Uzuri wa mwanamke sio urembo ni tabia

Uzuri wa mwanamke sio urembo ni tabia

KILAKA

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2014
Posts
374
Reaction score
127
Eid mubarak wana MMU,

Bila kupoteza wakati acha niende kwenye mada ambayo ningependa kuielezea. Kuna msemo maarufu sana kwamba UZURI WA MWANAMKE NI TABIA SIO UREMBO.

Huu usemi mimi ninakubaliana nao hasa pale linapokuja swala la kumtafuta mwenzi wako wa maisha ni lazima ujiridhishe kuwa tabia na mienendo yake, ni mizuri na imekuridhisha.

Tatizo linakuja jinsi ya kuitambua hiyo tabia ya mwenzi wako (mwanamke) unayetaka kufunga nae pingu za maisha, kwa kweli wanawake wengi kwa sasa wanavyojionyesha nje si vile walivyo ndani wanajua kufake tabia yao ionekana kama nzuri wakati sio kweli, kwa mfano mwonekano wa mavazi wa mwanamke unaweza ukazungumza tabia yake jinsi ilivyo ijapokuwa sio kwa asilimia mia.

Kuna mwanamke ambaye anaweza akawa anavaa nguo ndefu sana mpaka anaziburuza akitaka aonekane mwenye tabia nzuri lakini kumbe usiku utamkuta kwenye vigodoro au barabarani anajiuza ni kahaba.

Kwa sasa wanawake wengi ni waigizaji wazuri sana kuliko wasanii wa hollywood ijapokuwa huwa hawapati tuzo.
 
Kizazi cha sasa hivi kimevurugwa iwe wakaka au wadada. Na zamani zilikuwepo tabia ambazo ni general jamii inazitambua kama nzuri kwa binti yeyote wa kuoa. Leo vijana ndio wanachagua wanataka tabia gani. Zinaweza kuwa kuwa zinaonekana mbaya lakin wapendanao wanaelewana.
Ni changamoto sana kudefine tabia mbaya siku hizi
 
Sawa ila sio wote wanaangalia tabia mkuu...
Tabia waachie kijijini....ila mjini ni mkwanja, shape , na vitu zingine kama hizo!

Eid Mubarak!!!!!!
 
Tabia inarekebishwa bana, wacha kututisha ili tuwaogope watoto wazuri wazuri!!
 
kizazi cha sasa hv kimevurugwa iwe wakaka au wadada. Na zaman zilikuwepo tabia ambazo ni general jamii inaztambua kama nzuri kwa bint yeyote wa kuoa. Leo vijana ndo wanachagua wanataka tabia gan. Zinaweza kuwa kuwa zinaonekana mbaya lakin wapendanao wanaelewana.
Ni changamoto sana kudefine tabia mbaya siku hzi

Nakubali ni changamoto sana kudefine tabia nzuri, lakini usiniambie kuna wanaume wanavutiwa sana na wanawake makahaba ili wawaoe.
 
Sawa ila sio wote wanaangalia tabia mkuu...
Tabia waachie kijijini....ila mjini ni mkwanja, shape , na vitu zingine kama hizo!

Eid Mubarak!!!!!!

Kama itatokea mwanamme fulani ameamua kumuoa mwanamke kwa sababu ana shape au sura nzuri, itakuwaje kama mwanamke huyo katika kipindi wako kwenye maisha ya ndoa akapata ajali, hatuombei hivyo lakini au miaka ikaenda akazeeka, upendo ule wa mwanzoni wakati wanaoana utabakia???
 
Nakubali ni changamoto sana kudefine tabia nzuri, lakini usiniambie kuna wanaume wanavutiwa sana na wanawake makahaba ili wawaoe.

Nadhan unakubaliana nami kuwa kuna makahaba wanafikia kipindi wanaolewa. Hiyo inatosha kuthibitisha kuwa kuna wanaume wanavutiwa na makahaba
 
TEAMSuraNaShape kwanza........... sasa hivi wa tabia nzuri za kizamani hamna , sasa nikose tabia na uzuri pia?

hapana aseeeeh!!!!!!!

Niko makini sana katika kuchagua sura na shape zenye mvuto wa hali ya juu, lakini kama nina mpango wa kuchezea na kusepa zangu lakini sio kuoa.
 
Last edited by a moderator:
Tabia ni kama ngozi...kamwe haiwezi jificha milele.
 
nadhan unakubaliana nami kuwa kuna makahaba wanafikia kipindi wanaolewa. Hiyo inatosha kuthibitisha kuwa kuna wanaume wanavutiwa na makahaba

Hahahahaha!!!!!!! Kweli wapo makahaba ambao huwa wanaolewa lakini hao wanaume ambao wamewaoa walidanganywa(they were fooled) wanawake wengi walivaa ngozi ya kondoo wakati mbwa mwitu na ndio maana nimeandika huu uzi kujenga umakini kwa wanaume.
 
TEAMSuraNaShape kwanza........... sasa hivi wa tabia nzuri za kizamani hamna , sasa nikose tabia na uzuri pia?

hapana aseeeeh!!!!!!!

Anaweza akawa na sura nzuri shape vile vile akawa na tabia nzuri na muelewa kulingana na mazingira aliyokulia pia ukisema sura mbaya ndo akawa kishinda lami kwangu mimi awe mzuri na tabia njema hayo mengne ni extra sasa ana tabia nzuri huku hatazamiki hiyo ni sheeeedah
 
Last edited by a moderator:
Hahahahaha!!!! Dokta umenivunja mbavu zangu.

Ndiyo maana yake aseeeeeh!!!!!!!!

mimi kawaida napenda vitu vizuri zuri , sasa nikioa asiyechaguo la moyo na macho yangu nitakuja kutulia kweli.........

halafu binadamu wana tabia ya kubadilika , huyo unayemuona kondoo leo kesho anaweza kugeuka na kuwa chui khatari kabisa.......

lets enjoy life bana...........
 
Hahahahaha!!!!!!! Kweli wapo makahaba ambao huwa wanaolewa lakini hao wanaume ambao wamewaoa walidanganywa(they were fooled) wanawake wengi walivaa ngozi ya kondoo wakati mbwa mwitu na ndio maana nimeandika huu uzi kujenga umakini kwa wanaume.

Bora hao walioshindikana mana wanakuwa wamepitia mengi na wamejifunxa kwahyo akiolewa anatulia sasa wale ambao hawakula ujana wakaingia ndoani ndo huwa wasumbufu wakubwa kuna watu na wafahamu walikuwa wamekubuhu kwa tabia zao lakini wametulia na hawa hangaiki kwahyo ina change na hao watu wanaoita maka.. Ndo wanakujaga kutulia majority yao
 
Tabia ni kama ngozi...kamwe haiwezi jificha milele.

Heart, unaishi dunia gani??? wanawake wengi hapa mjini tabia wanazoonesha nje sio za ukweli kwa mfano unaweza ukakuta na mdada anayependa ufahari na luxury sana lakini kumbe ametokea katika familia masikini sana huko kijijini hata umeme alibahatika kuutumia alivyokuja mjini na kuna wengine wanavaa nguo descent sana wakati ni wachafu sana na wana uwezo wa kufanya hivyo kwa muda mrefu.
 
Ndiyo maana yake aseeeeeh!!!!!!!!

mimi kawaida napenda vitu vizuri zuri , sasa nikioa asiyechaguo la moyo na macho yangu nitakuja kutulia kweli.........

halafu binadamu wana tabia ya kubadilika , huyo unayemuona kondoo leo kesho anaweza kugeuka na kuwa chui khatari kabisa.......

lets enjoy life bana...........

Ninanukuu maneno ya lucky dube,"beautiful woman is another man's plaything" kwa hiyo angalia usije ukawa umeoa kumbe umewaolea watu.
 
Back
Top Bottom