Uwekezaji Kwenye Mafuta na Gesi: Haraka ya nini?

ZeMarcopolo

Platinum Member
May 11, 2008
14,017
7,220
Nauliza haraka ya nini? Mboni tuko mbioni?

Kuyafukua madini, mwaka huu si mwakani?

Ukifuatilia mijadala inayozunguka uwekezaji kwenye mafuta na gesi, utagundua kuwa wapo watanzania (tena wasomi) ambao hawajatambua kuwa rasilimali tunayoizungumzia ina uwezo wa kubadilisha kabisa hali ya maisha ya watanzania.

Rasilimali hii ni Game Changer...

Kama kwenye mpira wa miguu, ni sawa na kupewa penalt dakika ya 90.

Sasa hivi tumepewa penalt, halafu tumeshaonyesha dalili za kumpa penalt hiyo beki apige. Striker wetu tunasema akae pembeni! Hili ni kosa. Yatatukuta kama Yanga walivyofanywa na David Mwakalebela...

Hoja kubwa inayozunguzwa ni kwamba watanzania hawana uwezo wa kuwekeza kwenye sekta hii.

Tuko watanzania zaidi ya milioni 45. Watu milioni 45 tunashindwa vipi kuwekeza kwenye uchimbaji mafuta na gesi?

Jibu ni kwamba hatushindwi. Ila maamuzi ya haraka haraka yanafanya ionekane kama vile tunashindwa.

Kuna hoja zinaongelewa kama vile tunalazimika kuchimba mafuta mwaka huu, mara moja. Kama vile mafuta yatakimbia.

Mafuta yalikuwepo, yapo na yataendelea kuwepo. Tunachohitaji sisi ni mkakati wa jinsi ya kuyavuna kwa faida zaidi.

Ingefaa tuwe na mkakati wa miaka kumi (10) wa kujijengea uwezo wa kuchimba mafuta na gesi.

Katika kipindi hicho cha miaka 10 tupeleke vijana wakasome ujuzi wa kiufundi, kisheria, kiuchumi, kibiashara na kimazingira wa uchimbaji mafuta na gesi. Vijana 60 katika ufundi na wengine 10 katika fani nyingine, jumla vijana 100. Vijana hawa wangesoma kwa wastani wa miaka mitatu degree ya kwanza.

Baada ya hapo, tukawapeleka vijana hawa miaka miwili internship kwenye makampuni ya uchimbaji mafuta na gesi katika fani walizosomea. Paid intenship.

Baada ya miaka hiyo miwili tukawapeleka kusoma masters degree katika fani zitakazowekewa malengo maalum. Masters itakuwa kwa wastani wa muda wa miaka miwili.

hapo itakuwa imeisha miaka saba (7). Tutakuwa na wataalam wenye uelewa wa kutosha kuhusu uchimbaji mafuta na gesi, tuliowaandaa kwa malengo maalum. Wapo ambao hawatamaliza masomo lakini iwapo uchaguzi utafanyika vizuri, ambao hawatamaliza watakuwa wachache sana.

Wataalam hawa baada ya kumaliza masters degree warudi nyumbani kwa ajili ya kuanzisha masomo ya elimu ya uchimbaji mafuta na gesi kwa ngazi ya diploma na degree. At the same time watumiwe katika uwekezaji huu.

Je, pesa zitatoka wapi?

Miaka kumi inatosha kubuni mfuko wa kukusanya pesa za mtaji wa kuwekeza kwenye uchimbaji toka kwa wananchi.

Ili nchi za Africa ziendelee, kwanza kabisa inabidi zitambue kuwa haziwezi kufanikiwa iwapo zitakuwa zinaiga jinsi nchi zilizoendelea zinavyotatua masuala yao. Nchi zilizoendelea zina mifumo inayoziwezesha kutabili matokeo ya maamuzi wanayofanya. Sisi mifumo hiyo hatuna. Maamuzi yetu mengi ni trial and error.

Kwahiyo, inabidi tubuni utaratibu ambao uko customised kulingana na mazingira yetu.

Serikali inaweza kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa ukusanyaji mitaji. Kwa kipindi cha miaka saba nchi ifanye kazi ya kukusanya mitaji tu na kuhifandhi fedha hizo. Ukiangalia pesa zinazochangwa kwenye harusi, utakuwa shahidi wa kuwa uwezo tunao - kinachokosekana ni organisation tu. Ndio maana hata kwenye familia inayofanya harusi ya shilingi milioni tano si ajabu kukuta kuna mtoto anayekosa ada ya shilingi laki mbili!

