chuo hicho. Pia aliwarudisha wanafunzi wasiandamane hadi kwa mkuu wa mkoa ila wamsubiri mkuu wa mkoa aende chuoni, sasa hapo unataka aombe kibari cha uongozi wa chuo kuwarudisha wanafunzi waliokuwa wanaandamana. Hayo ni maoni ya KITUMWA sio huru. SERUKAMBA
Nimeamua kuweka video hapa ili watanzania muweze kuamua kama kweli Mhe. Lema alihusika na mauwaji na kuchochea vurugu chuo cha uhasibu Arusha kama mkuu wa Mkoa wa Arusha (Mulongo) anavyodai.
Part I
[video=youtube_share;_z-Cl4nNva0]http://youtu.be/_z-Cl4nNva0[/video]
Part II
[video=youtube_share;Y1Zy44AokSw]http://youtu.be/Y1Zy44AokSw[/video]
Hujaichakachua na kuweka yale ambayo roho yako inataka?!,mbona walipoweka ile ya Lwakatare mliwahi kusema imechakachuliwa?!hata sikuamini wewe una lako jambo siku hizi kwenye video unaweza fanya lolote lile,ukabadili ukweli kuwa uongo na uongo kuwa ukweli.