Vichocheo vya maisha vinazungumza nini juu ya kusudio la uhai?

KENZY

JF-Expert Member
Dec 27, 2015
26,215
56,855
Ni dhahiri kabisa pasipo uhai hakuna maisha!,kwa maana maisha ni uhai.

Lakini lipo jambo moja tata kuhusu uhai!. Nalo ni kusudio la uhai.

Tukijaribu kuangalia mfano wa vitu vidogo ambavyo vimetengenezwa na binadamu bila kusita vitu hivyo utapata kusudio lake.. lkn jambo lakushangaza kitu ambacho ni maana nzima ya uukiumbe hai kusudio lake bado ni mtambuka!.

Nafahamu yameandikwa mengi juu ya kusudio la uhai wetu lkn hata hivyo bado yamekuwa si majibu yenye uthibitisho wa kutosha!.. kukosa kwangu kwa majibu hayo kumenifanya kila siku kufikiri juu ya kusudio la uhai,lakini napo bado sijapata jibu la uhakika.

Leo nimeangazia vichocheo tulivyonavyo labda vinaweza Kuwa kielelezo au njia ya kufumbua swali hili tata!.. si kwamba ninalo jibu, hapana Sina hata punje lkn itafaa zaidi Kama tukiunga fikra zetu labda tunaweza pata kitu kipya zaidi!.

Uhai wetu umeegemezwa na vichocheo mbalimbali,navyo ndio vimekuwa nguvu ya msukumo ktk maisha yetu,Ni ukweli ulio dhahiri vichocheo hivyo ndio chachu ya uhai wetu!. Kama kutakuwa hakuna vichocheo basi hata uhai unakuwa ni sawa na gari lililokosa njia au uelekeo wa kwenda!.. kwa ambao bado hawajajua nazungumzia nini ni Kuwa nazungumzia hamu ama hisia tulizonazo ndio vichocheo vya maisha.

Kama tusingekuwa tunahamu ya kufanya mapenzi basi kusingekuwa na uzalianaji!,Kama kula kusingekuwa na hamu au kuhisi njaa basi uhai ungetetereka na ama usingekuwepo kabisa!. hata wewe unafanya kazi ili upate hela ilikusudi utimize malengo yako na hayo malengo ndio tageti yako na hiyo tageti basi nyuma yake kuna kichocheo na nyuma ya kichocheo Kuna uhai!..

Sasa swali la msingi ni kwanini uhai uwe na matamanio(vichocheo) ili uzidi kukua(kwa maana ya kuzaliana)..?

Ukifikiri kiundani unaona kabisa mienendo yetu imekuwa coded!,juu ya swala la nani katufanya Kuwa hivyo (Kuwa coded) kila mtu anamajibu yake ambapo wengi wao huishia kusema Kuwa ni Mungu.. okay ni vizuri hata mimi ntaishia hapo lkn tutatofautiana ni Mungu yupi!! (Nimegusia tu hapo).

Kama vichocheo hivyo vyote vimesimikwa kwa misingi ya kuutetea uhai sasa kwa kuviangalia vyenyewe je,tunaweza kupata kusudio la uhai..?

Kwa kupitia vichocheo hivyo binadamu amekuwa ktk maendeleo ya vitu vingi,mfano teknolojia n.k hayo ni matokeo ya vichocheo lkn bado haileti picha ya kusudio la uhai wetu!.

Labda niandike hivi kama tupo ili tufaidishe kitu fulani basi kitu hicho ni kipi..?
Kama tupo kwaajili ya maendeleo basi maendeleo hayo anayafaidi nani ikiwa tunakufa..? Au hakuna msamiati faida ktk ulimwengu..?

Au ndo tuseme Kuwa kilichoumbwa ama kutengenezwa hakipaswi kujua kusudio la chenyewe kuwepo,isipokuwa alietengeneza akijua basi inatosha..?😅

Namaanisha kikombe hakijui kusudio lake kwanini kipo lkn binadamu akijua kusudio lake la hicho kikombe basi ndo inatosha..?
Kama ni hivyo Basi kwanini tuwe na kimuhemuhe cha kujua kusudio letu..?

Najaribu kuweka maswali ili kuleta utafakari lkn swali kuu ni kichwa cha mada hivyo haya mengine ni vichokozi tu ili kufikiri kwa upana..

Nimejaribu kuchokoza kwa upana wake na hayo ndio yangu machache,so karibuni kwa mjadala na majibu.
 
Specifically kabisa wewe, ukiulizwa kusudi la kuwa hai mpaka sasa unadhani ni Lipi au Yapi?
 
Mpaka sasa kunauwezakano kuwa binadamu bado hajajua kwanini yupo duniani. Yaani lengo kuu la yeye kuwepo duniani.

Mambo mengi anayofanya binadamu kwa sasa ikiwepo kufanyakazi,biashara,kula na mengine mengi ni mambo ambayo yanamuwezesha binadamu kumudu kuwepo duniani ili akamilishe lengo lake la kuwepo duniani. Cha ajabu lengo hilo alijulikani.

Mfano.
Lengo kuu la kutengenezwa simu ni kurahisisha mawasiliano kama kupiga,kutuma sms au kwa njia ya internet. Hayo mambo ya simu kuwa na saa,gem,mziki,video,kikokotoo n.k ni mbwembwe tu.

Sasa ili ufikie lengo hili katika simu ni lazima simu iwe na vocha(bando) na chaji. Vitu kama chaji na vocha katika simu tunaweza kuvifananisha na chakula,biashara na kazi kwa binadamu kwani vitu hivi vinamsaidia tu binadamu aweze kufikia lengo la kuwepo duniani na vitu hivyo haviwezi kuwa ndiyo lengo la binadamu kuwepo duniani.

Maoni yangu.
Lengo la binadamu kuwepo duniani ni kuhakikisha MUNGU ANAKUWA HAI ILI KUKAMILISHA KUSUDIO LAKE LA YEYE KUIUMBA DUNIA.

Inavyooneka binadamu na Mungu ni vitu viwili vinavyotegemeana sana. Yaani binadamu asingekuwepo duniani kama kungekuwa hakuna Mungu na Mungu ili awepo duniani basi lazima binadamu wawepo hapa duniani.
 
Mpaka sasa kunauwezakano kuwa binadamu bado hajajua kwanini yupo duniani. Yaani lengo kuu la yeye kuwepo duniani.

Mambo mengi anayofanya binadamu kwa sasa ikiwepo kufanyakazi,biashara,kula na mengine mengi ni mambo ambayo yanamuwezesha binadamu kumudu kuwepo duniani ili akamilishe lengo lake la kuwepo duniani. Cha ajabu lengo hilo alijulikani.

Mfano.
Lengo kuu la kutengenezwa simu ni kurahisisha mawasiliano kama kupiga,kutuma sms au kwa njia ya internet. Hayo mambo ya simu kuwa na saa,gem,mziki,video,kikokotoo n.k ni mbwembwe tu.

Sasa ili ufikie lengo hili katika simu ni lazima simu iwe na vocha(bando) na chaji. Vitu kama chaji na vocha katika simu tunaweza kuvifananisha na chakula,biashara na kazi kwa binadamu kwani vitu hivi vinamsaidia tu binadamu aweze kufikia lengo la kuwepo duniani na vitu hivyo haviwezi kuwa ndiyo lengo la binadamu kuwepo duniani.

Maoni yangu.
Lengo la binadamu kuwepo duniani ni kuhakikisha MUNGU ANAKUWA HAI ILI KUKAMILISHA KUSUDIO LAKE LA YEYE KUIUMBA DUNIA.

Inavyooneka binadamu na Mungu ni vitu viwili vinavyotegemeana sana. Yaani binadamu asingekuwepo duniani kama kungekuwa hakuna Mungu na Mungu ili awepo duniani basi lazima binadamu wawepo hapa duniani.
Una maana kwamba kuna uwezekano kuwa Mungu anaweza kuw like ha exist kama binadamu asingekuwepo!.?
Kuna imani ambazo zina amin Mungu ana viumbe wengine wengi wanaomwabudu huko aliko na viumbe hivyo vina recognize Uungu wake.

So hata bila uwepo wa binadam, bado uwepp wake ungeku una stand valid.
Unalizungumziaje hili
 
Mpaka sasa kunauwezakano kuwa binadamu bado hajajua kwanini yupo duniani. Yaani lengo kuu la yeye kuwepo duniani.

Mambo mengi anayofanya binadamu kwa sasa ikiwepo kufanyakazi,biashara,kula na mengine mengi ni mambo ambayo yanamuwezesha binadamu kumudu kuwepo duniani ili akamilishe lengo lake la kuwepo duniani. Cha ajabu lengo hilo alijulikani.

Mfano.
Lengo kuu la kutengenezwa simu ni kurahisisha mawasiliano kama kupiga,kutuma sms au kwa njia ya internet. Hayo mambo ya simu kuwa na saa,gem,mziki,video,kikokotoo n.k ni mbwembwe tu.

Sasa ili ufikie lengo hili katika simu ni lazima simu iwe na vocha(bando) na chaji. Vitu kama chaji na vocha katika simu tunaweza kuvifananisha na chakula,biashara na kazi kwa binadamu kwani vitu hivi vinamsaidia tu binadamu aweze kufikia lengo la kuwepo duniani na vitu hivyo haviwezi kuwa ndiyo lengo la binadamu kuwepo duniani.

Maoni yangu.
Lengo la binadamu kuwepo duniani ni kuhakikisha MUNGU ANAKUWA HAI ILI KUKAMILISHA KUSUDIO LAKE LA YEYE KUIUMBA DUNIA.

Inavyooneka binadamu na Mungu ni vitu viwili vinavyotegemeana sana. Yaani binadamu asingekuwepo duniani kama kungekuwa hakuna Mungu na Mungu ili awepo duniani basi lazima binadamu wawepo hapa duniani.

Shukrani kwa kuifafanua mada hapo juu.

Lakini unaposema MUNGU ANAKUWA HAI ILI KUKAMILISHA KUSUDIO LAKE LA YEYE KUIUMBA DUNIA, Ina maana mungu hawezi kuwa hai bila binadamu?
 
Swali gumu, Tafakuri yake haina majibu yaliyojitosheleza .
bado nawaza kuhusu ai robots...like sofia..... wanaweza kuwa coded as we(humans) wakawa wanatambua battery ikiwa low wajichaji,hali fulani ikiwatokea mwilini wapumzike, Baada ya miaka kadhaa wazaliane, and so many fuckn things.
 
Mpaka sasa kunauwezakano kuwa binadamu bado hajajua kwanini yupo duniani. Yaani lengo kuu la yeye kuwepo duniani.

Mambo mengi anayofanya binadamu kwa sasa ikiwepo kufanyakazi,biashara,kula na mengine mengi ni mambo ambayo yanamuwezesha binadamu kumudu kuwepo duniani ili akamilishe lengo lake la kuwepo duniani. Cha ajabu lengo hilo alijulikani.

Mfano.
Lengo kuu la kutengenezwa simu ni kurahisisha mawasiliano kama kupiga,kutuma sms au kwa njia ya internet. Hayo mambo ya simu kuwa na saa,gem,mziki,video,kikokotoo n.k ni mbwembwe tu.

Sasa ili ufikie lengo hili katika simu ni lazima simu iwe na vocha(bando) na chaji. Vitu kama chaji na vocha katika simu tunaweza kuvifananisha na chakula,biashara na kazi kwa binadamu kwani vitu hivi vinamsaidia tu binadamu aweze kufikia lengo la kuwepo duniani na vitu hivyo haviwezi kuwa ndiyo lengo la binadamu kuwepo duniani.

Maoni yangu.
Lengo la binadamu kuwepo duniani ni kuhakikisha MUNGU ANAKUWA HAI ILI KUKAMILISHA KUSUDIO LAKE LA YEYE KUIUMBA DUNIA.

Inavyooneka binadamu na Mungu ni vitu viwili vinavyotegemeana sana. Yaani binadamu asingekuwepo duniani kama kungekuwa hakuna Mungu na Mungu ili awepo duniani basi lazima binadamu wawepo hapa duniani.
Ndio vitu hivyo sio kwamba ndio lengo lkn je,vinaweza kutuonyesha lengo kuu..?

Katika aya yako ya maoni nachokiona ni pasi ambayo bado haijaleta jibu!.. Kama nae Mungu ni hai na anategemeana na binadamu Sasa nini lengo la uhai wake ambao hata sisi huo uhai bado tunautafutia majibu...? Kwanini tutegemeane nae..?
 
Safari yako ya mars iliishia wapi mkuu?
Ha ha! Mkuu tunasubiri muda tu nafikiri ndani ya miaka hii kumi binadamu anaweza ikanyaga sayari hiyo,tunamtazamia zaidi Elon musk kwa maana naona project yake ndo ipo karibu zaidi kuliko ya NASA maana by 2024 anaweza fanya hivyo lakini NASA mwaka huo ndo wanatazamia kuweka koloni mwezini kisha ndo wafanye safari ya kwenda mars so sio leo haya mambo ni shughuli pevu nikipata wasaa nitaandika hatari zinazoweza patikana kwa kumsafirisha binadamu anga za mbali.. isn't easy sir.

Kuhusu Mimi ha ha mkuu mi siendi mars tutabanana hapahapa bongo land Sina huo mtonyo wa kufanya hivyo kama ya bando tu mtihani..🤣🤣🤣
Wengine tutaenda kifikra..😅
 
Ha ha! Mkuu tunasubiri muda tu nafikiri ndani ya miaka hii kumi binadamu anaweza ikanyaga sayari hiyo,tunamtazamia zaidi Elon musk kwa maana naona project yake ndo ipo karibu zaidi kuliko ya NASA maana by 2024 anaweza fanya hivyo lakini NASA mwaka huo ndo wanatazamia kuweka koloni mwezini kisha ndo wafanye safari ya kwenda mars so sio leo haya mambo ni shughuli pevu nikipata wasaa nitaandika hatari zinazoweza patikana kwa kumsafirisha binadamu anga za mbali.. isn't easy sir.

Kuhusu Mimi ha ha mkuu mi siendi mars tutabanana hapahapa bongo land Sina huo mtonyo wa kufanya hivyo kama ya bando tu mtihani..🤣🤣🤣
Wengine tutaenda kifikra..😅
Kuna uzi wako niliufumua kitambo!
Ndio nikakumbuka

Elon musk na space x yake lazima atoboe kwenye vumbi jekundu
 
Mpaka sasa kunauwezakano kuwa binadamu bado hajajua kwanini yupo duniani. Yaani lengo kuu la yeye kuwepo duniani.

Mambo mengi anayofanya binadamu kwa sasa ikiwepo kufanyakazi,biashara,kula na mengine mengi ni mambo ambayo yanamuwezesha binadamu kumudu kuwepo duniani ili akamilishe lengo lake la kuwepo duniani. Cha ajabu lengo hilo alijulikani.

Mfano.
Lengo kuu la kutengenezwa simu ni kurahisisha mawasiliano kama kupiga,kutuma sms au kwa njia ya internet. Hayo mambo ya simu kuwa na saa,gem,mziki,video,kikokotoo n.k ni mbwembwe tu.

Sasa ili ufikie lengo hili katika simu ni lazima simu iwe na vocha(bando) na chaji. Vitu kama chaji na vocha katika simu tunaweza kuvifananisha na chakula,biashara na kazi kwa binadamu kwani vitu hivi vinamsaidia tu binadamu aweze kufikia lengo la kuwepo duniani na vitu hivyo haviwezi kuwa ndiyo lengo la binadamu kuwepo duniani.

Maoni yangu.
Lengo la binadamu kuwepo duniani ni kuhakikisha MUNGU ANAKUWA HAI ILI KUKAMILISHA KUSUDIO LAKE LA YEYE KUIUMBA DUNIA.

Inavyooneka binadamu na Mungu ni vitu viwili vinavyotegemeana sana. Yaani binadamu asingekuwepo duniani kama kungekuwa hakuna Mungu na Mungu ili awepo duniani basi lazima binadamu wawepo hapa duniani.
Specifically kabisa wewe, ukiulizwa kusudi la kuwa hai mpaka sasa unadhani ni Lipi au Yapi?
Majibu ya swali hiyo unayapata Kwenye Biblia tu. Yapo kabisa.
 
Majibu ya swali hiyo unayapata Kwenye Biblia tu. Yapo kabisa.
Kwenye Bible hakuna jibu
linaloeleweka mkuu...majibu ya humo yanaongeza maswali.
Ingekua kuna majibu hakuna mtu angekua anahangaika kwa sasa.
 
Kwenye Bible hakuna jibu
linaloeleweka mkuu...majibu ya humo yanaongeza maswali.
Ingekua kuna majibu hakuna mtu angekua anahangaika kwa sasa.
Wanao soma biblia wanajua, ukiona mtu hajui jua sio msomaji wa biblia mzuri
 
Wanao soma biblia wanajua, ukiona mtu hajui jua sio msomaji wa biblia mzuri
Bible ni kitabu cha kawaida...lakini ninachoshangaa ni baadhi ya watu kujifanya wanaelewa zaidi lugha ya humo kuliko wengine kitu ambacho sikubaliani nacho...
Bible haina majibu yaliyo kamilika ya kwanini tunaishi au kwanini kuna life after death....majibu yaliyopo humo yanaongeza maswali badala ya ku clear doughts.
 
Back
Top Bottom