Uzito wa Zitto, Wepesi wa Hoja kwa Suala zito

Mchambuzi,Tutamjadili Zitto Kabwe kugombea urais wa Tanzania atakapofikisha umri ambao kikatiba unamruhusu, kwa sasa katiba haimruhusu Zitto Kabwe kugombea urais kwa vile yuko chini ya umri wa miaka 40. Hata 2015 kama kifungu cha katiba kuhusu umri wa kugombea urais Tanzania usipofanyiwa marekebisho bado hatakuwa na nafasi hiyo.

Bora Zitto na wanamwunga mkono wangehangaikia Katiba mpya kufanyiwa marekebisha badala ya kuhangaikia kitu ambacho kikatiba ni ukiukwaji.

Hiyo ni hoja nzito ambayo inagusa Katiba ya nchi kuhusu umri wa mgombea Urais

Jingine zaidi ya hapo zitto amekosa adabu mbele chama kwa kujitangazia uamuzi mkubwa bila kuhusisha chama labda kama anamaanisha kuwa rais hata kama sio kupitia cdm, kitu ambacho wengi tunaamini ndio chanzo cha'jeuri yake.

Inakuwaje afanye unilateral declaration wakati chama kipo na viongozi wenzake wapo? Tayari ameshaonyesha udhaifu mkubwa sana kuweza kuwa kiongozi wa nchi, hana ushirikiano na viongozi wenzake, atatawwala vipi bila wenziwe ambaye hakujali hata kutumia vikao vya ndani kujadili kama ni muda mwafaka kutoa tamko na pengine kwa staili gani kwa manufaa ya ushindi wa chama na taifa.

Wenye critical thinking wanahitimisha kuwa Zitto kalewa sifa zifuatazo: mosi, utetezi wake wa raslimali bungeni ambazo kawida sio'effort zake kama yeye bali ni chama, pili; kuchukulia advantage ya propanganda za kuwa cdm ni chama cha wakristo na ukanda kwa hiyo yeye kama muislamu ana support ya waislamu wote, tatu yeye as under 40 vijana wooootte na hasa wanamziki wa kibongo ni maswahiba ambao watamuunga mkono, mwisho ni uswahiba kwenye watawala. Hizi ni ndizo pillar za zzk kuvimba kichwa hadi kudharau chama. Je tuzipime ni misingi hii ambayo ndio mtaji wake wa kuupta urais ni wa maslahi kwa taifa na hasa wanyonge? Au ushabiki wa kuharibu na kugawanya tu kura kwa faida ya wengine. Cdm ingependa kupata rais wa wananchi sio wa mtandao fulani ndio maana ya harakati za m4c kwanza!!

Nashauri ZZK aache mambo hayo atangaze kufuta nia na awaambie wafuasi aliyojitengenezea warudi kujenga chama. Yeye atapata uwaziri kama kijana atatumia miaka kadhaa kujenga uzoefu wa uongozi na hatimae miaka ijayo inshallah mwenyeezi mungu atamshushia ndoto yake hyio. Demokrasia isiwe ticketi ya kuifanya taasisi ya Urais ikawa kama cm ya mchina kila mtu anauwezo wa kuinunua!
 
Zito ameonekana ni mtu asiye na msimamo na kuna kila dalili kwamba kuna msukumo kutoka nje unaotaka agombee,hasa kutoka CCM.Na pia ameonekana kuwa hatoi ushirikiano mzuri kwa wenzake kujenga chama,badala yake anawakoroga kwa matamshi yake.Hata,wananchi wengi hawamwamini,hata akipewa hiyo nafasi inabidi achunguzwe sana.Pia kuna taratibu za kutangaza nia ya kugombea,sio lazima ziandikwe,unatumia busara.
 
Pia kuna taratibu za kutangaza nia ya kugombea,sio lazima ziandikwe,unatumia busara.

Chini ya mfumo wa demokrasia ya uliberali, suala la mwanachama kugombea ni suala binafsi, sio suala la chama kama ilivyokuwa enzi za TANU na baadae CCM kabla ya ujio wa mageuzi ya kisiasa; Kwahiyo Chadema wana changamoto kubwa katika zama hizi;

Pia kuhusu suala la utaratibu wa kutangaza nia, chini ya mfumo wa demokrasia ya uliberali, utayari wa mwanachama au mgombea hutokana na masuala makuu mawili:


  • Name Recognition na
  • Uwezo wa Pesa ili kujipanga kama mgombea;

Suala la Timing halina nafasi kubwa kama halina uhusiano na masuala hay mawili, hasa iwapo mgombea au wagombea husika wanatoka Chama cha Upinzani kinachojipanga kukiangusha kwenye uchaguzi unaofuatia, Chama kilichopo madarakani;
 
Mchambuzi, umetumwa na nani? Wewe ni gamba zee, linaloishia kiunoni likivuliwa. Wewe ndiye wa kututungia hadidu rejea wanachadema juu ya rais atakaye gombea? ZITTO ni msaliti, Hatufai TENA.
 
EMT, Mchambuzi na wengine hakuna ubishi wa mgombea kutangazwa mapema, kujitangaza mapema au chama kuanza mchakato mapema. Haya maswala ya chama au nafsi kutangaza kuutaka uraisi na kuanza primaries ndani ya vyama vya siasa liko ndani ya uwezo wa vyama vya siasa wanaweza kuanza primaries zao hata miaka mitano na kumwandaa mgombea. Ila hata huko magharibi kampeni za kitaifa hazizidi miezi miine kama sikosei sema primaries ndizo zinachukuwa muda mwingi.

Ndio maana hakuna anayemlaumu yeyote aliyetangaza nia mapema na akaamua kuweka CV yake hadharani ili watu waingalie na kuichambua. Nitarudia tena Tatizo la ZZK sio muda wa kutangaza ila ni mambo halisi yalivyo ndani kwa mwanachadema mkweli mwenye nia ya dhati kukipeleka chama ikulu anaona timming ya dogo sio kuingiza chama ikulu ila kuvuruga jitahada zinazofanywa na makamanda ili mgombea atakayepatikana asiende ikulu. Hivi kweli kila mmoja mwenye nia ya kwenda Ikulu akaacha kujenga chama akaanza kujiandaa yeye na kikundi chake kushinda primaries sasa hivi CDM itashinda?? Hao wanachama wa kuwachagua wako wapi. Ndio maana nasema Tanzania bado vyama vingi ukiacha CCM ni vichanga sana. Huyo mgombea unayetaka kumuuza leo ukienda Tanga inabidi uanze kuuza chama kwanza halafu ndio mwanze eehee sasa tunataka mumchague mgombea uraisi. Come on tuliangalie hili swala kwa undani ila kama mjadala hauhiusu chadema well and good CCM wanatakiwa kuanza primaries hata 2013 kwani wao kama chama wamejijenga Tayari. 2020 chadema wakati huu watakuwa wanaongelea nani atagombea na halitaonekana tatizo kwani hapo mpaka kwekizu tutakuwa na wanachama. Kama mgombea ameshindwa kuifanya kigoma Chadema kweli ataiweza tanzania???

Kwa CDM naona kama tunakuwa tunasahau Historia haraka sana, 2010 CDM kilikuwa bado hakijawa sio tu na uwezo mzuri wa kimtandao hata fedha za kuweza kufanya mikutano nchi nzima ilikuwa ni tabu. Mgombea wa uraisi wa CDM 2005 na 2010 ni watu waliojitolea kujenga chama na matunda yake ndio haya. Ni ukweli usiopingika 2010 kungekuwa na primaries za Uraisi CDM 2010 labda ungekosa hao wa kuweka majina hata hawa ambao leo wanasema wanataka usingewaona hata kama katiba zingeruhusu.

Ni vyema kuwatembeza wagombea mapema ndani ya chama ili wanachama wote waamue ni nani anafaa, na hii inaweza kufanywa muda wa kutosha. Anyway CDM kwa sasa itaanza mchakato wa kupata wagombea wake wote kuanzia mwaka 2014 hii ni kuwezesha wananchi wengi kuwajua wagombea wao. Swala la urasi ni vyema tukaanza mapema. Ila je utaratibu kubadilka isiwe ni fujo. Kama mlikubaliana na utaratibu wa kwanza kwa busara na sasa unaonekana haufai au umepitwa na wakati ni vyema haya mambo yakawekwa kwenye katiba za vyama kuliko viongozi kuanza kutunishiana misuli kwa mambo yanayozungumzika.

Faida za kumpata mgombea mapema ni nyingi sana, ila tukumbuke bila kujenga chama imara chenye sera imara maadili na nia ya dhati ya kuiendeleza Tanzania na watu wake hata mgombea akijulikana 1995 hawezi kushinda. Wako wengi wanajulikana mapema na wenye sifa nyingi sana ila vyama vyao vimeoza kisera na kiitika na hawezi sio tu kushinda hata kupitishwa kwenye mchujo wa awali.
 
Mchambuzi, umetumwa na nani? Wewe ni gamba zee, linaloishia kiunoni likivuliwa. Wewe ndiye wa kututungia hadidu rejea wanachadema juu ya rais atakaye gombea? ZITTO ni msaliti, Hatufai TENA.

Nimetumwa na uzalendo kwa nchi yangu; Vinginevyo:

Basi jengeni hoja hiyo kwa mujibu wa Kanuni na Katiba ya Chadema ili muondokane nae, kwani akipita kwenye mchakato wa Chadema, na pia apite kwenye uchaguzi mkuu, Zitto atakuwa sio Rais wa Chadema bali wa Watanzania, mimi nikiwemo; Ndio maana I believe kwamba kama raia wa Tanzania, I do have a stake in this i.e. Suala La Zitto Candidacy, na uzito wake;

Kumbuka kwamba Uanachama wangu wa CCM haunizuii kupigia kura mgombea wa chama kingine chochote nitakayeona anafaa zaidi, kwani katika demokrasia ya uliberali, utambulisho wangu wa kwanza ni MPIGA KURA Raia wa Tanzania, na Suala la Uanachama wa Chama cha Siasa (CCM), likifuatia baada ya suala hili la msingi, lakini hii pia ni kutokana na Katiba ya JMT (1977) kutoruhusu interest za siasa independently, na badala yake, by affiliation na Chama Cha Siasa, affiliation ambayo for me, haina maana kwamba ni kwa CCM hadi umauti unifike; Naweza nikawa mwanachama wa Chadema, CCK, CUF, TLP, NCCR, kesho, who knows, kwani nina haki ya kikatiba kufanya hivyo;
 
Kama mlikubaliana na utaratibu wa kwanza kwa busara na sasa unaonekana haufai au umepitwa na wakati ni vyema haya mambo yakawekwa kwenye katiba za vyama kuliko viongozi kuanza kutunishiana misuli kwa mambo yanayozungumzika.

Hoja hii ina husiana na swali langu langu la kwanza kwa kambi inayompinga Zitto, ambapo kwenye bandiko namba moja nililiuza, JE:

  • Pingamizi hii inatokana na Zitto kukiuka Kanuni Yoyote Ya Chadema KIKATIBA

Nia ya swali langu hili ilikuwa ni kujaribu kuleta mjadala wenye uzito wa hoja kutoka linalopinga uamuzi wa Zitto, na kwa bahati nzuri, tunazidi kuona hoja zenye uzito kutoka kundi hili, hasa zinazolenga suala la umri wa kugombea Urais, kwa mujibu wa katiba ya JMT (1977); Lakini nikauliza pia, je kwanini vikao husika havimuiti zitto na kumweleza haya kwa ustaraabu, hasa awe mvumilivu na asubiri maoni ya Katiba mpya juu ya hili, na badala yake, pingamizi dhidi yake, hata kutoka kwa viongozi wa chama chake zinatokea barabarani na vibarazani? Je huku ni kujenga chama au kukibomoa?

Iwapo kuna hisia kwamba kitendo cha Zitto kinabomoa, nadhani utaratibu niliopendekeza hapa kuhusu namna ya kushughulikia suala hili, ungepokelewa vizuri sana na UMMA wa watanzania, kuliko hali ya sasa ya mwasisi kusema hivi, mjumbe wa kamati kuu kusema vile, kitu ambacho kinazidi kuwa an ASSET TO ZITTO (kwani hapingwi kikanuni bali kifitina zaidi na kihisia) and a LIABILITY TO CHADEMA, mbele ya UMMA; Ni muhimu Chadema kama chama kikaja na hoja nzito ya kudhibiti suala hili, kikatiba before its too late;

Faida za kumpata mgombea mapema ni nyingi sana, ila tukumbuke bila kujenga chama imara chenye sera imara maadili na nia ya dhati ya kuiendeleza Tanzania na watu wake hata mgombea akijulikana 1995 hawezi kushinda. Wako wengi wanajulikana mapema na wenye sifa nyingi sana ila vyama vyao vimeoza kisera na kiitikadi na hawezi sio tu kushinda hata kupitishwa kwenye mchujo wa awali.

Kwa maana hii, pengine ni muhimu kwa wanachama na pia viongozi wenye nia ya kugombea, hasa katika mazingira haya ya demokrasia ya uliberali, wakafanya maamuzi binafsi kama Zitto ili kuepuka vikwazo hivi, kwani suala la mgombea chini ya mfumo wa demokrasia ya uliberali, ni suala la mtu binafsi, sio suala la Chama, kama ilivyokuwa kwa TANU na baadae CCM kabla ya kuingia kwa mfumo wa vyama vingi; Ndio maana hata sasahivi ndani ya CCM kuna mgongano mkubwa sana kuhusu baadhi ya wanachama kutia nia yao mapema, na bila kupitia taratibu za chama, wakati ukweli uliopo ni kwamba CCM ni chama kinachoendeshwa kwa mfumo wa enzi za chama kimoja ambapo maamuzi kama haya yalifanywa kichama, wakati chama hiki kinaendesha siasa zake za ushindani katika mazingira ya demokrasia ya uliberali, ambapo suala la mgombea ni suala binafsi, sio la chama;
 
Nimetumwa na uzalendo kwa nchi yangu; Vinginevyo:

Basi jengeni hoja hiyo kwa mujibu wa Kanuni na Katiba ya Chadema ili muondokane nae, kwani akipita kwenye mchakato wa Chadema, na pia apite kwenye uchaguzi mkuu, Zitto atakuwa sio Rais wa Chadema bali wa Watanzania, mimi nikiwemo; Ndio maana I believe kwamba kama raia wa Tanzania, I do have a stake in this i.e. Suala La Zitto Candidacy, na uzito wake;

Kumbuka kwamba Uanachama wangu wa CCM haunizuii kupigia kura mgombea wa chama kingine chochote nitakayeona anafaa zaidi, kwani katika demokrasia ya uliberali, utambulisho wangu wa kwanza ni MPIGA KURA Raia wa Tanzania, na Suala la Uanachama wa Chama cha Siasa (CCM), likifuatia baada ya suala hili la msingi, lakini hii pia ni kutokana na Katiba ya JMT (1977) kutoruhusu interest za siasa independently, na badala yake, by affiliation na Chama Cha Siasa, affiliation ambayo for me, haina maana kwamba ni kwa CCM hadi umauti unifike; Naweza nikawa mwanachama wa Chadema, CCK, CUF, TLP, NCCR, kesho, who knows, kwani nina haki ya kikatiba kufanya hivyo;

Kwa hiyo umesharidhika hakuna kiongozi wa kukuridhisha kwenye chama chako hadi uhangaike na wa Zitto wa cdm??

Ingefaa uje kujiunga na cdm kwa kupendezwa na sera zao sio kwa ajili ya zitto. Wapo wengi kuzidi zitto hawajatangaza tu kwa vile wako bize na kuuza sera na kutoa elimu ya uraia wanachama wawe wengi.
 
Kwa hiyo umesharidhika hakuna kiongozi wa kukuridhisha kwenye chama chako hadi uhangaike na wa Zitto wa cdm??

Iwapo ulisoma bandiko langu namba moja la uzi huu hadi mwisho, nilimalizia kwa kusema haya:

Mbali ya Zitto, hata huko mbeleni tujitahidi kupima wagombea wengine wote kutoka vyama vyote kwa mwendo huu, kwani kwa kufanya hivyo, tutahamia katika ushindani wa siasa wenye tija kwa wananchi kwa maana ya kwamba - SIASA ZA MASUALA - ZINAZOLINGANISHA MASUALA NA WATU (WAGOMBEA) badala ya SIASA ZA WATU (WAGOMBEA) - ZINAZOLINGANISHA WATU NA WATU (WAGOMBEA), kama ilivyo sasa;
 
Inashangaza kuona vyama vingi vya siasa including Chadema, wameiga mfumo wa CCM hata kioganaizesheni; Je hii ina maana kwamba, tukiachana na udhaifu mwingine wa CCM kama vile ufisadi, Chadema iliona mfumo huu ni more effective au ilitokana na ukosefu wa ubunifu?

Chadema wanasahau kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Muungano wa TANU na ASP, na chama kiliposhika hatamu mwaka 1977, ndio kikaja na mfumo wake ulioendelea mpaka pale vyama vingi vya siasa ulipoingia, ambapo ilbidi ubadilishwe kidogo na kuendelea mpaka hivi sasa; Chadema inaonekana wanacheza ngoma ile ile, sasa sielewi kama ni mfumo effective? Ukosefu wa ubunifu? ni matakwa chini ya sheria ya msajili wa vyama vya siasa?

cc: candid scope

Selection process yao haina tofauti na ile ya CCM. Selection process inaweza kuwa inclusiveness or exclusiveness. Inclusiveness ni necessary condition for democratisation. The more inclusive the candidate selection, the more open, transparent and democratic the selection process can be and the more representative and legitimate mandate the candidate can claim to have.

Do party insiders control the candidacy of presidential hopefuls or is it the voters who make up the selectorate? Kwa sasa ni watu wachache tuu wanakaa na ku-select anayefaa kugombea Urais. Wananchi hawahusishwi kabisa. Wao wanaletewa tuu mgombea wam-elect kuwa Rais. Hatutaki watu wajifunge kwenye chumba halafu watoke na jina la mgombea kuwa this is the one we have selected for you to elect. Over my dead body!

Vyama vinaogopa kuwahusisha wananchi kwenye selection process simply because hii inapunguza role ya elites kwenye kuchagua nani awe rais. Kila siku tunaimba kuhusu transparency and participation. This should extend to the selection of presidential candidates as well. Kama unaletewa mgombea ambaye ameshakuwa selected na watu wachache halafu unaambiwa mchague kuwa kiongozi, akitokea kuwa kiongozi mbaya nani wa kulaumiwa? Ndiyo maana viongozi wakishakuwa elected tuu wanaongoza wanavyotaka kwa sababu hatuwezi kuwafanya chochote. We did not select them.

Suala la Zitto kujitangazia kugombea Urais linaweza kutokana na selection process ya mgombea ndani ya Chadema kuwa dominated by party elites. May be he is sending across a certain message ya kuwepo kwa personalty and individualism kwenye chama chake. Hii ni common sana kwenye vyama vipya na vile ambavyo ni extremely personalistic and individualistic. Kwenye vyama vya aina hii hata viongozi wao ambao hawawezi tena kugombea kwa sababu mbalimbali, wana-handpick a "crown prince" kama mgombea wa urais.

Mfano, angalia Rawlings's selection of Atta Mills in Ghana 2000, Frederick Chiluba's selection of Levy Mwanawasa in Zambia 2001, and Daniel Arap Moi's selection of Uhuru Kenyatta in Kenya 2002. Hata hapa kwetu, tulishawahi kuambiwa na party elite fulani kuwa kama tunamchagua mtu kwa sura yake basi tumchukue tukanywe nae chai. This party elite wanted his "crown prince" he handpicked kuwa rais.

Alternatively, labda Zitto ameona hataweza ku-achieve his super dream ndani ya Chadema kirahisi kwa sababu watu wengi huko Chadema wanam-regard as a dissenting politician ndani ya chama. Kwa sababu hiyo, the only option ni kuanzisha chama chake cha siasa au kugombea kama mgombea binafsi. Kwa hiyo kutangaza kugombea Urais kutamfanya actually asiwe selected kugombea kupitia Chadema kwa sababu ya ku-dissent na hivyo kumpa nafasi ya ku-pursue his presidential ambition in either of the two options.

Self-nomination ni viable option kwa ambitious politician kama Zitto. Lakini ukiangalia kwa undani, hii ni strategy inayotumiwa na wanasiasa ambao wameshindwa kupata nomination kwenye vyama vyao hasa vile vikubwa. Kwa hiyo, self-selection is pretty much a sub-category of elite arrangement. Ndiyo maana watu kama akina jmushi1 wana-argue kuwa kuna elites nje ya Chadema ambao wako kwenye process ya kum-select Zitto kugombea urais kwa interests zao.
 
Mkwawa nakubaliana na uliyosema. Labda kwa manufaa ya wasomaji tuu, kuna tofauti kati ya nomination na selection of a candidate. Hizi ni processes mbili tofauti ambazo mara nyingi hutumika interchangeably. Nomination ni procedure ya kisheria ambapo mamlaka husika zinam-certify mgombea mtarajiwa kama amepita vigezo vyote vya kisheria kugombea and print his/her name on the election ballot for that office. Candidate selection ni extralegal process ambapo chama kinaamua ni nani anayefaa kugombea hiyo nafasi. This is where my point lies.
 
Last edited by a moderator:
Iwapo ulisoma bandiko langu namba moja la uzi huu hadi mwisho, nilimalizia kwa kusema haya:


Hujajibu swali,
labda nikuulize interest kwa zitto imekuje? Kwa nn isiwe wagombea wa ccm ndio uwafanyie hiyo tathmini? Au ulishamaliza tathmini yao , na kama ndio majibu yake yako vipi? Umeweka wazi ww ni mwana ccm unayefanya tathmni ya kiongozi anaetakiwa, tupe kwanza huko kwenu kupoje- charity starts at home!
 
umri wa kugombea urais ni miaka 40 ama imebadilishwa??? Manake mwaka 2015 Zitto atakuwa na miaka 39, hapo itakuwaje wadau?? Ama katiba mpya itakuwa imefanya marekebisho katika suala la umri??
 
Kwa sababu zinatawaliwa na hoja zenye wepesi katika suala zito;
Mkuu Suala la ZItto kutaka kugombea URAIS wala sio Zito kama unavyotaka kutuaminisha hapa.
Ni Suala Jepesi Mnoo, Kutokana na Katiba ya Sasa, Zitto kuna sifa ana lack za Kugombea.
So kitu atakachokifanya ni Kuhakikisha kuwa suala la Umri linarekebishwa kwenye mchakato wa katiba Mpya chini ya Tume ya Judge Warioba ili apate sifa za Kuwa Mgombea which is BASICALLY NI UBINAFSI NA UROHO WA MADARAK ambao kimsingi unampotezea sifa zoote za kuwa hata katibu wa Tawi la Chama.......Over.
 
bado hamjafahamu kwa nini Zitto analalamikiwa,Mchambuzi ametoa hoja nzuri kuijadili kama changamoto kwa vyama lakini hoja hizo si muafaka kwa aina ya malalamiko ya wapenda mageuzi wengi juu ya Zitto.
mfano ili nieleweke,mnafikiri Mnyika angetangaza nia angelalamikiwa kwa hoja anazolalamikiwa Zitto?
tatizo la Zitto si kitendo cha kutangaza nia tu ni mengi yanayoambatana na hilo.
 
huyu zito amewalipa bei gan? Manake kutwa kuchwa mnamjadili!! Hebu subirin 2mzike kamanda balo kwanza hki ni kipind cha majonzi makubwa kwa taifa!!


Wapendwa watanzania na wana CDM. Zitto amkwenye mtego nasi tumenasa. Mtego wenyewe ni kujadili watu. Zitto ametutumbukiza huko kwa kujua ama kutokujua, ni kwa tamaa ya tamaa zake tu, ama kwa makusudi akijua madhara yake. Badala ya CDM sasa kujadili namna ya kupenya vijijini, tunashindwa kutwa tunamzungumzia Zitto. Mimi nashauri tumpuuze yeyote anayejaribu kututoa kwenye focus.

Mambo anayofanya Zitto si mageni, na ni silka yake tu na wakati wote huwa haimsaidii sana yeye kama anavyojaribu kutuaminisha. Alijaribu uenyekiti, akapigwa chini, akavamiwa uongozi wa kambi ya upinzani bungeni, akapigwa chini, sasa amekurupuka na urais, sasa mtu wa namna hii si wa kumpuuza tu? Hii haijalishi kama alishiriki vipi kukijenga chama huko nyuma kama wengine wanavyojaribu kumtetea, sisi tunaangalia mbele na Mrithi wa JK bado sana kumjua. Tuendelee na harakati za elimu kwa uma, M4C, Rais yupo tu, na naomba kwa Mungu asiwe Zitto.

Tupuuze kabisa hizi hoja za Zitto na mjadala huu ufungwe.
 
Mchambuzi hoja ya watu kumpinga Zitto zipo hivi;

Ielelweke kuwa Zitto hajavunja kanuni yoyote ya chama au katiba ya CDM kutangaza kugombea urais 2015. Tatizo linakuja, hajafanya "proper timing" ya yeye kutangaza suala hilo. Leo ni 2012, mpaka 2015 bado safari ni ndefu sana upepo wa kisiasa unaweza kuvuma vyovyote.

In connection to that, CCM inateswa na mzimu wa urahisi 2015. Sasa kitendo cha yeye kutangaza hilo maana yake hajajifunza makosa ya CCM kukesha kulumbana, kuhujumiana n.k kwa sababu ya urais tu!!!!! Sasa kwa nini yeye asijifunze kutoka kwa wapinzani CCM?????

Mimi ningeomba Zitto aelewe mpaka sasa CDM haijasema itamsimamisha nani kwa sababu inajua kazi kubwa iliyopo mbele yake ya kuchanga karata yake vizuri katika kipindi kilichobaki ili 2015 mambo yaende kama ndoto zao zilivyo yaani kushika dola.

Nijuavyo Zitto ni mjuvi sana na si kwamba haya tusemayo hayajui ila sielewi ni kwa nini anafanya hivi. Namtahadharisha asidhani CCM tayari imeshindwa 2015 kiasi cha kung'ang'ania au kugombea urais kiasi hicho.

Namuombea kwa Mungu ampe uhai na hekima ili KUDRA ya Mwenyezi Mungu ifanye kazi.
Nakubaliana na wewe ni mawazo yangu ya kua wengi wanaopinga kauli ya Zitto kuelekea uchaguzi 2015 hawana matatizo na Zitto kwa uwezo wake wa kua Rais au utendaji wake wa kazi,amefanya mengi na anaendelea kufanya mengi katika kukijenga chama.Tatizo ambalo nafikiri wengi wanaopinga kauli yake hiyo ni wakati,wakati aliouchagua kutoa kauli hiyo SIOMUAFAKA "proper timing"Ni mapema na imezua malumbano na kuwaondoa watu katika hoja ya muhimu ya kukijenga chama na kuanza kujadili kauli ya Zitto hali ambayo inaweza kupelekea chuki,migawanyiko na makundi kama ilivyo katika CCM na kuigawa nguvu ya chama ambayo ni muhimu sasa katika kujiimarisha.Mh.Zitto ujenzi wa CHADEMA sasa umefikia katika ngazi ya madirisha ingelikua vizuri iakaongezeka juhudi ya kumalizia paa kabla ya mvua{Uchaguzi 2015}Badala ya kuanza kujadiri nani atafungua nyumba hiyo kitendo ambacho kinaweza kutufanya imvua itukute kabla ya kumalizia paa na hivyo kuaribu kila kitu.MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Back
Top Bottom