Mamndenyi
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 40,563
- 52,200
Mwaka 2016 nilifiwa na mama mzazi baada ya kumuuguza sana nyumbani na pale kcmc, nilikuwa karibu sana naye.
Ikatokea jioni moja dada mkubwa akaja kunipokea ili akesha pale, japo mchana nilishinda nampaka dawa maana mwili sehemu sehemu zilianza kuungua.
Muda wote nikiwa naye akiwa ICU (tulipewa kibali maalum cha kukaa mle ndani ICU ) nilikuwa namwimbia nyimbo za kanisani na kumsomea neno la Mungu. Japo hasemi ila nilikuwa nasogea karibu na sikio au moyo wake nakumwambia mama uende na neno la Mungu, nilijua hawezi pona tena.
Muda kidogo niliambiwa mama hayupo tena.
Siku ya kufuata mwili nilikuwa mbele sikutaka sikose kuona process yote .
Walipomtoa kwenye yale makabati aligeuza shingo nikawa natazamana naye uso kwa uso.
Mshana Jr mama alinichekea, naapa alicheka na ile tabasamu iliendelea kosa nililofanya nikamshtua mdogo wangu nikamwambia ona mama hajafa mbona ananichekea, yaani pale pale akabadilika na tabasamu ikaondoka.
Kweli maiti inaongea.
Ikatokea jioni moja dada mkubwa akaja kunipokea ili akesha pale, japo mchana nilishinda nampaka dawa maana mwili sehemu sehemu zilianza kuungua.
Muda wote nikiwa naye akiwa ICU (tulipewa kibali maalum cha kukaa mle ndani ICU ) nilikuwa namwimbia nyimbo za kanisani na kumsomea neno la Mungu. Japo hasemi ila nilikuwa nasogea karibu na sikio au moyo wake nakumwambia mama uende na neno la Mungu, nilijua hawezi pona tena.
Muda kidogo niliambiwa mama hayupo tena.
Siku ya kufuata mwili nilikuwa mbele sikutaka sikose kuona process yote .
Walipomtoa kwenye yale makabati aligeuza shingo nikawa natazamana naye uso kwa uso.
Mshana Jr mama alinichekea, naapa alicheka na ile tabasamu iliendelea kosa nililofanya nikamshtua mdogo wangu nikamwambia ona mama hajafa mbona ananichekea, yaani pale pale akabadilika na tabasamu ikaondoka.
Kweli maiti inaongea.