Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

Dunia imekuwa kama kijiji kutokana na uwezo mkubwa aliounyesha mwanadamu wa kugundua hata ambavyo vilifikirika kwamba haviwezekani

Elimu na ufahamu kuhusu mwili wa mwanadamu kuanzia kuumbwa tumboni kuzaliwa hadi kufa umetafitiwa na kunyumbulishwa kwa mapana yake na wengi wamepata elimu ya juu kabisa PhD kwenye hili eneo, lakini wakashishindwa kitu kimoja tuu!!! Uwezo wa kumuita marehemu na kuongea naye

Zamani kabla ya dini za kigeni hazijaja Africa tulikuwa kwa kiasi fulani tuna uwezo wa kuwaita marehemu kwa njia ya matambiko na kuwaomba hili au lile, lakini ikumbukwe kwamba hawakuja live bali dalili na ishara kadha zilionyesha uwepo wao na kukubali au kukataa ombi husika

Tumekuwa tunaondokewa na wapendwa wetu na watu tunaowahitaji mno katika maisha yetu, tumekuwa na vipindi vigumu kabisa ambapo tunawahamu na kuwahitaji japo wajitokeze kwa dakika chache tu lakini haikuwezekana kabisa

Mfu ni mfu na hatuna uwezo wowote iwe wa kimwili au wa kiroho kuweza kumuita na kuongea naye lolote, hii ni kwakuwa roho inapotengana na mwili hakuna tena huyo MTU bali kunatokea vitu vitatu visivyoweza kuungana tena na kutengeneza kitu kimoja. vitu hivyo ni roho mwili na nafsi, vitatu hivi ndio vinatengeneza MTU nje ya hapo kuna 'mwili wake', 'roho yake' au 'nafsi yake'

Watu wamejaribu kutoa shuhuda nyingi za kutokewa na marehemu, hili linawezekana kwasababu baada ya kifo kuna roho huwa zinawayawaya duniani, zipo tu na hizi ndizo ambazo hugeuka mizimu mizuri au mibaya

Wakati mmoja tu marehemu anaweza kusikia sauti ya mwanadamu na kuitii ni pale tu anapoandaliwa kwa safari yake ya mwisho kaburini, hasa kwenye ishu ya kumsafirisha au kumvalisha nguo

Nikiwa mtu ambaye nilidili na miili ya marehemu kwa miaka mitatu mfululizo nilikutana mara nyingi tu na hizi hali, marehemu hataki dharau ubishi au kufokewa nguo hata iwe inamtosha Siku hiyo itakataa mpaka mumbembeleza

Tuna wajuaji wengi Siku hizi wanaojifanya wametokewa na marehemu fulani na kumpa maagizo Fulani hizi kwa asilimia 90 ni story tu kwakuwa hatujakuwa na uwezo wa kuwaita au wao kututokea tu na uchafu wote huu tulionao
Nimepapenda "marehemu huwa hawataki dharau"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Viko vitatu vinavyotengeneza ID/utambulisho wa kiumbe hai/mwanadamu! Kimoja (mwili)kinaonekana viwili nafsi na roho haionekani

1. mwili ni jumba la kubeba roho/uhai
2. roho ndio inayofanya mwili uwe na uhai
3. nafsi/kujitambua ndio huleta ufahamu kwenye mwili wenye roho

Kuna wakati nafsi inakosekana lakini mwili na roho vina endelea kuwa live, tendo la kukosa fahamu hufanya mtu kukosa kujitambua kuwa yuko wapi na anafanya nini
Kwa kiingereza ni ME, MYSELF and I
Ni sawa na kusema:-
1- Mwili ni Hardware
2- Nafsi ni Software
3- Roho ni Electricity (Power)
 
Mambo hayo
Screenshot_20191222-123015.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umezungumzia kuhusu kuongea na wafu elimu iliyoshindikana duniani. Ukweli hii elimu haijashindikana, ipo! Ila ni elimu inayokutaka utoke kwenye ukawaida uliyo wa ukawaida.

