VIDEO: Kilichotokea Chuo cha Uhasibu Arusha, Lema alivyowatuliza wanachuo

Wampe kesi ya mauaji.chezea dola wewe!!,nanyinyi ambao muna kimbelembele cha maandamano endeleeni,si munakumbuka walikufa watatu mwanzo,wamesahaulika na maisha yanaendelea.kudadadadeki!!!,na kwa mungu virungu.
 
Nimeamua kuweka video hapa ili watanzania muweze kuamua kama kweli Mhe. Lema alihusika na mauwaji na kuchochea vurugu chuo cha uhasibu Arusha kama mkuu wa Mkoa wa Arusha (Mulongo) anavyodai.
Part I
[video=youtube_share;_z-Cl4nNva0]http://youtu.be/_z-Cl4nNva0[/video]

Part II
[video=youtube_share;Y1Zy44AokSw]http://youtu.be/Y1Zy44AokSw[/video]

kago kachomwa kisu na watu wasiojulikana hujambiwa Lema ndo kamuua acha kupotosha watu kijana, kuhusu fujo nan kanzia tutajua
 
Wakuu wa Mikoa ni janga la Taifa. Mbona mwenzie Kandoro hakupanic wana Mbeya walipotulizwa na Sugu na kusukuma gari lake hadi nyumbani kwake na kumwita Rais wa Mbeya? Naomba mwenye kumfahamu vizuri huyu Magesa Mulongo ni nani na kabla ya hapo alikuwa wapi na shule yake ikoje ili tuweze kumjadili vizuri hapa
 
Watawala wetu wamekosa hekima na uvumilivu! Inasikitisha Kikwete amemwona Mulugo anafaa zaidi kuliko mamilioni ya watanzania kuwa mkuu wa mkoa na ubongo wake huu mdogo! Appalling!
 
Tanzania ya unafiki ilikwishapita. Lema aliwatuliza wanachuo, wakatulia. Akawaeleza kuwa amewasiliana na Mkuu wa Mkoa, na yupo njiani anakuja. Ni dhahiri wanachuo walikubali ushauri wa Lema kutokana na kuwahakikishia kuwa Mkuu wa Mkoa anakuja, na kwamba Mkuu wa Mkoa angetoa kauli ya serikali. Mkuu wa Mkoa amekuja, kisha akaondoka. Lema aliyekuwa kiungo kati ya wanachuo na Mkuu wa Mkoa, kiutaratibu alikuwa anawajibika kuwaambia wanachuo ni kwa nini Mkuu wa Mkoa anaondoka.

Lema alifanya vema kuwaambia wanachuo kuwa Mkuu wa Mkoa amesema kuwa hawezi kuongea bila kipaza sauti, na kwamba wanachuo hawana adabu. Lema aliwaambia wanachuo maneno aliyotamka Mkuu wa Mkoa. Ulitaka awaambie uwongo? Hii si Tanzania ya kudanganyana tena, ni lazima kila kitu kitamkwe kwa ukweli. Na wala siyo Tanzania ya kufichiana udhaifu.

Kilichodhihirika hapa ni kuwa Mkuu huyu wa Mkoa, kama walivyo wengi wa awamu hii ya JK, hana uwezo wa kuongoza, anaishi kwa ubabe. Viongozi hawa hawatufai hata kidogo. Namwunga mkono kwa 100% Lema, alifanya kazi yake vizuri kama kiongozi na kama mwakilishi. Bahati mbaya Mkuu wa Mkoa hana basics za uongozi, sijui aliokotwa wapi!!

Hii video imemuumbua Lema. Kwa hakika hapa Lema hakwepi. Ni wazi kwamba alichochea vurugu, na amemdharau mkuu wa mkoa.

Kwanini yeye asingeacha hayo maneno yasemwe na mkuu wa mkoa mwenyewe? Haya bwana ameyatafuta mwenyewe. Mwanzoni alifanya vizuri sana na ameongea maneno ya msingi sana. Lakini kuanzia baada ya mkuu wa mkoa kufika, Lema hakupaswa kuendelea kuwa msemaji tena.

Kwa busara za kawaida kabisa, alipaswa amuachie mkuu wa shule na mkuu wa mkoa waseme wanayotaka, lakini kitendo cha kusimama na kuwatangazia alichokisema mkuu wa mkoa na kuwatamkia wanafunzi kwamba hawa ndiyo aina ya viongozi tulionao na nini ambacho mkuu wa mkoa alipaswa kufanya hakikuwa sawa kabisa. Kwanza alipaswa aheshimu uamuzi wa mkuu wa mkoa kufika eneo la tukio.

Katika hili sitaweza kumtetea Lema. Amelikoroga.
 
Wampe kesi ya mauaji.chezea dola wewe!!,nanyinyi ambao muna kimbelembele cha maandamano endeleeni,si munakumbuka walikufa watatu mwanzo,wamesahaulika na maisha yanaendelea.kudadadadeki!!!,na kwa mungu virungu.
Tukisema CCM ni wauwaji kuna punguwani wanakataa ona wameanza kujisahau.....
 
Soma vizuri ili uweze kuelewa kikamilifu:
1) Lema hakwenda mwenyewe bali aliitwa na wanachuo
2) Lema ndiye aliyempigia simu Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Chuo alitoroka, haikujulikana alikwenda wapi
3) Ni Lema ndiye aliyewazuia/kuwatuliza wanachuo wasiandamane kwa kuwaahidi kuwa Mkuu wa Mkoa anakuja
4) Baada ya Mkuu wa Mkoa kuja na kuondoka bila ya tamko la serikali, Lema kama mwakilishi alikuwa na wajibu wa kuwaambia Wanachuo kwa nini Mkuu wa Mkoa ameamua kuondoka
5) Kuzomewa kwa Mkuu wa Mkoa kulitokea kabla ya Lema kuwaambia wanachuo alichotamka Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo kuzomewa kwa Mkuu wa Mkoa hakuna uhusiano na hotuba ya Lema kwa wanachuo baada ya Mkuu wa Mkoa kuondoka
6) Hata baada ya Lema kuwaambia wanachuo maneno ya hovyo aliyotamka Mkuu wa Mkoa, wanachuo waliendelea kuwa watulivu
7) FFU wamekwenda kuwashambulia wanachuo chuoni kwao wakati kukiwa hakuna vurugu
8) Lema alitaja kampeni za udiwani kuelezea kutokuwajibika kwa mtu aliyestahili kushughulikia tatizo la wanachuo lakini halikuwa jambo alilokuwa akilijadili. Mara ngapi tumemsikia JK akiwa msibani akiongelea kuwa nimesikia habari ya kifo hiki nikiwa nahudhuria mkutano fulani? Ina maana kwa kutaja mkutano kwenye msiba, tayari ni kosa? Ungemsikia Lema kwenye tukio hili akisema kuwa, 'mnaona hawa viongozi hawawasaidii, mkitaka kusaidiwa chagueni diwani wa CHADEMA; hapo ungekuwa na sababu ya kumlaumu.

Hitimisho: Mkuu wa Mkoa hafai, hana uwezo wa uongozi, hastahili kuwa hata Afis Mtendaji wa Kijiji. Is an exceptionally hopeless leader with no qualities.

Ulukolokwitanga Sikatai Lema kwenda kama jirani ila kwenye maneno yake aliyowaambia wanafunzi baada ya mkuu wa mkoa kudai kipaza sauti ndipo aongee yalivuka mipaka na yaliwaongezea wanafunzi hasira na huo ndio unaitwa uchochezi; after all baada ya mkuu wa mkoa kufika pale chuoni; mwenyeji wake alistahili kuwa Mh. Lema au uongozi wa chuo? Pili, kueleza mambo ya michakato ya chaguzi za madiwani nayo yalikuwa ni mahali pake?
 
Mimi nasema ule tu mwitikio wa mkuu wa mkoa kwenye tukio hili ulikuwa ni ustaarabu tosha. Maana angetaka angegoma na kumtuma mkuu wa wilaya au afisa mwingine yeyote wa mkoa au wilaya. Lakini yeye alitoka mwenyewe ofisini kwenda kuonana na wanafunzi. Hilo pekee linastahili pongezi. Yaliyojiri hapo, haikuwa kazi ya Lema kuyaelezea.

Mkuu, hivi wewe ukiamka asubuhi kwenda shule unastahili kupongezwa? Yaani kazi ama shughuli ama wajibu wako mwenyewe bado unataka upongezwe, umeitoa wapi wewe hii? Mrejesho kwenye jambo lolote ni muhimu na ndo maana ni lazima wanachuo waambiwe kisa na mkasa cha mkuu wa mkoa kukataa kuongea nao, maana toka mwanzo aliwahakikishia kuwa ameshanogea naye na wavute subira, what else ulitaka?

