SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,130
- 7,901
Ni zaidi ya mara mbili nimemsikia Haji Manara akisema kuwa Fabrice Ngoma ni mchezaji mwenye umri mkubwa sana kuliko unaotangazwa katika taarifa zake rasmi. Toka nimemsikia nilikuwa nina mashaka na hizo taarifa ila sikuzifuatilia.
Manara mara zote hizo amekuwa anasema alimshuhudia kwa macho yake Ngoma akicheza mashindano ya CECAFA Challenge Cup mwaka 2004 tena akiwa captain wa DRC, akasema kipindi hicho kwa Tanzania captain ni Juma Kaseja na Selemani Matola.
Juzi nilivyosikia anayarudia maneno haya nikasema embu ngoja leo nipoteze muda wangu nione kama huyu mpuuzi yuko sahihi. Zama hizi ni za utandawazi, hauwezi kudanganya watu halafu wakakuangalia tu.
Nikaanza kwa kuangalia Challenge Cup ya 2004, nikakuta DRC hawakushiriki. Nikasema labda alikosea mwaka nikaangalia miaka tofauti ya kipindi hicho, nikakuta miaka yote ya 2000 DRC hawakushiriki kwenye Challenge Cup.
Nikaenda mbali zaidi kwa kutumia vyanzo mbalimbali kuangalia vikosi vya DRC vya mwaka 2004, jina la Fabrice Ngoma halikuwepo katika list hizo zote.
Nahisi Manara alihusika moja kwa moja katika juhudi za kumleta Ngoma pale Yanga, halafu Simba walipomdaka juu kwa juu amebaki na kisirani na kusambaza uzushi ili kumkomoa.
Manara mara zote hizo amekuwa anasema alimshuhudia kwa macho yake Ngoma akicheza mashindano ya CECAFA Challenge Cup mwaka 2004 tena akiwa captain wa DRC, akasema kipindi hicho kwa Tanzania captain ni Juma Kaseja na Selemani Matola.
Juzi nilivyosikia anayarudia maneno haya nikasema embu ngoja leo nipoteze muda wangu nione kama huyu mpuuzi yuko sahihi. Zama hizi ni za utandawazi, hauwezi kudanganya watu halafu wakakuangalia tu.
Nikaanza kwa kuangalia Challenge Cup ya 2004, nikakuta DRC hawakushiriki. Nikasema labda alikosea mwaka nikaangalia miaka tofauti ya kipindi hicho, nikakuta miaka yote ya 2000 DRC hawakushiriki kwenye Challenge Cup.
Nikaenda mbali zaidi kwa kutumia vyanzo mbalimbali kuangalia vikosi vya DRC vya mwaka 2004, jina la Fabrice Ngoma halikuwepo katika list hizo zote.
Nahisi Manara alihusika moja kwa moja katika juhudi za kumleta Ngoma pale Yanga, halafu Simba walipomdaka juu kwa juu amebaki na kisirani na kusambaza uzushi ili kumkomoa.