Ni elimu ambayo haijikiti na mwili! Ni elimu ambayo inajikita na roho. Ni elimu ambayo ili uifikie inabidi ujikane wewe mwenyewe kwanza. Kwa sababu ulimwengu wa kuyashuhudia hayo si ulimwengu wa kimwili bali wa kiroho.

Wazee wa kale hawakuwa wakiwaita wafu bali ni viumbe vyengine vilivyokuwa na ukaribu A-Z na aliyefariki. Vile ndivyo vinavyokuja mbadala wa vile vilivyokufa na kukuaminisha kwamba ndiyo wao ila uhakika wa mambo si hao wafu ndiyo waliyokuja. Walijitambulisha kama mizimwi muda mwengine.

Uzi uliyonipa kama marejeleo hakikuwa ninachomaanisha. Ukiipata elimu ya kiriho ya inayokutaka kujikana mwenyewe utawaona na kugundua si kila aliyekufa amekufa!

Na ni wenye msaada mkubwa kwako pengine. Na pengine ndiye waliyokuwa walezi wako tangu ulivyozaliwa mpaka ulipofikia sasa pasipo wewe mwenyewe kujua.

Ni elimu iliyotoka kwenye ukawaida wa ubinadamu haieleweki kwa maelezo bali inaeleweka kwa vitendo.
 
Umezungumzia kuhusu kuongea na wafu elimu iliyoshindikana duniani. Ukweli hii elimu haijashindikana, ipo! Ila ni elimu inayokutaka utoke kwenye ukawaida uliyo wa ukawaida.

Ni elimu ambayo haijikiti na mwili! Ni elimu ambayo inajikita na roho. Ni elimu ambayo ili uifikie inabidi ujikane wewe mwenyewe kwanza. Kwa sababu ulimwengu wa kuyashuhudia hayo si ulimwengu wa kimwili bali wa kiroho.

Wazee wa kale hawakuwa wakiwaita wafu bali ni viumbe vyengine vilivyokuwa na ukaribu A-Z na aliyefariki. Vile ndivyo vinavyokuja mbadala wa vile vilivyokufa na kukuaminisha kwamba ndiyo wao ila uhakika wa mambo si hao wafu ndiyo waliyokuja. Walijitambulisha kama mizimwi muda mwengine.

Uzi uliyonipa kama marejeleo hakikuwa ninachomaanisha. Ukiipata elimu ya kiriho ya inayokutaka kujikana mwenyewe utawaona na kugundua si kila aliyekufa amekufa!

Na ni wenye msaada mkubwa kwako pengine. Na pengine ndiye waliyokuwa walezi wako tangu ulivyozaliwa mpaka ulipofikia sasa pasipo wewe mwenyewe kujua.

Ni elimu iliyotoka kwenye ukawaida wa ubinadamu haieleweki kwa maelezo bali inaeleweka kwa vitendo.
Ni elimu iliyotoka kwenye ukawaida wa ubinadamu haieleweki kwa maelezo bali inaeleweka kwa vitendo.....
Asante kwa maarifa nimekupata vizuri sana
 
Kwanza lazima tukubaliane kuwa ndoto ni vague memories ya matukio yote ya kila siku yawe ya kuwaza kunena na kutenda lakini inapotokea marehemu kakutokea ndoroni na ujumbe fulani kwako hiyo ni ndoto ya ujumbe yenye uhalisia

Binafsi babu yangu mzaa mama aliniaga, nakumbuka ilikuwa kwenye saa nane usiku hivi nikajikuta niko nyumbani kwa babu tumekaa naye kuna kitu ananianbia

Kuamka asubuhi zikaja taarifa za kifo chake na sehemu tulipokuwa tumekaa ule usiku ndipo alipozikwa
Mshana Jr Sasa Kama anakutokea kila siku inakuwaje na unapewa mjumbe mzito
 