Hitimisho: Mkuu wa Mkoa hafai, hana uwezo wa uongozi, hastahili kuwa hata Afis Mtendaji wa Kijiji. Is an exceptionally hopeless leader with no qualities.

Mkuu, nimepata mashaka kuhusu uwezo wake, amesahau kuwa anaongoza watu milioni mbili na ushee ambao wanatofautiana kwa kila hali, kuanzia uwezo wa kufikiri, elimu, uchumi, itikadi, malezi na kadha wa kadha. Haya kwanini Arusha tu na hawezi kutuliza, Loliondo shida, mjini napo shida, na bado mkuu wa mkoa yupoyupo tu ofisini kama kawaida, kazi yake ni nini kama sio kulinda maslahi ya wananchi? Mungu tuponye.
 
Nimeangalia weee video zote mbili, sijaona kosa la Lema wala wanafunzi!! Yule mkuu wa mkoa anaonekana hana akili kabisa, alishindwa kabisa kusama upepo wa wanafunzi kwa wakati ule walitakiwa waambiwe nini!!!!!!!
 
Nilikuwa najiuliza kila siku kwa nini Lema anapendwa sana huko arusha baada ya kuona video hizi nimeamini huyu jamaaa ni kiongozi wa kipaji. Anaweza kushika wadhifa wowote ule regadless ya shule yake. Na kwa mkuu wa mkoa anazidi kuonyesha kuwa mtu aliye mchagua aliangalia tu list ya marafiki zake. ni sifuri kabisa.
 
Mkuu, hivi wewe ukiamka asubuhi kwenda shule unastahili kupongezwa? Yaani kazi ama shughuli ama wajibu wako mwenyewe bado unataka upongezwe, umeitoa wapi wewe hii? Mrejesho kwenye jambo lolote ni muhimu na ndo maana ni lazima wanachuo waambiwe kisa na mkasa cha mkuu wa mkoa kukataa kuongea nao, maana toka mwanzo aliwahakikishia kuwa ameshanogea naye na wavute subira, what else ulitaka?
Mkuu sikatai mawazo yako. Ila haikuwa kazi ya Lema tena kurudisha feedback kwa wanafunzi juu ya nini amesema mkuu wa mkoa. Ilikuwa ni kazi ya mkuu wa shule. Soma post ya Ulukolokwitanga. Lema hakuwa mwenyeji wa mkuu wa mkoa? Na kiprotacally, si Lema aliyepaswa kuwajibu wanafunzi. Na hata kama aliona ni vema kuwajibu kwa kuwa ndiye aliyewaahidi kwamba amemwita, basi angewaambia tu kwamba unafanyika utaratibu wa kupata mic ili aweze kuongea na ninyi. Au kauli zile za eti woga ndiyo adui mkubwa .... mara sijui hawa ndiyo aina ya viongozi tulionao na kuanza kuelezea namna kiongozi anavyopaswa kuwa.... blabla yalikuwa yanini? huko ndo kulikuwa ni kuwapandisha hasira wanafunzi. Na pia ilikuwa ni dharau kwa mkuu wa mkoa. Ni vizuri tuwe wakweli kwamba Lema alikosa hekima. Na inawezekana ana bifu binafsi na mkuu wa mkoa. Kama mkuu wa mkoa alikubali kuja basi ni dhahiri kwamba alikuwa na nia njema. Na ni kweli kwamba mic ilikuwa mhimu ili kuweza kuongea na ule umati. Na kwa kuwa mkuu wa mkoa alisema hayo na makamu mkuu wa shule, basi hakukuwa na sababu ya Lema kumsemea. Angemwachia makamu mkuu wa chuo kufanya hayo.
 
Last edited by a moderator:
Hii video imemuumbua Lema. Kwa hakika hapa Lema hakwepi. Ni wazi kwamba alichochea vurugu, na amemdharau mkuu wa mkoa.

Kwanini yeye asingeacha hayo maneno yasemwe na mkuu wa mkoa mwenyewe? Haya bwana ameyatafuta mwenyewe. Mwanzoni alifanya vizuri sana na ameongea maneno ya msingi sana. Lakini kuanzia baada ya mkuu wa mkoa kufika, Lema hakupaswa kuendelea kuwa msemaji tena.

