mirindimo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2009
- 1,116
- 2,481
Mwenyekiti wa Wamiliki wa Malori nchini Tanzania TAMSTOA, Chuki Shabani amesema kwamba kuna baadhi ya watendaji wa Serikali wanamdanganya Mhe. Rais.
Akijibu swali la mwandishi kuhusu ufanisi wa bandari ya Kwala kufanya kazi kama ilivyoahidiwa kuwa itakuwa ni asilimia 100% amesema siyo kweli wanamdanganya Rais Kwala haifanyi kazi kama walivyomuahidi.
Amesema kwamba wiki iliyopita alifanya ziara ya kutembelea Kwala kwenda kuzungumza na baadhi ya wananchi na kuwauliza kwa siku zinaingia contena ngapi wakasema ni 20 tuu pekee.
Aidha katika hatua nyingine amesema miundombinu ya kiutendaji katika eneo hilo haiko tayari kwa kazi ambayo ilitangazwa kuwa ni mchaka mchaka wa asilimia 100% kwani baadhi ya mashine zingine zimekufa hazifanyi kazi.
Hiyo iliyopo ni moja hivyo inazidiwa kitendo ambacho kinapelekea madereva kukaa siku nyingi kusubiria kupakia mizigo katika eneo hilo.
Chanzo: CHAWAMATA TV
Akijibu swali la mwandishi kuhusu ufanisi wa bandari ya Kwala kufanya kazi kama ilivyoahidiwa kuwa itakuwa ni asilimia 100% amesema siyo kweli wanamdanganya Rais Kwala haifanyi kazi kama walivyomuahidi.
Amesema kwamba wiki iliyopita alifanya ziara ya kutembelea Kwala kwenda kuzungumza na baadhi ya wananchi na kuwauliza kwa siku zinaingia contena ngapi wakasema ni 20 tuu pekee.
Aidha katika hatua nyingine amesema miundombinu ya kiutendaji katika eneo hilo haiko tayari kwa kazi ambayo ilitangazwa kuwa ni mchaka mchaka wa asilimia 100% kwani baadhi ya mashine zingine zimekufa hazifanyi kazi.
Hiyo iliyopo ni moja hivyo inazidiwa kitendo ambacho kinapelekea madereva kukaa siku nyingi kusubiria kupakia mizigo katika eneo hilo.
Chanzo: CHAWAMATA TV