Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

Mwaka 2016 nilifiwa na mama mzazi baada ya kumuuguza sana nyumbani na pale kcmc, nilikuwa karibu sana naye.

Ikatokea jioni moja dada mkubwa akaja kunipokea ili akesha pale, japo mchana nilishinda nampaka dawa maana mwili sehemu sehemu zilianza kuungua.

Muda wote nikiwa naye akiwa ICU (tulipewa kibali maalum cha kukaa mle ndani ICU ) nilikuwa namwimbia nyimbo za kanisani na kumsomea neno la Mungu. Japo hasemi ila nilikuwa nasogea karibu na sikio au moyo wake nakumwambia mama uende na neno la Mungu, nilijua hawezi pona tena.

Muda kidogo niliambiwa mama hayupo tena.

Siku ya kufuata mwili nilikuwa mbele sikutaka sikose kuona process yote .

Walipomtoa kwenye yale makabati aligeuza shingo nikawa natazamana naye uso kwa uso.

Mshana Jr mama alinichekea, naapa alicheka na ile tabasamu iliendelea kosa nililofanya nikamshtua mdogo wangu nikamwambia ona mama hajafa mbona ananichekea, yaani pale pale akabadilika na tabasamu ikaondoka.

Kweli maiti inaongea.
 
Mwaka 2016 nilifiwa na mama mzazi baada ya kumuuguza sana nyumbani na pale kcmc, nilikuwa karibu sana naye.

Ikatokea jioni moja dada mkubwa akaja kunipokea ili akesha pale, japo mchana nilishinda nampaka dawa maana mwili sehemu sehemu zilianza kuungua.

Muda wote nikiwa naye akiwa ICU (tulipewa kibali maalum cha kukaa mle ndani ICU ) nilikuwa namwimbia nyimbo za kanisani na kumsomea neno la Mungu. Japo hasemi ila nilikuwa nasogea karibu na sikio au moyo wake nakumwambia mama uende na neno la Mungu, nilijua hawezi pona tena.

Muda kidogo niliambiwa mama hayupo tena.

Siku ya kufuata mwili nilikuwa mbele sikutaka sikose kuona process yote .

Walipomtoa kwenye yale makabati aligeuza shingo nikawa natazamana naye uso kwa uso.

Mshana Jr mama alinichekea, naapa alicheka na ile tabasamu iliendelea kosa nililofanya nikamshtua mdogo wangu nikamwambia ona mama hajafa mbona ananichekea, yaani pale pale akabadilika na tabasamu ikaondoka.

Kweli maiti inaongea.
Mtani lile tabasamu lilikuwa lako na si la mtu mwingine yeyote
 
Iko hivi sikuwa anakataa live bali wakati wa kumvisha kama ni koti shati au hata suruali kuna kiungo kimoja hukakamaa kwa mfano kama ni mkono haunyanyuki au haukunjiki, kama ni mguu unajipinda au unakuwa mzito kunyanyua
Hivi vitu vinafanyika kwa namna ya ajabu na ya kipekee kabisa

Vilevile kuna kukosea vifungo au zipu kujichanganya! Yani mnaanza kufunga kifungo cha kwanza vizuri kabisa mkifika mwisho aidha vimepishana au mmeruka matundu, tulishawahi kukosea vifungo Mara SABA
Ni mpaka nilipotumia elimu niliyojifunza kuongea na marehemu kwa upole na kwa kumbembeleza ndio mambo yakawa sawa, na pia ndani ya chumba husika kama yupo mtu alikuwa na ugomvi na marehemu hakuna kitakachokwenda sawa hapo mpaka yule mtu atoke
Hizi zote ni hisia za mtu mhusika au wahusika katika tendo la kumwandaa marehemu. Hakuna uhalisia wowote hizi zote ni hysteria tu au woga walionao watu husika. Biblia ina sema msihangaike na hoa waliolala katima umauti kwani hakuna chochote wanachoweza kukusaidia wala sisi kuwasaidia huyo alielala katika umaiti.
 
Hizi zote ni hisia za mtu mhusika au wahusika katika tendo la kumwandaa marehemu. Hakuna uhalisia wowote hizi zote ni hysteria tu au woga walionao watu husika. Biblia ina sema msihangaike na hoa waliolala katima umauti kwani hakuna chochote wanachoweza kukusaidia wala sisi kuwasaidia huyo alielala katika umaiti.
Haya sawa.. Asante kwa kushiriki mjadala
 
Huyu Jamaa vijimambo vyake huwa ni vifupi2 visivyoeleweka ingawa wasiyojua mambo haya humsifia sana! Eleza Jambo kwa ufasaha na mifano ili ueleweke, ujue kuna wataalam humu wanakuangalia tu!
 
Mshana jr.
Umetoa wapi mawazo haya leo? Au babu yako kakutembelea? Siku ya arusi yangu, bibi mzaa baba aliyekuwa amefariki miaka kama 12 hivi iliyokuwa imepita alinijia usiku. Sisemi ilikuwa ndoto kwani nilikuwa sija lala na kibatari kilikuwa kinawaka. Akasimama karibu na kitanda changu akanikumbusha alivyokuwa ananipenda mjukuu wake.
Akasema; Nasikia unaoa, ninataka nitoe mchango wangu. Nitakupa weye mchango wangu kesho. Aka[otea, nilifadhaika kidogo ila kwa kuwa hakuna mtu mwingine aliyesikia sauti ya bibi nkaogopa kusema wasinicheke.



Je huo haukuwa mchango wa bibi yangu? Nafsi bado zipo hapa ila roho imerudi kwa mwenyewe ka mwili ulivyo rudi kuwa mavumbi
Ghafula pale chini sakafuni nikaona noti ya shs 10. Enzi hizo za '70 hiyo ilikuwa hela kubwa sana. Kama laki+ leo. elfu 10 je hii noti tayari ilikuwepo?
 