Wakati haya yakifanyika serikali inaendelea na uboreshaji wa TPDC kimfumo, kisera na kimiundombinu ili iwe tayari kwa kazi hii. Hii ni pamoja na kuanzicha chuo cha TPDC chenye lengo la kuzalisha wataalam wa ngazi mbalimbali za ujuzi katika sekta ya mafuta na gesi.

Kwa utaratibu huu, katika kipindi cha miaka saba nchi inakuwa na wataalam pamoja na pesa na TPDC inakuwa standby. Inabaki miaka mitatu ya wataalam hao kushirikiana na wale wachache ambao tayari wapo na watendaji wa serikali kutengeneza utaratibu rasmi wa uchimbaji kutokana na utaalam waliojifunza. Pale tunapopungukiwa tunaweza kuajiri washauri wenye uzoefu zaidi, lakini wanakuja kama waajiriwa wanaosikiliza mahitaji ya mwajiri ambaye ni sisi.

Haraka ya nini? Mbona kama kuna kitu kinakimbiliwa kabla jambo fulani halijatokea? Je, ni nini future ya miradi hii baada ya jambo hilo kutokea? - kwa sababu ni lazima litokee.

Nchi yetu imejiendesha zaidi ya miaka 50 bila mafuta na gesi, inaweza kuvumilia miaka mingine kumi bila mafuta na gesi wakati tukijiandaa.

Tufikirie vizazi vijavyo. Hakuna mwingine wa kuwaandalia mazingira bora watanzania wa kesho ila ni sisi.

Kupanga ni kuchagua...
 
Hatuhitaji mikakati, malengo, mipango, elimu, semina, mifuko, kapu la pamoja n.k n.k tunachokitaka ni faida ya rasilimali zetu!

Kuna shida gani kuwaachia yeyote achimbe gesi kwa masharti ya kutuachia 50% ambayo asilimia 30% itaenda afya, 30% elimu na 40% kwenye kilimo na ufugaji?

Ndio maana hatuwataki nyie vikongwe wa CCM.
 
ZeMarcopolo tatizo wala si watanzania wa kawaida bali viongozi wetu wanaoabudu Rushwa na kujilimbikizia mali. Hakuna jingine. Tunachowasihi mlioko kwenye kapu la kijani mtusaidia kupigana vita ya raslimali.

Hope u-mzalendo na mtaifa pia. Yaani UTAIFA kwanza Chama baadaye.
 
Hatuhitaji mikakati, malengo, mipango, elimu, semina, mifuko, kapu la pamoja n.k n.k tunachokitaka ni faida ya rasilimali zetu!

Kuna shida gani kuwaachia yeyote achimbe gesi kwa masharti ya kutuachia 50% ambayo asilimia 30% itaenda afya, 30% elimu na 40% kwenye kilimo na ufugaji?

Ndio maana hatuwataki nyie vikongwe wa CCM.

Kumbuka mambo mawili:
1. Yule anayekuja kuchimba na yeye pia ana strategies zake za kumaximise profit ambazo zinaweza kutuumiza. Sisi hatuna hata wataalam/uwezo wa kutumabia kuwa gharama za uwekezaji tunazotajiwa ni sahihi. Ndio kwanza tuko katika hatua ya kujenga uwezo wa kuhakiki kiasi cha mafuta na gesi kitakachovunwa na thamani yake at the same tunakubali kulipa gharama za uwekezaji ambazo hatujazihakiki!

2. Akishakuja anakuwa na luba. Hachomoki huyo. Mafuta yetu yatalipa gharama zake zote za uwekezaji, halafu ataendelea kuwa anavuna mafuta yetu MILELE au mpaka yakauke.
 
We mtu, ZeMarcoplo, kumbe kuna wakati mwingine huwa unaongea kama mwanaume? Lakini mara nyingi huwa unaniudhi pale unapoweka akili yako rehani na kuongea kama msichana! Kwa mara ya kwanza ninaku-support!!
 
Niliwahi kukutana na geologist mmoja nikamuuliza hili swali. Alinipa jibu lenye hoja nyepesi sana kuwa "Teknolojia inabadilika kwa haraka sana miaka hii. Pengine miaka kadhaa idhayo itagunduliwa teknolojia mpya ya kugenerate energy na power ambayo inatumia vitu rahisi zaidi ya mafuta, uranium na kadhalika, tukajiluta tumebaki na mimafuta, miuranium na migesi yetu huko ardhini bila cha kuifanyia"
Nikamuuliza biashara yeyote ni about risking. Je, kwa hili hapa tunaogopa kurisk? Majibu aliyonipa hata siyakumbuki, kwani yalikuwa bla bla...

Back to topic... ZeMarcopolo, asikudanganye mtu kwa level ya ufisadi tuliyo nayo hili linawezekana, never. Swala kama hili linahitaji uaminifu na usafi wa hali ya juu kulifanikisha.

Kwa mfano, Kwanza: raisi angetangaza leo kuwa tunapeleka vijana 20 kwenda kusoma kama ulivyosema... nakuhakikishia, 18 kati ya hao watakuwa watoto, ndugu au jamaa wa mawaziri, makatibu wakuu na makamishna ambao majority hawatakuwa na uwezo kiakili kwenda kusomea hayo mambo.
Pili: Tuliambiwa kuwa gharama ya kuchimba kisima kimoja ni $100m. Ok, tuassume kwamba hiyo ndiyo genuine figure. Ukiwaambia leo TPDC wachimbe mafuta, hakyanani gharama za kuchimba kisima kimoja zitakuwa sio chini ya $500m. Hivi mzee umesahau tundu moja la choo kujengwa kwa m30? Au lori moja la mchanga kugharimu laki 5? au kitasa cha mlango wa ofisi ya mwalimu mkuu kilichonunuliwa kwa laki 7 na ngapi sijui.

So, what should be done? Tukubali kuchimba kwa hasara 20% ya mafuta/gesi tuliyo nayo then hiyo itusaidie kufanya capacity building ya kufaidi hiyo 80% iliyobali. Nimesema hivi nikijua kabisa Mkapa, na Yona walituambia hivi hivi wakati ule wa Bulyanhulu, but hadi leo, more than 80 ya yale madini yameshachimbwa and yet hatujajenga hiyo capacity zaidi ya watu kujenga maghorofa na vitambi

So.... tumuombe tu Mungu...
 
Last edited by a moderator:
Niliwahi kukutana na geologist mmoja nikamuuliza hili swali. Alinipa jibu lenye hoja nyepesi sana kuwa "Teknolojia inabadilika kwa haraka sana miaka hii. Pengine miaka kadhaa idhayo itagunduliwa teknolojia mpya ya kugenerate energy na power ambayo inatumia vitu rahisi zaidi ya mafuta, uranium na kadhalika, tukajiluta tumebaki na mimafuta, miuranium na migesi yetu huko ardhini bila cha kuifanyia"
Nikamuuliza biashara yeyote ni about risking. Je, kwa hili hapa tunaogopa kurisk? Majibu aliyonipa hata siyakumbuki, kwani yalikuwa bla bla...

Back to topic... ZeMarcopolo, asikudanganye mtu kwa level ya ufisadi tuliyo nayo hili linawezekana, never. Swala kama hili linahitaji uaminifu na usafi wa hali ya juu kulifanikisha.

Kwa mfano, Kwanza: raisi angetangaza leo kuwa tunapeleka vijana 20 kwenda kusoma kama ulivyosema... nakuhakikishia, 18 kati ya hao watakuwa watoto, ndugu au jamaa wa mawaziri, makatibu wakuu na makamishna ambao majority hawatakuwa na uwezo kiakili kwenda kusomea hayo mambo.
Pili: Tuliambiwa kuwa gharama ya kuchimba kisima kimoja ni $100m. Ok, tuassume kwamba hiyo ndiyo genuine figure. Ukiwaambia leo TPDC wachimbe mafuta, hakyanani gharama za kuchimba kisima kimoja zitakuwa sio chini ya $500m. Hivi mzee umesahau tundu moja la choo kujengwa kwa m30? Au lori moja la mchanga kugharimu laki 5? au kitasa cha mlango wa ofisi ya mwalimu mkuu kilichonunuliwa kwa laki 7 na ngapi sijui.

So, what should be done? Tukubali kuchimba kwa hasara 20% ya mafuta/gesi tuliyo nayo then hiyo itusaidie kufanya capacity building ya kufaidi hiyo 80% iliyobali. Nimesema hivi nikijua kabisa Mkapa, na Yona walituambia hivi hivi wakati ule wa Bulyanhulu, but hadi leo, more than 80 ya yale madini yameshachimbwa and yet hatujajenga hiyo capacity zaidi ya watu kujenga maghorofa na vitambi

So.... tumuombe tu Mungu...

Jibu alipitia geologist ni la kichekibobu. Halina ukweli wala uhalisia.

Taifa lazima liwe na mikalati endelevu la kuhakikisha vizazi vijavyo vinakuta mazingira yanayofaa kwa maisha.

Katika swala hili la gesi na mafuta, vizazi vijavyo hatujavifikiria.
 
Last edited by a moderator:
marcopollo naomba unisaidie kuulizia hapo lumumba zile trilioni karibu mbili za stimulate package zilipewa makampuni gani?na faida yake ni ipi/na je haziwezi kuchimba hata kisima kimoja cha gesi?
 
marcopollo naomba unisaidie kuulizia hapo lumumba zile trilioni karibu mbili za stimulate package zilipewa makampuni gani?na faida yake ni ipi/na je haziwezi kuchimba hata kisima kimoja cha gesi?

Sijafahamu pesa gani unazungumzia.

Pia sina access na Lumumba.
 
Nauliza haraka ya nini? Mboni tuko mbioni?

Kuyafukua madini, mwaka huu si mwakani?

Ukifuatilia mijadala inayozunguka uwekezaji kwenye mafuta na gesi, utagundua kuwa wapo watanzania (tena wasomi) ambao hawajatambua kuwa rasilimali tunayoizungumzia ina uwezo wa kubadilisha kabisa hali ya maisha ya watanzania.

Rasilimali hii ni Game Changer...

Kama kwenye mpira wa miguu, ni sawa na kupewa penalt dakika ya 90.

Sasa hivi tumepewa penalt, halafu tumeshaonyesha dalili za kumpa penalt hiyo beki apige. Striker wetu tunasema akae pembeni! Hili ni kosa. Yatatukuta kama Yanga walivyofanywa na David Mwakalebela...

Hoja kubwa inayozunguzwa ni kwamba watanzania hawana uwezo wa kuwekeza kwenye sekta hii.

Tuko watanzania zaidi ya milioni 45. Watu milioni 45 tunashindwa vipi kuwekeza kwenye uchimbaji mafuta na gesi?

Jibu ni kwamba hatushindwi. Ila maamuzi ya haraka haraka yanafanya ionekane kama vile tunashindwa.

Kuna hoja zinaongelewa kama vile tunalazimika kuchimba mafuta mwaka huu, mara moja. Kama vile mafuta yatakimbia.

Mafuta yalikuwepo, yapo na yataendelea kuwepo. Tunachohitaji sisi ni mkakati wa jinsi ya kuyavuna kwa faida zaidi.

Ingefaa tuwe na mkakati wa miaka kumi (10) wa kujijengea uwezo wa kuchimba mafuta na gesi.

Katika kipindi hicho cha miaka 10 tupeleke vijana wakasome ujuzi wa kiufundi, kisheria, kiuchumi, kibiashara na kimazingira wa uchimbaji mafuta na gesi. Vijana 60 katika ufundi na wengine 10 katika fani nyingine, jumla vijana 100. Vijana hawa wangesoma kwa wastani wa miaka mitatu degree ya kwanza.

Baada ya hapo, tukawapeleka vijana hawa miaka miwili internship kwenye makampuni ya uchimbaji mafuta na gesi katika fani walizosomea. Paid intenship.

Baada ya miaka hiyo miwili tukawapeleka kusoma masters degree katika fani zitakazowekewa malengo maalum. Masters itakuwa kwa wastani wa muda wa miaka miwili.

hapo itakuwa imeisha miaka saba (7). Tutakuwa na wataalam wenye uelewa wa kutosha kuhusu uchimbaji mafuta na gesi, tuliowaandaa kwa malengo maalum. Wapo ambao hawatamaliza masomo lakini iwapo uchaguzi utafanyika vizuri, ambao hawatamaliza watakuwa wachache sana.

Wataalam hawa baada ya kumaliza masters degree warudi nyumbani kwa ajili ya kuanzisha masomo ya elimu ya uchimbaji mafuta na gesi kwa ngazi ya diploma na degree. At the same time watumiwe katika uwekezaji huu.

Je, pesa zitatoka wapi?

Miaka kumi inatosha kubuni mfuko wa kukusanya pesa za mtaji wa kuwekeza kwenye uchimbaji toka kwa wananchi.

Ili nchi za Africa ziendelee, kwanza kabisa inabidi zitambue kuwa haziwezi kufanikiwa iwapo zitakuwa zinaiga jinsi nchi zilizoendelea zinavyotatua masuala yao. Nchi zilizoendelea zina mifumo inayoziwezesha kutabili matokeo ya maamuzi wanayofanya. Sisi mifumo hiyo hatuna. Maamuzi yetu mengi ni trial and error.

Kwahiyo, inabidi tubuni utaratibu ambao uko customised kulingana na mazingira yetu.

