The Assassin
JF-Expert Member
- Oct 30, 2018
- 4,355
- 17,321
Sisi watu wa kuja Dar ambao tuliletwa hasa na mambo ya shule nk kwa namna moja ama nyingine tumewahi kulizwa katika jiji letu hili pendwa.
Mimi nina matukio kadhaa ya wizi ambayo nimewahi kufanyiwa hapa Dar.
Tukio la kwanza, ilikua miaka ya 2009, enzi hizo nakaa maeneo ya riverside hapo karibu na Mabibo Hosteli, sasa siku moja wakati natokea Ubungo pale darajani karibu kabisa na landmark hotel, nikauziwa simu fake mchana kweupe jua limewaka nikapigwa 20,500.
Nimeuziwa nikaambiwa nisiifungue kwanza, kweli nikawa mjinga sikufungua ile nimefika home kufungua kumbe ni udongo kwa ndani, nilijiona mjinga wa nambari moja.
Tukio la 2, miaka hiyo hiyo ya 2009 nilipanda daladala kutoka Mnazi mmoja kuja ubungo, sa 2 usiku na kisimu changu cha nokia 1100 ama nokia ya tochi, nimepanda daladala nimeshikilia mfuko lakini nikashangaa kufika Buguruni sina simu.
Tukio la 3, baada ya kumaliza masomo hapa Dar nikapata kazi mkoani, nikakaa muda baadae nikapata kazi tena kampuni nyingine hapa Dar ikanibidi kurudi Dar.
Nilipofika nikatafta madalali wa nyumba, nikapata mtandao wa kupatana, nikapata madalali wakanionyesha hadi nyumba maeneo ya Mbezi Kwa Zena/Mbezi ya chini.
Kisha nikapelekwa kwa mwenye nyumba upanga, nikalipia kisha niliporudi kwenye nyumba ili kufanya usafi nikakuta watu tofauti, hapo nikajua nimepiwa.
Nikapeleka kesi Kawe, ikawa kila siku ni danadana, nikaamua kutulia na kufanya mambo mengine. Wale jamaa wakaendelea kua wanafanya utapeli wao mtandaoni kama kawaida, mimi nikawaacha wakajisahau kwa miezi 3, kisha nikawatafta kwa kutumia vijana wangu hapa Dar, nikakamata mmoja. Tulichomfanya baadae niliamua kumsamehe kabisa. Sijui kama yuko hai ama alikufa. Wenzake walikimbia mji.
Tukio la 4, mwaka 2019, bodaboda alinyakua simu yangu kali kabisa Note 9 ndio zimetoka tu nikanunua jamaa akanyakua. Akaendelea kua nayo hewani siku 2 nzima. Nikatafta vijana wangu tukamsakua na kumkamata huko porini Mbagala, hatanisahau.
Tukio la 5, kipindi naishi Tabata kwa Ashura, wezi wameingia ndani nikiwemo nimelala wakaiba tv nchi 65 wakanywa juice kwenye friji, hiyo sikuhangaika kuitafta ikanibidi nihame tu mtaa.
Sasa nikikamata kijana ameniibia simpeleki polisi tena, nampiga miti kisha namuachia
Mimi nina matukio kadhaa ya wizi ambayo nimewahi kufanyiwa hapa Dar.
Tukio la kwanza, ilikua miaka ya 2009, enzi hizo nakaa maeneo ya riverside hapo karibu na Mabibo Hosteli, sasa siku moja wakati natokea Ubungo pale darajani karibu kabisa na landmark hotel, nikauziwa simu fake mchana kweupe jua limewaka nikapigwa 20,500.
Nimeuziwa nikaambiwa nisiifungue kwanza, kweli nikawa mjinga sikufungua ile nimefika home kufungua kumbe ni udongo kwa ndani, nilijiona mjinga wa nambari moja.
Tukio la 2, miaka hiyo hiyo ya 2009 nilipanda daladala kutoka Mnazi mmoja kuja ubungo, sa 2 usiku na kisimu changu cha nokia 1100 ama nokia ya tochi, nimepanda daladala nimeshikilia mfuko lakini nikashangaa kufika Buguruni sina simu.
Tukio la 3, baada ya kumaliza masomo hapa Dar nikapata kazi mkoani, nikakaa muda baadae nikapata kazi tena kampuni nyingine hapa Dar ikanibidi kurudi Dar.
Nilipofika nikatafta madalali wa nyumba, nikapata mtandao wa kupatana, nikapata madalali wakanionyesha hadi nyumba maeneo ya Mbezi Kwa Zena/Mbezi ya chini.
Kisha nikapelekwa kwa mwenye nyumba upanga, nikalipia kisha niliporudi kwenye nyumba ili kufanya usafi nikakuta watu tofauti, hapo nikajua nimepiwa.
Nikapeleka kesi Kawe, ikawa kila siku ni danadana, nikaamua kutulia na kufanya mambo mengine. Wale jamaa wakaendelea kua wanafanya utapeli wao mtandaoni kama kawaida, mimi nikawaacha wakajisahau kwa miezi 3, kisha nikawatafta kwa kutumia vijana wangu hapa Dar, nikakamata mmoja. Tulichomfanya baadae niliamua kumsamehe kabisa. Sijui kama yuko hai ama alikufa. Wenzake walikimbia mji.
Tukio la 4, mwaka 2019, bodaboda alinyakua simu yangu kali kabisa Note 9 ndio zimetoka tu nikanunua jamaa akanyakua. Akaendelea kua nayo hewani siku 2 nzima. Nikatafta vijana wangu tukamsakua na kumkamata huko porini Mbagala, hatanisahau.
Tukio la 5, kipindi naishi Tabata kwa Ashura, wezi wameingia ndani nikiwemo nimelala wakaiba tv nchi 65 wakanywa juice kwenye friji, hiyo sikuhangaika kuitafta ikanibidi nihame tu mtaa.
Sasa nikikamata kijana ameniibia simpeleki polisi tena, nampiga miti kisha namuachia