Ghafula pale chini sakafuni nikaona noti ya shs 10. Enzi hizo za '70 hiyo ilikuwa hela kubwa sana. Kama laki+ leo. elfu 10 je hii noti tayari ilikuwepo?
Itakuwa ni typing error... Most likely alitaka kusema noti ya shilingi mia moja
 
Nikiwa mtu ambaye nilidili na miili ya marehemu kwa miaka mitatu mfululizo nilikutana mara nyingi tu na hizi hali, marehemu hataki dharau ubishi au kufokewa nguo hata iwe inamtosha Siku hiyo itakataa mpaka mumbembeleza
Hii niliisha ishuhudia- jeneza lilkataa kuingia katika gari mpaka wakagundua kuwa marehemu hakupendezwa na baadhi ya mambo waliyopanga ndipo likaingia
 
Dunia imekuwa kama kijiji kutokana na uwezo mkubwa aliounyesha mwanadamu wa kugundua hata ambavyo vilifikirika kwamba haviwezekani

Elimu na ufahamu kuhusu mwili wa mwanadamu kuanzia kuumbwa tumboni kuzaliwa hadi kufa umetafitiwa na kunyumbulishwa kwa mapana yake na wengi wamepata elimu ya juu kabisa PhD kwenye hili eneo, lakini wakashishindwa kitu kimoja tuu!!! Uwezo wa kumuita marehemu na kuongea naye

Zamani kabla ya dini za kigeni hazijaja Africa tulikuwa kwa kiasi fulani tuna uwezo wa kuwaita marehemu kwa njia ya matambiko na kuwaomba hili au lile, lakini ikumbukwe kwamba hawakuja live bali dalili na ishara kadha zilionyesha uwepo wao na kukubali au kukataa ombi husika

Tumekuwa tunaondokewa na wapendwa wetu na watu tunaowahitaji mno katika maisha yetu, tumekuwa na vipindi vigumu kabisa ambapo tunawahamu na kuwahitaji japo wajitokeze kwa dakika chache tu lakini haikuwezekana kabisa

Mfu ni mfu na hatuna uwezo wowote iwe wa kimwili au wa kiroho kuweza kumuita na kuongea naye lolote, hii ni kwakuwa roho inapotengana na mwili hakuna tena huyo MTU bali kunatokea vitu vitatu visivyoweza kuungana tena na kutengeneza kitu kimoja. vitu hivyo ni roho mwili na nafsi, vitatu hivi ndio vinatengeneza MTU nje ya hapo kuna 'mwili wake', 'roho yake' au 'nafsi yake'

Watu wamejaribu kutoa shuhuda nyingi za kutokewa na marehemu, hili linawezekana kwasababu baada ya kifo kuna roho huwa zinawayawaya duniani, zipo tu na hizi ndizo ambazo hugeuka mizimu mizuri au mibaya

Wakati mmoja tu marehemu anaweza kusikia sauti ya mwanadamu na kuitii ni pale tu anapoandaliwa kwa safari yake ya mwisho kaburini, hasa kwenye ishu ya kumsafirisha au kumvalisha nguo

Nikiwa mtu ambaye nilidili na miili ya marehemu kwa miaka mitatu mfululizo nilikutana mara nyingi tu na hizi hali, marehemu hataki dharau ubishi au kufokewa nguo hata iwe inamtosha Siku hiyo itakataa mpaka mumbembeleza

Tuna wajuaji wengi Siku hizi wanaojifanya wametokewa na marehemu fulani na kumpa maagizo Fulani hizi kwa asilimia 90 ni story tu kwakuwa hatujakuwa na uwezo wa kuwaita au wao kututokea tu na uchafu wote huu tulionao
Inawezekana.Tabu inakuja hapa,hiyo process mnufaika ni nani?
 
Kwa uelewa wangu nakataa kabisa. Ni jambo linalowezekana kwa 100% kuongea na wafu. Nasio tu kuongea nao ndotoni hata moja kwa moja kanakwamba wapo hai.


Nikusaidie kitu Kaka. Hii sio elimu tu hapana ni kipawa ambacho kinakuwa connected kiuteule, nina ushahidi wa watu na tafiti kadhaa wenye kipawa chakuongea na wafu.


Pia inaweza kuwa elimu sababu kuna mtu aliwahi kuniambia nikitaka anaweza kunipa elimu na maarifa yote juu ya kuwa connected na wafu. So Duniani kuna maarifa ya Siri sana na maarifa haya yapo kwa watu wachache sana.
 
Kwa uelewa wangu nakataa kabisa. Ni jambo linalowezekana kwa 100% kuongea na wafu. Nasio tu kuongea nao ndotoni hata moja kwa moja kanakwamba wapo hai.


Nikusaidie kitu Kaka. Hii sio elimu tu hapana ni kipawa ambacho kinakuwa connected kiuteule, nina ushahidi wa watu na tafiti kadhaa wenye kipawa chakuongea na wafu.


Pia inaweza kuwa elimu sababu kuna mtu aliwahi kuniambia nikitaka anaweza kunipa elimu na maarifa yote juu ya kuwa connected na wafu. So Duniani kuna maarifa ya Siri sana na maarifa haya yapo kwa watu wachache sana.
Pia inaweza kuwa elimu sababu kuna mtu aliwahi kuniambia nikitaka anaweza kunipa elimu na maarifa yote juu ya kuwa connected na wafu. So Duniani kuna maarifa ya Siri sana na maarifa haya yapo kwa watu wachache sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom