Uzi maalum wa kuishauri serikali

Uzi maalum wa kuishauri serikali

Vyama havipiti...vipo kwa mujibu wa katiba...DEMOKRASIA NA UHURU WA KUONGEA....then mengine yafuate katiba.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu

Ushauri wangu mkubwa Kwa serikali lazima tuwe na vipaumbele kama taifa ambavyo vinagusa maslahi ya wananchi wa kawaida..lakini pia kama serikali iepuke migogoro na wananchi ambayo inaleta chuki Kwa wananchi dhidi ya serikali yao...

Mi nashauri kwa wale wazawa waanzilishi wa viwanda vidogo vidogo serikali itoe tax holiday ili wakisha kaa sawa ndio ianze kiuwachaji kodi. Unaanzisha kiwanda hata hujajua mbeleni itakuaje unakumbana na serikali wanadai magharama kibao mwishowe unaishia kufunga tu kiwanda

iweke maafisa habari kila wilaya, maana nim eona kuna mapungufu makubwa sana katika wilaya, yani huwezi jua nani kafanya nini na kwa lini mpka lini ila hii kazi ilitakiwa iwe inaandikwa na afsa habari na kutoa taharifa ya utendaji kwa wannchi sio siri serikali ina watumishi wengi Mizigo


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri wng mkuu kwa serikali yetu ni kuacha kutumia nguvu kubwa kupambana na watu/wanasiasa wenye mitazamo tofauti na viongoz wa serikali...
Serikali ktk awamu zilizopita iliona chama cha mapinduzi pekee hakiwez kutuletea maendeleo ndio maana wenye busara zao wakaamua kuruhusu uwepo wa vyama pinzan vitakavyoleta mawazo mbadala kwa kuikosoa na hata kuichachafya serikali kwa hoja pale inapobid......
Naishauri serikali iruhusu ustawi wa vyama vya upinzan kwa manufaa ya Tanzania yetu
 
Ushauri wng mkuu kwa serikali yetu ni kuacha kutumia nguvu kubwa kupambana na watu/wanasiasa wenye mitazamo tofauti na viongoz wa serikali...
Serikali ktk awamu zilizopita iliona chama cha mapinduzi pekee hakiwez kutuletea maendeleo ndio maana wenye busara zao wakaamua kuruhusu uwepo wa vyama pinzan vitakavyoleta mawazo mbadala kwa kuikosoa na hata kuichachafya serikali kwa hoja pale inapobid......
Naishauri serikali iruhusu ustawi wa vyama vya upinzan kwa manufaa ya Tanzania yetu
Natamani ushauri huu ufanyiwe kazi katika muktadha wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri wangu mwingine naojua pia hautofanyiwa kazi kwa vigezo vya TUSIPANGIANE..

VYEO VYA MA DC NA RC VIONDOLEWE TUBWKI NA WAKURUGENZI WA MAENDELEO WA WILAYA NA MIKOA....TUTAOKOA ZAIDI YA ROBO YA BAJETI YA TAMISEMI ila hao ndio itakuwa chama dola kimejiondoa madarakani maana ni wanasiasa maslahi kwa chama tawala na sio taifa.

KUCHAGUA NI KUPANGA NA KUPANGA NI KUAMUA....MASLAHI YA TAIFA AU MASLAHI YA CHAMA.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
 
Kuna hili la jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani.. Rushwa ni donda ndugu kwenye hii kada na wanachafua jina la nchi hata kimataifa kwa kuomba rushwa waziwazi kwa wageni
LESENI. : Kitengo hiki nacho ni majanga pale kinachokupa LESENI ni pesa yako sio vigezo....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1.Tulitangaziwa kuhusu BOT kuzipunguzia Benk riba,sasa serikali iweke riba elekezi kwa mabenki ili wakopeshe wananchi.
2. Madaraja ya watumishi wa umma imekua kero sasa.
3. Watanzania tumezoea kuishi kwa upendo. Serikali hii ionyeshe upendo kwa majimbo yote. Kusiwepo na ubabe.
 
Mi nitashaur sehem Mbili muhim Kama watauchukua huu ushaur Nakuhakikishia Umasikin by by nchi.
Naanza na kilimo.
Juz Kati hapa nilimsikia Wazir Mkuu Mh. Majaliwa Cassim Majaliwa akizuia Watu kuuza mahind nje ya nchi hususan Kenya. Sasa ukiangalia Katika sura ya karibu hili jambo ni jema lakin kama unaona mbali ni kosa kubwa la kimkakati. Nitatoa mifano.
Dunian kote kila nchi inapambana kutafuta masoko. Na kwa hapa kwetu tuna uhakika wa soko la bidhaa za kilimo Kenya, Zambia, na hata sehem ya Congo. Mi nilifikir sasa serikali ingetumia fursa hiyo kuhimiza Watu wakalime ili wachangamkie hilo soko. Mfano mi nafanya biashara ya Nguo kkoo lakin miaka mawili nyuma nimejiwekeza kwenye kilimo nimepata faida na kwa hii faida Watu wengi wamenifuata nyuma kuja kulima sasa changamoto iliyojitokeza serikali imezuia masoko wakat wangeweza kuwaweka Watu wa TRA mipakan na kuchaji kila Lory kiasi flan wanapata hela nzur tu na vijana wengi wangeenda kulima nchi kwanza ingejitosheleza kwa chakula Pili ingeuza nje na kuleta hela za kigen. Serikali inadai kwanza tukiruhusu Watu wakiuza chakula kitaisha lakin unaweza kuwawekea utaratibu kwamba kila familia Kama kuna anaetaka kuuza chakula ahakikishe amotoa labda kila nyumba gunia tatu kinachozid kinauzwa kama wanavyofanya Watu wa Kilimanjaro huwa kuna eneo kinawekwa chakula cha akiba. Nitatoa mawazo mengine cku nyingine
 
'Serikali' alishakana kuamini mitandao ya jamii. Hata swala la yule jamaa anayedaiwa kutokuwa na vyeti lilipuuzwa...hata mh.Meya alipowasilisha rasmi bado ilipuuzwa.

Lakini labda serikali 'itachambua-chambua' ushauri unaoipendeza...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri wangu mwingine naojua pia hautofanyiwa kazi kwa vigezo vya TUSIPANGIANE..

VYEO VYA MA DC NA RC VIONDOLEWE TUBWKI NA WAKURUGENZI WA MAENDELEO WA WILAYA NA MIKOA....TUTAOKOA ZAIDI YA ROBO YA BAJETI YA TAMISEMI ila hao ndio itakuwa chama dola kimejiondoa madarakani maana ni wanasiasa maslahi kwa chama tawala na sio taifa.

KUCHAGUA NI KUPANGA NA KUPANGA NI KUAMUA....MASLAHI YA TAIFA AU MASLAHI YA CHAMA.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
Hili ni jambo muhimu sana.hata idadi ya mikoa ingepunguzwa kuepuka gharama.
 
Mi nitashaur sehem Mbili muhim Kama watauchukua huu ushaur Nakuhakikishia Umasikin by by nchi.
Naanza na kilimo.
Juz Kati hapa nilimsikia Wazir Mkuu Mh. Majaliwa Cassim Majaliwa akizuia Watu kuuza mahind nje ya nchi hususan Kenya. Sasa ukiangalia Katika sura ya karibu hili jambo ni jema lakin kama unaona mbali ni kosa kubwa la kimkakati. Nitatoa mifano.
Dunian kote kila nchi inapambana kutafuta masoko. Na kwa hapa kwetu tuna uhakika wa soko la bidhaa za kilimo Kenya, Zambia, na hata sehem ya Congo. Mi nilifikir sasa serikali ingetumia fursa hiyo kuhimiza Watu wakalime ili wachangamkie hilo soko. Mfano mi nafanya biashara ya Nguo kkoo lakin miaka mawili nyuma nimejiwekeza kwenye kilimo nimepata faida na kwa hii faida Watu wengi wamenifuata nyuma kuja kulima sasa changamoto iliyojitokeza serikali imezuia masoko wakat wangeweza kuwaweka Watu wa TRA mipakan na kuchaji kila Lory kiasi flan wanapata hela nzur tu na vijana wengi wangeenda kulima nchi kwanza ingejitosheleza kwa chakula Pili ingeuza nje na kuleta hela za kigen. Serikali inadai kwanza tukiruhusu Watu wakiuza chakula kitaisha lakin unaweza kuwawekea utaratibu kwamba kila familia Kama kuna anaetaka kuuza chakula ahakikishe amotoa labda kila nyumba gunia tatu kinachozid kinauzwa kama wanavyofanya Watu wa Kilimanjaro huwa kuna eneo kinawekwa chakula cha akiba. Nitatoa mawazo mengine cku nyingine
Unajua nakubali kabisaa.hii ishu ya kilimo tanzania imefanyiwa siasa sana.wengi wanashindwa kuelewa kilimo cha leo ni biashara.kilimo hakina tofauti na biashara yoyote ile.hiv unaweza kuingiza hela ktk biashara halaf mtu ambaye hata senti moja hakuweka akupangie bei? Serikal iruhus watu wauze wanapotaka..kwa bei wanayotaka.ila wao waangalie namna ya kupata kod ndogo.
 
Serikali itangaze kununua mazao mfano mahindi toka kwa wakulima mwakani na iyahifadhi yenyewe ndio iuze nje! Mwaka 2014/2015 NFRA Dodoma ilinunua mahindi toka kwa wakulima kilo @500/ ilikuwa jambo njema sana na hela hiyo ilikuwa kubwa sana. Kuna mwamko mkubwa wa wananchi kufanya kazi sasa, serikali iwaunge mkono kwa kuwalipa ili wawe na hela kurahisisha mzunguko fedha na kupunguza umaskini jambo litakolo punguza lawama kwa Govt yetu pendwa. Vijijini Vijana waanzishe vikundi na wakopeshwe matrekta na mbegu badala ya fedha. Mfano yale mabilioni ya Kikwete yaliliwa tu sijui kama hata 50% ya hiyo hela ilirejeshwa. Serikali ishughulikie kuondoa malalamiko kwa wananchi wake mfano watumishi walipwe stahiki zao sasa, wananchi wanaobomolewa nyumba zao kwa upana 121m kama haikuwa hivyo kabla ya ujenzi walipwe fidia, na kama haistahili mbona wahusika hawatoi ufafanuzi , tunasikia upande wa wanaovunjiwa tu. Kimsingi kuna kitu chema Mhe. Rais anajenga kwa Taifa letu, tumuunge mkono, ni mwanadamu si malaika . Mhe.Rais imetosha sasa lawama,lawama nyingi hasa kwa wananchi wako wa chini, wastaafu, wajane na mayatima ambao nyumba zao zinavunjwa.
 
Nashauri serikali iongeze bajeti kwa ajili ya wanafunzi wanaokwenda kusoma nje ya nchi watanzania wengi wapate fursa ya kwenda kujifunza technologia mbalimbali katika nchi mbalimbali zilizoendelea watakaporudi watumie uzoefu walioupata waipeleke mbele Tanzania katika utendaji wa viwanda ,afya, miundombinu, na uchumi kwa ujumla. Watanzania bado tuko nyuma kielimu kulinganisha nawenzetu hata wa EAC Kama Kenya na Rwanda. Nchi iliyo nawasomi wachache kuendelea nivigumu Sana. Elimu ni ufunguo wa maisha.Tanzania Kwanza.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
'Serikali' alishakana kuamini mitandao ya jamii. Hata swala la yule jamaa anayedaiwa kutokuwa na vyeti lilipuuzwa...hata mh.Meya alipowasilisha rasmi bado ilipuuzwa.

Lakini labda serikali 'itachambua-chambua' ushauri unaoipendeza...

Sent using Jamii Forums mobile app
Nashauri tuandike tu! Tuandike sana lakini kwa makini weledi na tafakuri chanya.... Maandishi hayafutiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nashauri utaratibu wa kukagua waliofungua biashara zao jumamosi kabla ya saa nne asubuhi na kuwakamatwa ubadilishwe mara moja.

Kama hoja ilikua ni kufanya usafi kila jumamosi hapa dar es salaam,basi wajikite zaidi kwenye kukagua maaneo yaliyo machafu kisha ndo wahusika wachukuliwe hatua.kuliko ilivyo sasa hata eneo linalo kuzunguka likiwa safi bado watakukamata tuu na kukutoza fine.ili kua hamsini sasa wanatoza lakimoja.

Ukurupukaji huu umesababisha lengo husika la jiji kua safi lisifikiwe,kwani watu hulala ma kwao hadi hiyo saa nne ndipo hufungua biasahara zao bila kufanya usafi.
 
Back
Top Bottom