Uzi maalum wa kuishauri serikali

Uzi maalum wa kuishauri serikali

Mnajisumbua kwa uongozi huu ..ni sawa na kumpigia mbuzi gitaar mkitarajia amwage mauno bora Bata ....Rais mwenyewe anakuambia
..Sishauriki na ukijaribu ndo unaharibu kabisaaaa...vipi kwa vibaraka wake ..?
Ama kwel saul tumemtaka wenyewe acha ajitawale atakavyo...
"Kusikia kwa kenge hadi...."
Hapana hii mada itafika panapohusika na kuna baadhi (si yote) yatafanyiwa kazi... Trust me utaona kuna mabadiliko baada ya muda
Hivi hadi sasa maamuzi ya kukurupuka yamelitia taifa hasara kiasi gani vile...vile viwanda zaidi ya 1000 vimeajiri vijana kiasi gani vile ....hiv wale waliosema Rais aongezewe muda wa kuwa madarakani ni watz au wasomalia..? mbona twaweza wako kimya wapi tafiti au ile 1/4 imeongezeka..?
Hapa upepo tu kazi muulize punda....


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unashangaa nini..? unafikiri wakiamua hawawezi..? miafrika tutaendelea kulia umaskini kwa upumbavu wetu but we can made it.. mbona yenyewe yanatuletea dawa zenye madhara..? huko china uwo mchele wa plastic unafikiri government yao haijui..?
if you can't fight them join them! lkn kwa upande wako jilinde,wanauhitaji wa bangi tuwalime tuwapelekee lkn nahamasisha iwe chini ya ulinzi mkali..
leo hii kuna vitu tunavikataa lkn huko mbeleni vitakubaliwa tu lkn inategemea kwa misingi ipi..?

chengine inachokosea serikali haitoi semina kwa vijana ni namna gani watumie pesa zao ili wamentain maisha yao,wapi tuwekeze,sekta ipi inalipa nknk kuna watu wanapata milion 1,2,3...10+ lkn zinakwisha kama hayawani mwandamizi! umaskini upo kichwani mwetu.
 
Unashangaa nini..? unafikiri wakiamua hawawezi..? miafrika tutaendelea kulia umaskini kwa upumbavu wetu but we can made it.. mbona yenyewe yanatuletea dawa zenye madhara..? huko china uwo mchele wa plastic unafikiri government yao haijui..?
if you can't fight them join them! lkn kwa upande wako jilinde,wanauhitaji wa bangi tuwalime tuwapelekee lkn nahamasisha iwe chini ya ulinzi mkali..
leo hii kuna vitu tunavikataa lkn huko mbeleni vitakubaliwa tu lkn inategemea kwa misingi ipi..?

chengine inachokosea serikali haitoi semina kwa vijana ni namna gani watumie pesa zao ili wamentain maisha yao,wapi tuwekeze,sekta ipi inalipa nknk kuna watu wanapata milion 1,2,3...10+ lkn zinakwisha kama hayawani mwandamizi! umaskini upo kichwani mwetu.
OK OK sawa nimekupata vema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uzi mzuri sana huu mshana yakwangu ni haya mpk sasa serikali inachukiwa mno na watumishi kwanamna ilivyowanyima madaraja yao na stahiki zao za malimbikizo watumishi wameamua kukaa kimya ila moyoni wanajua wanachowaza kiufupi serikali inajitengenezea chuki kubwa mara dufu kabla ya uchaguzi imagine mshahara aliouacha jakaya haujawahikupanda ila umeshuka mara dufu ukiona Kuna mtumishi anaisema serikali vizuri ujue ni kiunafiki asilimia 98 wanaichukia huo ndio ukweli serikali ilione hili irekebishe taswira yake kwa watumishi wake hongera mshana kwa Uzi huu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mie ushauri kwa serikali nauchukulia kama KUPANGIANA...mpaka kauli ya TUSIPANGIANE itakapofutwa nitatoa ushauri wangu.

Na kama hauamini nisemayo basi naanza na ushauri huu mwepesi tuu..SERIKALI IRUHUSU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA KAMA WAKATI WA JK NA MKUU AKUBALI KUWAITA WAPINZANI IKULU WANYWE NAYE CHAI AONE MAMBO YATAKAVYONYOOKA.

haipendezi laisi kuweka beef na watu wake hasa wanaotakiwa kumsaidia kuona nchi inapoenda mrama...UPINZANI SIO UADUI.

WAANZE NA HILO LISILOGHARIMU HATA MIA YA SERIKALI...MENGINE YAJA.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
Unaweza kua na mawazo mazuri lakin ebu fafanua anachukiaje wapinzani na ukatupa na evidance itakua poa zaid, na je kusema mikutano na maandamano mpka 2020 ni kuwachukia wapinzani au?unaitafsiri vip chuki ilohali anawachagua sehem ya kutekeleza majukumu ya nchi hao hao? Je nikisema upinzani ndo unaichukia serikali unaweza kunisahihisha vip kwa hoja? Je nikisema upinzani unatamani serikali ifilisike, serikali ifilie mbali, serikali ikose msaada wwte, serikali ikwame kila sehem na wapinzani wakiona hali ni tofauti na matarajio yao kwa nn wasikubali ukwel unaoonekana?chuki na wapinzani kama unavyotuaminisha zinatokana na nini zaid? Je kungekua na mikutano na maandamano suala la chuki dhidi yao lingesemwa au vip?

Mwsho namweshimu sana mleta uzi, jibu kistaarab huku ukiamin mawazo yako yatasaidia wengi na hata yanaweza wafikia tunaowalenga,,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu uzi ni mzuri sana hasa kwa wenye mawazo sawiya na mleta uzi iwapo jazba,mizaha,vyama n.k vikiwekwa pembeni lakini kwa huko tuendako naona kama makusudio ya uzi huu unaaanza kupotea taratibu waTanzania tunapenda sana kulalamika kwanini tusitumie fursa kama hizi kuwasilisha mawazo yetu na ushauri kwa serikali kwa nia ya kujenga zaidi na matunda yake sote tutayaona hapa
 
Najaribu kufanya uzi wenye manufaa kwa serikali jukwaa na kila mmoja wetu lakini naona kuna changamoto zake.... Anyway tutafika tuui
Nina uhakika wengi tuna cha kuishauri serikali yetu, usihofie kama ushauri wako utafanyiwa kazi ama la, wewe andika maandishi hayafutiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali iache ubabe na matamko yasiyo na mantinki kupitia kwa wakuu wa mikono, wilaya na mawaziri pia serikali ipitishe mijadala yake yote kwa wadau wa sekta husika kabla haijatoa tamko,Raia, Wanafunzi wengi sasa ivi wamekatishwa sana ndoto zao.
 
Ushauri wangu mkubwa Kwa serikali lazima tuwe na vipaumbele kama taifa ambavyo vinagusa maslahi ya wananchi wa kawaida..lakini pia kama serikali iepuke migogoro na wananchi ambayo inaleta chuki Kwa wananchi dhidi ya serikali yao...
 
Mi nashauri kwa wale wazawa waanzilishi wa viwanda vidogo vidogo serikali itoe tax holiday ili wakisha kaa sawa ndio ianze kiuwachaji kodi. Unaanzisha kiwanda hata hujajua mbeleni itakuaje unakumbana na serikali wanadai magharama kibao mwishowe unaishia kufunga tu kiwanda
 
iweke maafisa habari kila wilaya, maana nim eona kuna mapungufu makubwa sana katika wilaya, yani huwezi jua nani kafanya nini na kwa lini mpka lini ila hii kazi ilitakiwa iwe inaandikwa na afsa habari na kutoa taharifa ya utendaji kwa wannchi sio siri serikali ina watumishi wengi Mizigo
 
Back
Top Bottom