Vicent amlipua Tendwa, Mkapa aomba suluhu

Aliyeanza kuongea mambo ya kitoto ni yeye Mkapa na imetusikitisha wengi kauli kama ile. Haki ya yeye kupanda jukwaa la kumnadi mwana CCM anayo hata kama ni Rais mstaafu but kauli zake hazikuwa na mshiko. Bahati mbaya viongozi wengi waliopo wamechafuka hakuna anayeweza kupanda jukwaani akasikilizwa hata kwa wana CCM wenyewe waliogawanyika. Mkapa kwa record ya utendaji anakubalika sasa wenzie wanaweza mtuma tuma ili naye pia achafuke. Hii nasema hivi kwa kuwa hata Mwigulu kwa umri wake asikabidhiwa majukumu makubwa yale lakini naye hajachafuka ukiacha udhaifu mdogo ambao vijana wengi wanao hasa wanapopata mafanikio kiuongozi kama yeye. Hata kina Zito, Mnyika wana viudhaifu vya ujana. Hapa Mkapa kama mtu aliosoma arts alipaswa kuchuja ya kuzungumza bado angaisaidia CCM. Mkapa huwa ana maneno ya namna hiyo hata 2010 pale jangwani kufunga mkutano wa kampeni wa CCM alitukana na mi nilikuwa nawambia watu tulookaa nao kadri alivokuwa anaongea jazba ilikuwa inampanda nikawanong'oneza kuwa sasa hivi anatukana namalizia tu akashusha kitu. Hivo lazima ajidhibiti sana kwenye maneno na washauri wake pia wamsaidie.

Kuhusu udhaifu wa hayo mengine ya kifo cha mwalimu ukweli hizo speculation zilishakuwepo muda mrefu na wengine wanatuhumu hata kipindi akiwa sayansi ya teknolojia wakati katibu mkuu akiwa Ngororo alikuwa hatoi kibali cha scholarship kwenda nje hadi utoe kitu kidogo. Naamini wapo walioathirika na hili na wanaweza kuliweka pia hapa kuthibitisha. Nadhani haya mbeleni ndo yalileta kiwira, anben nk. Tusiseme vcent ataumbuka na eti mtoto wa baba mdogo au mkubwa hawezi mzungumzia baba mkubwa, kwa ambao hawajafika Butiama ni kuwa wale wameisha pamoja ukoo mzima wamejenga nyumba hapo hapo pamoja kama familia. Haya maisha ndo yalikuwepo zamani baba alikuwa na wake wengi na wanaishi hapo hapo wote kwa hiyo kina Kiboko, kina Julius wote watoto wa mmoja na walikuwa wanaishi hapo hapo na hata nyumba ya mwalimu ipo hapo tofauti ni kuwa nyumba ya mwl ina fence nyinge zipo kwa nje lkn compound moja, nadhani angalau litaeleweka but waswahili wanasema akuanzaye mmalize.
Mkuu KK, nafikiri umemwelewesha vizuri kama alikuwa hajui ukaribu wa baba mkubwa na mdogo, unajua watu waliozaliwa kwenye flat za Upanga hawawezi kujua boma ni kitu gani, hawajui kuwa Wazanaki, Wasukuma, Wamasai, Wakurya na makabila mengi zamani walikuwa wanaishi pamoja wanajenga nyumba kwenye boma moja karibu familia nzima. Watoto wa flat wao wanajua familia ni Baba,mama na watoto tuwengine wote ni ma uncle na ma aunt awe dada yako au binamu wote ni ma aunt. Sijui kweli makabila ya kusini labda wana tabia hizo za kizungu hawana cha mjomba wala shangazi.
 
Hivi Benki kuu wamesema mfumuko wa bei ni asilimia ngapi hebu Kamuulize Jakaya Mrisho Kikwete anafanya nini pale magogoni kuuza kila kitu bado kuuza hewa ya Tanzania tuu ,hazina chapa haina kitu

wanajisifu imeshuka mpaka 19.4 kutoka 19.7
 
Kwa hiyo Vincent anaona ni kuzaliwa kwenye ukoo wa Nyerere ni kitu cha maana sana! Maana sioni kama anatoa hoja yeyote ya maana. Ingawaje watu wanachekelea domo lake linavyosema ovyo kumchafua Mkapa kwa hoja za kitoto, ajue anamchafua zaidi huyo Nyerere ambaye anamwita baba yake. Iko siku atajutia maneno yake na sidhani kuwa mtoto wa baba mdogo ana haki ya kumuongelea baba mkubwa kuliko wanaye wa damu.