Kwa busara za kawaida kabisa, alipaswa amuachie mkuu wa shule na mkuu wa mkoa waseme wanayotaka, lakini kitendo cha kusimama na kuwatangazia alichokisema mkuu wa mkoa na kuwatamkia wanafunzi kwamba hawa ndiyo aina ya viongozi tulionao na nini ambacho mkuu wa mkoa alipaswa kufanya hakikuwa sawa kabisa. Kwanza alipaswa aheshimu uamuzi wa mkuu wa mkoa kufika eneo la tukio.

Katika hili sitaweza kumtetea Lema. Amelikoroga.

form four 2012 huyu.. haelewi maana
 
Dah, kweli akili ni nywele...sasa sijui mkuu kuwa na upara ni athari au ?
He could hv used simple words, kuwatuliza wanafunzi lkn hata sura yake ukiiangalia ni ubabe tu na hawajui body language at times inaweza athiri mtu/watu unaoongea nao !! Kuongea kwa kutishia, eti mmeitaka serikali na serikali hii hapa inaashiria nini..!!

Dawa ni kuwapigia kura tuu. Hivi hizi kozi za ngurdoto n.k wanafundishwa nini haswa..?? Badala ya kumtuma mbunge kuwa hawezi kuongea bila kipaza sauti, angesema yeye mwenyewe, hata kusingizia kuwa anabanja au hana sauti !!

Ili tupate maendeleo, tunahitaji watu kama Lema, unawachana chana hadharani !!
 
Wakuu wa Mikoa ni janga la Taifa. Mbona mwenzie Kandoro hakupanic wana Mbeya walipotulizwa na Sugu na kusukuma gari lake hadi nyumbani kwake na kumwita Rais wa Mbeya? Naomba mwenye kumfahamu vizuri huyu Magesa Mulongo ni nani na kabla ya hapo alikuwa wapi na shule yake ikoje ili tuweze kumjadili vizuri hapa

Ni Mjita mmoja mjinga mjinga aka mpenda sifa!! Alikuwa DC mbeba maboksi ya JK kule Bagamoyo! Baada ya kumfurahisha Mr FAST JET ndiyo akamzawadia u-RC Arusha ili akamdhibiti LEMA kwa kumbwaga Chakula ya wakubwa Dr aliyepelekwa Tanzania Embassy NRB. Chezea K weweeeee!!
 
Mkuu video haifunguki, nilishaanza kupiga makofi wa wa wa !!!

CC: Kwa wale wakipendao chama chao hata kama hakina mashiko kwa maskini wa tanzania!!! Imagine over 60% are poor!! And few in heaven!! To hell!! Kweli haya ndiyo maisha na ukombozi aliopigania marehemu baba wa Taifa hili? Sitakusahamu mwalim, kama si wewe nisingesoma mama yule mjane asingeweza kunisomesha!!
Nashangazwa na watanzania walivyokuwa walalamikaji, kwamba wanahitaji ukombozi wakati huohuo wanadai nchi hii ilikombolewa. Yote sawa, lakini sikumbuki katika historia kama kweli tulipata ukombozi kama ujinga, umaskini na maradhi ndiyo waliokuwa maadui toka uhuru na baada ya uhuru, basi ukombozi na Uhuru haukuwa wa kweli ni kiini macho. Hakuna cha Mwalim wala mwanafunzi tusidanganyane hapa. Nilitarajia waliokuwepo wangeweka misingi imara ya kiuchumi, kijamii, kielimu na hata kisaikolojia. Msingi haukuwa imara, nyufa kibao ndiyo maana sasa watu wanagombea fito. Eti leo ndiyo babara zajengwa, mipango miji haikuwepo, alifanya ninin huyo anayesemwa alitengeneza kama siyo kuharibu, dhulma za mali za watu akidai kutaifisha mali za umma, mashule taasisi za kijamii, mashamba na alishindwa kuendeleza kama rafiki yake Mugabe. HE was a messed up Conspirator. Uhuru kwa heri Ukoloni karibu.
 
Nimeangalia weee video zote mbili, sijaona kosa la Lema wala wanafunzi!! Yule mkuu wa mkoa anaonekana hana akili kabisa, alishindwa kabisa kusama upepo wa wanafunzi kwa wakati ule walitakiwa waambiwe nini!!!!!!!

Atenge bajeti akasomo "crisis management"?
 
Back
Top Bottom