Serikali inaweza kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa ukusanyaji mitaji. Kwa kipindi cha miaka saba nchi ifanye kazi ya kukusanya mitaji tu na kuhifandhi fedha hizo. Ukiangalia pesa zinazochangwa kwenye harusi, utakuwa shahidi wa kuwa uwezo tunao - kinachokosekana ni organisation tu. Ndio maana hata kwenye familia inayofanya harusi ya shilingi milioni tano si ajabu kukuta kuna mtoto anayekosa ada ya shilingi laki mbili!

Wakati haya yakifanyika serikali inaendelea na uboreshaji wa TPDC kimfumo, kisera na kimiundombinu ili iwe tayari kwa kazi hii. Hii ni pamoja na kuanzicha chuo cha TPDC chenye lengo la kuzalisha wataalam wa ngazi mbalimbali za ujuzi katika sekta ya mafuta na gesi.

Kwa utaratibu huu, katika kipindi cha miaka saba nchi inakuwa na wataalam pamoja na pesa na TPDC inakuwa standby. Inabaki miaka mitatu ya wataalam hao kushirikiana na wale wachache ambao tayari wapo na watendaji wa serikali kutengeneza utaratibu rasmi wa uchimbaji kutokana na utaalam waliojifunza. Pale tunapopungukiwa tunaweza kuajiri washauri wenye uzoefu zaidi, lakini wanakuja kama waajiriwa wanaosikiliza mahitaji ya mwajiri ambaye ni sisi.

Haraka ya nini? Mbona kama kuna kitu kinakimbiliwa kabla jambo fulani halijatokea? Je, ni nini future ya miradi hii baada ya jambo hilo kutokea? - kwa sababu ni lazima litokee.

Nchi yetu imejiendesha zaidi ya miaka 50 bila mafuta na gesi, inaweza kuvumilia miaka mingine kumi bila mafuta na gesi wakati tukijiandaa.

Tufikirie vizazi vijavyo. Hakuna mwingine wa kuwaandalia mazingira bora watanzania wa kesho ila ni sisi.

Kupanga ni kuchagua...
Mtoa maada kuna vitu labda hufahamu, hatuhitaji utaalamu a.k.a elimu kwa sababu tuna mali, angalia waarabu je walienda kusomea mafuta? we are rich all we need ni strategies, kila kitu kinawezekana , tungeweza kkusanya mitaji via DSE, Tuka hire expertiese! ect!
 
Mtoa maada kuna vitu labda hufahamu, hatuhitaji utaalamu a.k.a elimu kwa sababu tuna mali, angalia waarabu je walienda kusomea mafuta? we are rich all we need ni strategies, kila kitu kinawezekana , tungeweza kkusanya mitaji via DSE, Tuka hire expertiese! ect!

Ukitegemea sana watu kutoka nje matokeo yake ni kupigwa mchanga wa macho...
 
ZeMarcopolo tuna haraka kugawa maeneo hayo ya visima vya gesi na mafuta kwa kuwa watawala wetu hawataki kupoteza nafasi hii adimu ya kujilimbikizia mali na wanataka wakimaliza ngwe yao wajikute washatengeneza mfumo ambao utawahakikishia kuendeela kula kwa miaka kadhaa ijayo
Tuna haraka kwa kuwa washagawiwa chao na hawataki kuwaangusha wale waliowapa hicho chao wajikute hawajawagawia kile walichowaahidi
Shangaa uharaka huo wakati bado hatujajitengeneza huku nyumbani kujua kama nyumba ni safi wageni wanaweza kuja na kuingia kwa maana ya sera na sheria ambazo zinaweza kutupa mwanga ni asilimia ngapi na namna mwananchi wa kawaida atakavyofaidika kwenye uwekezaji huo
 
Last edited by a moderator:
Nauliza haraka ya nini? Mboni tuko mbioni?

Kuyafukua madini, mwaka huu si mwakani?

Ukifuatilia mijadala inayozunguka uwekezaji kwenye mafuta na gesi, utagundua kuwa wapo watanzania (tena wasomi) ambao hawajatambua kuwa rasilimali tunayoizungumzia ina uwezo wa kubadilisha kabisa hali ya maisha ya watanzania.

Rasilimali hii ni Game Changer...

Kama kwenye mpira wa miguu, ni sawa na kupewa penalt dakika ya 90.

Sasa hivi tumepewa penalt, halafu tumeshaonyesha dalili za kumpa penalt hiyo beki apige. Striker wetu tunasema akae pembeni! Hili ni kosa. