UWT YASIMAMA KIDETE KUMSAIDIA NDUGU. MARIA NGODA KATIKA KESI INAYOMKABILI
RUFAA YA MARIA NGODA YASIKILIZWA
IRINGA
Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Ikiongozwa na Mwenyekiti wake Ndugu. Mary Chatanda (MCC) imeendelea kusimama kidete katika kuhakikisha inamsaidia Mwanamama Maria Ngoda ambapo jan Tarehe 01 Februari, 2024, Mahakama Kuu ya Mkoa Wa iringa Chini ya Jaji Mfawidhi Mgetta imesikiliza kesi ya Rufaa Namba 84101/2023 kati ya Ndg Maria Ngoda (almaarufu Mama wa Nyama wa Swala) Dhidi ya Jamhuri.
Akiongoza jopo la Mawakili nane (8) upande wa mrufani wakili Moses Ambwindile wakishirikiana na Mwanasheria Kutoka Umoja wa wanawake (UWT) Amesema, wametetea Sababu zao za Rufaa 14 mbele ya Jaji Mfawidhi , Aidha Jaji Mgetta ameahirisha Shauri hilo mpaka hapo tarehe 2 Februari, 2024 (leo).
Mfungwa Maria Ngoda (mkata rufaa) alihukumiwa kifungo cha miaka 22 kwa kukutwa na vipande 12 vya nyama ya swala mnamo tarehe 3 Novemba, 2023.
#UWTImaraJeshiLaMamaSamia
RUFAA YA MARIA NGODA YASIKILIZWA
IRINGA
Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Ikiongozwa na Mwenyekiti wake Ndugu. Mary Chatanda (MCC) imeendelea kusimama kidete katika kuhakikisha inamsaidia Mwanamama Maria Ngoda ambapo jan Tarehe 01 Februari, 2024, Mahakama Kuu ya Mkoa Wa iringa Chini ya Jaji Mfawidhi Mgetta imesikiliza kesi ya Rufaa Namba 84101/2023 kati ya Ndg Maria Ngoda (almaarufu Mama wa Nyama wa Swala) Dhidi ya Jamhuri.
Akiongoza jopo la Mawakili nane (8) upande wa mrufani wakili Moses Ambwindile wakishirikiana na Mwanasheria Kutoka Umoja wa wanawake (UWT) Amesema, wametetea Sababu zao za Rufaa 14 mbele ya Jaji Mfawidhi , Aidha Jaji Mgetta ameahirisha Shauri hilo mpaka hapo tarehe 2 Februari, 2024 (leo).
Mfungwa Maria Ngoda (mkata rufaa) alihukumiwa kifungo cha miaka 22 kwa kukutwa na vipande 12 vya nyama ya swala mnamo tarehe 3 Novemba, 2023.
#UWTImaraJeshiLaMamaSamia