Ndugu yangu kwenye hili hamna lolote zaidi ya siasa. Hata wewe ukipata nafasi ya kumuua nyoka unaanza kumponda kichwa siyo mkia! Anachofanya Vicent baada ya kupata chance ni kumponda kichwa huyu nyoka BWM! Asipofanya hivyo atapondwa yeye!
 
Hot issue JF kwa sasa ni ufisadi ndani ya CDM, haya mengine hayana mashiko kwa sasa
Kwa kuwasaidia tu strategy moja iki feli jaribu nyingine si busara kulazimisha aina moja, hii ya tuhuma mnalazimisha imefikia stage ya kuita watu kwenda kuchangia duh! hadi mnatia huruma. Mnahangaika na screen wakati wenzenu wako kwa wananchi for your information leo Dr. Slaa yuko Mwanza-SAUT anaongea na wanachama na huku AM jimbo ndilo hilo limeshaondoka, poleni sana.
 
kwa hiyo vincent anaona ni kuzaliwa kwenye ukoo wa nyerere ni kitu cha maana sana! Maana sioni kama anatoa hoja yeyote ya maana. Ingawaje watu wanachekelea domo lake linavyosema ovyo kumchafua mkapa kwa hoja za kitoto, ajue anamchafua zaidi huyo nyerere ambaye anamwita baba yake. Iko siku atajutia maneno yake na sidhani kuwa mtoto wa baba mdogo ana haki ya kumuongelea baba mkubwa kuliko wanaye wa damu.

ulitaka azaliwe kwenye ukoo wa nani?
Muulize bwm anayekataa hakuzaliwa ktk ukoo huo.
 
“Mimi huyu ni baba yangu na kila siku lazima nimtaje na sisi wakatoliki tuna sala maalum ya kumwombea Nyerere na leo (jana) pia nimesali mara baada ya kuamka, sasa yeye ni nani anayenizuia kutaja jina lababa yangu, kama anataka ajiunge na ukoo wetu aombe kwa barua, kama alivyofanya mwenzake Mkapa, aliandika barua akaingizwa katika ukoo,”alisema Nyerere.
Kati ya Julius Kambarage Nyerere, Joseph Kizurira Nyerere na Josephat Kiboko Nyerere, nani baba yake Vincent Nyerere. Au wote kwa mpigo:thinking:
 
Kama hilo ulikuwa utani, vipi kuhusu ahadi ya kumshauri raisi kuhusu kuwapatia wana ar ardhi,mwisho wa uchaguzi tusishangae kuskia kuwa ulikuwa utani pia.
 
Kwa hiyo Vincent anaona ni kuzaliwa kwenye ukoo wa Nyerere ni kitu cha maana sana! Maana sioni kama anatoa hoja yeyote ya maana. Ingawaje watu wanachekelea domo lake linavyosema ovyo kumchafua Mkapa kwa hoja za kitoto, ajue anamchafua zaidi huyo Nyerere ambaye anamwita baba yake. Iko siku atajutia maneno yake na sidhani kuwa mtoto wa baba mdogo ana haki ya kumuongelea baba mkubwa kuliko wanaye wa damu.

Ajutie kivipi au ndo mnataka kumuua na yeye. Fanyeni tu ila ipo siku dunia itapasuka. Hakuna tendo baya lisilojulikana. Viongozi wa babae kama akina Osama, Sadam leo wako wapi? Kaka Vicent pamoja daima ukweli unaumiza sana. BWK ndo katufikisha hapa, katupiga mabomu sana hajali hatimaye miaka yake kumi ikaisha.
Mungu mbariki Vicent, Mungu mlaze mahari pema JKN na Mungu ibaliki Tanzania na raisi wetu mpole asiyekuwa namaamzi mazito
 
Aisee, usilolijua ni kima usiku wa Kiza. Kumbe BWM aliandika barua kuomba kuwa mwanafamilia ya Nyerere? Maswali magumu ya kujiuliza ni haya yafuatayo:

1. Ni nani muasisi wa wazo hilo?
2. Je, alifanya hivyo kwa hiari au aliambiwa aandike maombi?
3. Je motive ya kuomba kuwa mwanafamilia ni nini?
4. Na kwa wanaofahamu what are the criteria and conditions?
5. Je unaweza kulifanya hivyo katika familia yoyote?

There are so many questions than answers.
 
