Vatican, nchi yenye watu 800 kwa mujibu wa sensa ya 2008

eden kimario

JF-Expert Member
Jun 13, 2015
10,227
16,179
80a44d666c159d8b3d81385f4b69fe6f.jpg
0e95af2008bdce8f67e526349c406920.jpg

Vatican ni dola mji
Hivyo ni nchi ndogo duniani kuliko zote
Ni nchi ya papa ambae ni askofu wa roma na mkuu wa kanisa katoliki duniani
Iko ndani ya jiji la roma upande wa mangaribi
Jina limetokana na mlima vatikan au mons vaticanus
Pamoja na basilika la mt. Petro ambalo ndilo kanisa kubwa kuliko yote duniani
Vatikani ina makanisa mengine 7
Vatikani pia ina makumbusho ya sanaa kubwa ya hazina kiasi kwamba inahesabiwa na UNESCO kua ni urithi wa dunia tangu mwaka 1984
Mji wa vatican ni mabaki ya dola la papa lililotawala sehemu kubwa ya italia ya kati kwa karne nyingi hadi mwaka 1870
Tangu mwaka wa 1860 baadhi ya maeneo hayo yalitawaliwa na ufalme mpya wa italia uliolenga kuunganisha sehemu zote za peninsula ya italia
Utawala wa papa juu ya mji na mkoa wa roma ulilindwa na ufaransa hadi mwaka 1870
Vita ya mwaka 1870 kati ya ujerumani na ufaransa kuliifanya ufaransa kuondoa jeshi lake roma hivyo mji huo kutekwa na jeshi la italy tarehe 20/9/1870
Wakati huo serikali ya italia ilitaka kumuachia papa pius sehemu ya mji wa roma lakini papa pius alikataa akitumaini wakatoliki wa italia na sehemu nyingine duniani watalazimisha serikali ya italy kumrudishia mji wote wa roma
Kwa hali hiyo mapapa walijifungia ndani ya jumba la vatikani kwa miaka 57 bila kutoka

Mwaka 1929 serikali ya benito musolini ilitafuta amani na papa pius aliekua tayar kwa makubaliano
Hivyo vatikani kua nchi huru kuanzia wakati huo

Mji mkuu- vatican
Wimbo wa taifa- ino e marcia pontificale
Katbu wa dola - pietro parolini
Vatican ina uhusiano za kibalozi na nchi 180 duniani kupitia ikulu ya vatikani
Vatican ina posta pia ikitoa stempu na hata sarafu za euro
Vaticani ina jeshi dogo kabisa duniani lakini lenye historia ndefu kabisa duniani
Ni kikosi cha walinzi waswisi ambacho kipo tangu mwaka 1, 506 na kina wanajeshi 100 tu
Wote ni wakatoliki raia wa uswisi kwa kuzaliwa

Je unaielewa vipi vaticani
Karibu kwa kuongezea zaidi ili wengine waelewe
 
Jamani mnaojua zaidi mwageni facts hapa. Nahisi story ya vatican ni tamu sana. Kuna kipindi Askofu Kilaini alikuwa anatoa kupitia redio Tumaini ila kwa bahati mbaya kutokana na majukumu nilikuwa nakosa vipindi vingi. Kujeni jamani!
 
Huo mji una maktaba kubwa sana ambayo ni kati ya sehemu za siri kabisa dunia hakuna mtu anayeruhusiwa kuingia kwenye hio maktaba
Sio kweli kwamba huruhusiwi. Unaruhusiwa kuingia Vatican Archives kwa kuomba kibali maalum, na mara nyingi maktaba hii hutumiwa na watafiti mbalimbali.

Ingekuwa hairuhusiwi watu kuingia.. je nani angekuwa anafanya usafi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom