Uzinzi ni dhambi lakini si kosa kisheria

Wakati sasa umefika wa kutunga sheria mpya ya kudhibiti dhambi ya uzinzi, kama ilivyo kwa makosa mengine.

Sheria hiyo mpya iweke wazi kuwa, mtu yeyote akizini atakuwa ametenda kosa la jinai na apewe adhabu kali.

Tukifanikiwa kutunga sheria hii, tutaweza kupunguza mimba za utotoni kwa kiasi kikubwa.
nakubaliana na mtoa mada.

1. Uzinzi ni dhambi, hilo halina mjadala kwasababu vitabu vya dini vinaeleza hilo. uzinzi maana yake ni kufanya mapenzi na mtu asiye mke wako (kwetu sisi wanaume).

2. uzinzi ni kosa la jinai kama umeufanya na mwanamke kwa kulazimisha (bila ridhaa yake). adhabu yake ni kifungo kisichopungua 30yrs hadi life.

3. uzinzi hata kama umetokana na ridhaa, kama mwanaume mtu mzima ataufanya na binti chini ya miaka 18 ambaye sio mke wake, ni kosa la jinai. adhabu yake ni kifungo cha miaka isiyopungua 30 hadi life.
 
Uzinzi = Zinaa, ni dhambi kwa mujibu wa vitabu vitakatifu vya dini za kiislam, kikristo, nk.

Ila kwa hapa nchini kwetu Tanzania, zinaa (uzinzi) si kosa kwa mujibu wa sheria, na hakuna kanuni za adhabu katika mahakama zetu.
... tena kwa sheria za Tz ukimjeruhi (kuua umeenda mbali sana) kidume uliyemfuma akimgonga mkeo ni kosa lenye kustahili adhabu mbele ya sheria. Unatakiwa upite kando ukafungue kesi ya kuomba fidia; ni suala la madai wala sio jinai.
 
Usiue = kuua ni kisa la jinai
Usiibe = wizi ni kosa la jina
Usizini = ????
... usiue ==> ni kosa la jinai kwa sababu unamsababishia madhara uliyemtendea kosa; usimtendee jirani yako usivyopenda kutendewa naye!
... usiibe ==> ni kosa la jinai kwa sababu unamsababishia madhara uliyemtendea kosa; kanuni ya usimtendee jirani yako usivyopenda kutendewa naye ina-apply!
... usizini ==> hakuna madhara ya moja kwa moja kati ya wawili wafanyao uzinzi. Kanuni ya usimtendee jirani yako usivyopenda kutendewa naye hai-apply! Hence, inakosa misingi ya kisheria. Simple logic!
 
Dhambi labda ukimlazimisha mtu, Mungu aliweka starehe ambayo inamsaidia katika kazi ya uumbaji. Alishasema nendeni mkaijaze Dunia, hiyo dhambi iko wapi?
 
Back
Top Bottom