Hii ngumu kidogo. Kma anaweza kataa nguo ina maana hubaki na mawasiliano katika ya nafsi, roho na mwili?
Hii nimeshuhudia live marehemu alikataa kuingia ndan ya jeneza!
Kisa kilipoanzia:
Muda wa kwenda kuchukua mwili umefika na jeneza lipo wakat huo marehemu amevalishwa vema.lile jeneza lililoletwa akaingizwa lakn shingo plus kichwa havikuenea
( Si Kama hawakumpima na vipimo vilifanyika)

Basi yule mtu wa mochuari akawaambia ndugu waliokuja kuchukua mwili ilibidi ku mmbembeleze kikwenu familia iwasiliane mambo yaende vema. Basi wakajipanga kwa kuvuta kumbukumbu na mtoto wa kwanza wa marehem wanapatana na marehemu akapigiwa simu na kuelezwa yaliotokea mochwar ,jaman tembea uone! Mtoto wa marehem akasema mpen simu marehem simu ikawekwa sikion ikiwa loud ( aliongea kwa kilugha chao tena Cha kumbembeleza)
Jeneza lilivokuja lingine maana walikwenda kubadili walihisi n dogo ijapo walimpima
Khe!, Marehem alitosha mpaka kupwaya na ndan kukabak kukubwa tu

Mpaka shughuli za mazishi zinamalizika walimtumia mtoto anaepatana na marehemu!.
 
Hii nimeshuhudia live marehemu alikataa kuingia ndan ya jeneza!
Kisa kilipoanzia:
Muda wa kwenda kuchukua mwili umefika na jeneza lipo wakat huo marehemu amevalishwa vema.lile jeneza lililoletwa akaingizwa lakn shingo plus kichwa havikuenea
( Si Kama hawakumpima na vipimo vilifanyika)

Basi yule mtu wa mochuari akawaambia ndugu waliokuja kuchukua mwili ilibidi ku mmbembeleze kikwenu familia iwasiliane mambo yaende vema. Basi wakajipanga kwa kuvuta kumbukumbu na mtoto wa kwanza wa marehem wanapatana na marehemu akapigiwa simu na kuelezwa yaliotokea mochwar ,jaman tembea uone! Mtoto wa marehem akasema mpen simu marehem simu ikawekwa sikion ikiwa loud ( aliongea kwa kilugha chao tena Cha kumbembeleza)
Jeneza lilivokuja lingine maana walikwenda kubadili walihisi n dogo ijapo walimpima
Khe!, Marehem alitosha mpaka kupwaya na ndan kukabak kukubwa tu

Mpaka shughuli za mazishi zinamalizika walimtumia mtoto anaepatana na marehemu!.
Hiki kisa kimenisisimua ...haya ndio tunayokutana nayo mochwari na kwenye shughuli nyingi za wafu
 
na vipi kuhusu izi habari tunazozisikia mara kwa mara, watu wanaenda kuzika marehemu anaongea anaweza akatoa kauli moja tu watu wote mkakimbia.
watu wanaweza wakawa wanaosha mwili au wanamvesha marehemu akafungua macho alafu akayafunga tena au akachezesha kiungo cha mwili either mkono au mguu.
Mshana jr hii imekaaje? mmemuwek vema marehemu Kama kumfunga mdomo lakn baada ya muda mnakuta meno yote yako nje mithili anacheka
 
Mshana jr hii imekaaje? mmemuwek vema marehemu Kama kumfunga mdomo lakn baada ya muda mnakuta meno yote yako nje mithili anacheka
Hiyo mara nyingi hutokea kwa wale marehemu wa vifo vya ghafla kama ajali au kuuliwa huku wakipambana wasife...
 
Mkuu mshana jr unaikumbuka hii, heh heh...





























Sjacheka the way nilivyocheka kwenye post za jamaa hata skumbuki mara ya mwisho nimecheka hivi ni lini aseee.

Jamaa kaniongezea UHAI leo kiasi flani mkuu dah, NI HATARI SANA.

THAT'S WHY I LOVE THIS PLACE | JF.
Hahahaha hii post jaman hahaha u made my day hahah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom