Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,902
- 945
CDE. REUBEN SAGAYIKA AWASHIKA MKONO WATOTO YATIMA KUELEKEA MWAKA 2024
Ndugu Reuben Sagayika ambaye ni Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa pamoja na Mjumbe wa Baraza Kuu la UWT Taifa kutokea Mkoa wa Geita, Ndugu Mery Mazula wameongozana na viongozi mbalimbali wa CCM tarehe 31 Disemba, 2023 na kutembelea kituo cha kulelea watoto yatima cha Ebenezer kilichopo Kata ya Buhalahala na kutoa misaada kwaajili ya kuukaribisha mwaka 2024.
Vilevile, Katika kuumaliza mwaka 2023 na kuukaribisha Mwaka 2024 Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana CCM Taifa (UVCCM) Mkoa wa Geita, Reuben Sagayika ametoa msaada wa vitu mbalimbali kwa wagonjwa waliopo kwenye Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.
Aidha, Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana CCM Taifa (UVCCM) Mkoa wa Geita, Reuben Sagayika ameambata na viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Geita ambapo akiwa kwenye Hospital ya Rufaa ya mkoa wa Geita amepita na kutoa pole kwenye wodi mbalimbali ikiwemo ya kinamama, watoto na wanaume.
Attachments
-
WhatsApp Image 2024-01-02 at 20.28.05.jpeg45.1 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2024-01-02 at 20.28.06.jpeg52.6 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2024-01-02 at 20.28.08.jpeg41.5 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2024-01-02 at 20.28.08(1).jpeg43.8 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2024-01-02 at 20.28.09(1).jpeg49.5 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2024-01-02 at 20.28.09.jpeg49.6 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2024-01-02 at 20.28.07(1).jpeg55.8 KB · Views: 2
-
WhatsApp Image 2024-01-02 at 20.28.07(2).jpeg52.1 KB · Views: 2