Kati ya Julius Kambarage Nyerere, Joseph Kizurira Nyerere na Josephat Kiboko Nyerere, nani baba yake Vincent Nyerere. Au wote kwa mpigo:thinking:[/FONT][/COLOR]

Katika Afrika wote ni Baba zake. Ila kama unamaanisha biological father (kisayansi), ni Josephat Kiboko Nyerere.
 
Mkapu hatakiwi kurumbana na my Bro vicent, kwanza huo ni ujasili wa kifisadi. sasa hoja hiyo ataizima vipi? maana wa tz wote ikiwa ni pamoja na ndugu wa marehemu wameshamjua mbaya wao. ningekuwa mimi nisingesimama kwenye jukwaa tena
 
Hot issue JF kwa sasa ni ufisadi ndani ya CDM, haya mengine hayana mashiko kwa sasa

Kama isingekuwa hot asingekimbilia kwa Butiku. Mkubali tu kuwa siasa za majitaka zimemrudi. Hili ni funzo kwa wanasiasa wote, ni muhimu kutumia siasa za kistaarabu
 
Kwa hiyo Vincent anaona ni kuzaliwa kwenye ukoo wa Nyerere ni kitu cha maana sana! Maana sioni kama anatoa hoja yeyote ya maana. Ingawaje watu wanachekelea domo lake linavyosema ovyo kumchafua Mkapa kwa hoja za kitoto, ajue anamchafua zaidi huyo Nyerere ambaye anamwita baba yake. Iko siku atajutia maneno yake na sidhani kuwa mtoto wa baba mdogo ana haki ya kumuongelea baba mkubwa kuliko wanaye wa damu.
Kweli magamba mna upofu wa fikra. Kati ya Mkapa na Vincent, wewe unadhani nani anaona kuzaliwa kwenye ukoo wa Mwalimu ni kitu cha maana sana?????Mbona Vincent alikuwa kimya tu hadi yule aliyeona kuzaliwa kwenye ukoo wa nyerere ni kitu cha maana alipoanza kukejeli watu????

Kimsingi Mkapa ndo anaona mtu kuzaliwa kwenye ukoo wa Nyerere ni big deal na ndo mana alitokwa povu. Mtu mwenye akili yake asingeweza sema kuwa, mimi sijui kama wewe ni wa ukoo wa Mwalimu, yeye aujue ukoo wa Mwalimu kama nani???Je Mkapa asipojua kuwa mtu flani ni wa ukoo wa Mwalimu, ndo inamwondolea mtu huyo haki ya kuwa wa ukoo wa Mwalimu?? Alitegemea mzaliwa wa ukoo wa mwalimu awe na mapembe????? Kweli CCM imezeeka kifikra.
 
Kwa hiyo Vincent anaona ni kuzaliwa kwenye ukoo wa Nyerere ni kitu cha maana sana! Maana sioni kama anatoa hoja yeyote ya maana. Ingawaje watu wanachekelea domo lake linavyosema ovyo kumchafua Mkapa kwa hoja za kitoto, ajue anamchafua zaidi huyo Nyerere ambaye anamwita baba yake. Iko siku atajutia maneno yake na sidhani kuwa mtoto wa baba mdogo ana haki ya kumuongelea baba mkubwa kuliko wanaye wa damu.

kwa hiyo mkapa alipatia? Acha porojo
 
Kwa hiyo Vincent anaona ni kuzaliwa kwenye ukoo wa Nyerere ni kitu cha maana sana! Maana sioni kama anatoa hoja yeyote ya maana. Ingawaje watu wanachekelea domo lake linavyosema ovyo kumchafua Mkapa kwa hoja za kitoto, ajue anamchafua zaidi huyo Nyerere ambaye anamwita baba yake. Iko siku atajutia maneno yake na sidhani kuwa mtoto wa baba mdogo ana haki ya kumuongelea baba mkubwa kuliko wanaye wa damu.

Inaelekea mkuu umedandia gari kwa mbele na hukujua mwanzo wa malumbano haya, kinachoongelewa hapa si ufahari au sifa ya kuwa katika ukoo wa Nyerere, sasa aliyemchafua mwenzie ni nani hapa? Mkapa alianza kutoa maneno machafu akapewa majibu sasa shida ipo wapi? kama mawazo yako ni hayo nakupa assignment kwa nini Mkapa atake suluhu?, na wewe inaelekea ni gamba la kobe kabisa
 
Back
Top Bottom