Uzi maalum wa kuishauri serikali

Uzi maalum wa kuishauri serikali

Rais mstaafu JK juzi kaongea kitu kizuri mno! Alitoa ushauri katika ujumla wake.... Maneno yake yale hata kama tunaweza kusema hakumaanisha lakini yameamsha hamasa mpya mbele ya hadhira na kile kilichokuwa kilio cha wengi.... Kunyanyapaa na kunyanyasa wale tunaopingana nao!
Pengine kuna lingine nyuma ya pazia na inawezekana kabisa hafurahishwi na yale majipu yanayotumbuliwa sasa(kwakuwa yanamgusa moja kwa moja) lakini tuseme tu kwamba amesema ambalo viongozi wengi wastaafu wameshindwa kabisa kulisema
Na tumuunge JK kwenye hili.... Amejitokeza kushauri kwa uwazi! Amefungua njia tupite kwa uhuru sasa ila tusiiharibu hata ambao walikuwa hawasikii watasikia sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli, maadam ni serikali sikivu na ya wanyonge, watu wote kwa mimi, ushauri wangu ningependa vitu vyote vinavyouzwa viwekewe bei elekezi kama ni kiberiti kiandikwe code zake na bei yake kama vocha,
Ili hata hao wanaopandisha vitu tupate kuwajoji..... Imekuwaje
Na kwa njia hii itakuwa rahisi kujua kitu harisi na bandia.
Mf. Mzuri bidhaa za nje huwekwa code na bei yake

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna soko kama hilo duniani kwa sababu kila mfanyabiashara anapata gharama tofauti na mwingine katika kuendesha biashara yake so this can't be done.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi nauliza tu kwanini tunalipa kuingia Ubungo Bus Terminal kuna huduma gani ya ziada kwa raia wa kawaida tunayoipata? Kama ni huduma ya choo tunalipia pia hata Mabasi yanalipia parking japo miundombinu ni mibovu. Kama ni utararatibu wa kisheria kwanini usiwekwe stendi zote nchi nzima?? Why Ubungo?? Hii inasumbua pia ni kero viongozi waliangalie hili ni usumbufu kwetu wananchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri wangu mkubwa Kwa serikali lazima tuwe na vipaumbele kama taifa ambavyo vinagusa maslahi ya wananchi wa kawaida..lakini pia kama serikali iepuke migogoro na wananchi ambayo inaleta chuki Kwa wananchi dhidi ya serikali yao...

ni kweli mkuu,isifike mahali tunauana wenyewe kama kibiti,
 
mie naona serikali isikurupuke kufanya vitu ambavyo vinawaletea sifa za muda mfupi,huku zikiwaacha kudharaulika...........hata majukwaani,kuongea iwe ya mwisho baada ya kila kitu kuwa done,ama thoroughly investigated.

Nashauri katika kazi au vipaumbele vya Taifa,viwe vinatajwa kwa uwazi, vitangazwe kwa mwananchi wa kawaida ,atoe maoni yake,nachosema ni Mwananchi aambiwe kila stage afahamu linaloendelea...............serikali ijenge platform ya mwananchi wa kawaida,kusema maoni yao.,,,,,,,before making decisions,serikali IWA INVOLVE WANANCHI WOTE,WABUNGE WETU SIO WAWAKILISHI WETU,WALE WAKO KIBINAFSI MULE,IJENGWE PLATFORM NYINGINE INAYOWARUHUSU WANANCHI KUSIKIKA FOR EVERY GOVERNMENT DECISION. SIO SASA HIVI,UNASKIA TU KIWANJA KINAJENGWA CHATO,BOMBARDIER IMEINGIA NCHINI,vitu ni bin vuuuup, am sure WANANCHI WANGESHIRIKISHWA THEN TUNGEONA THERSMORE than these(it wasn't in our prority lists)......................tunataka tushirikishwe kwenye mipango yote ya maendeleo,its national cake,we too,have a right to 'eat it'...............
 
Mi nauliza tu kwanini tunalipa kuingia Ubungo Bus Terminal kuna huduma gani ya ziada kwa raia wa kawaida tunayoipata? Kama ni huduma ya choo tunalipia pia hata Mabasi yanalipia parking japo miundombinu ni mibovu. Kama ni utararatibu wa kisheria kwanini usiwekwe stendi zote nchi nzima?? Why Ubungo?? Hii inasumbua pia ni kero viongozi waliangalie hili ni usumbufu kwetu wananchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee sahihi kabisa ile kero ya kiingilio cha ubungo terminal ni kubwa.... Na sijui yale mapato yanaenda wapi kwakuwa sioni maboresho yoyote..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mie nashauri serikali ipunguze kujenga ma barabara kila mkopo ni barabara tu, pesa nyingine zipelekwe kwenye wizara ya elimu,maji na afya. Wanavyuo sasa hivi hawapati mikopo kabisa hata wanaopewa ni kwa mbinde

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mie nashauri serikali ipunguze kujenga ma barabara kila mkopo ni barabara tu, pesa nyingine zipelekwe kwenye wizara ya elimu,maji na afya. Wanavyuo sasa hivi hawapati mikopo kabisa hata wanaopewa ni kwa mbinde

Sent using Jamii Forums mobile app
Na ni vema roadmap plan 2015- 2020 iwekwe wazi, na kupeana mrejesho kila tunapokamilisha jambo fulani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na ni vema roadmap plan 2015- 2020 iwekwe wazi, na kupeana mrejesho kila tunapokamilisha jambo fulani

Sent using Jamii Forums mobile app
Nchi hii sasa hv kila kiongozi anakuja na mambo yake..ni vyema kama Taifa tungekuwa na dira ya kutuongoza ili tujue tunaelekea wapi. Kukosekana kwa dira matokeo yake ndio kutunga sheria za hovyohovyo mwisho wa siku tunaua uchumi wa taifa tunaishia kutafuta mchawi ni nani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom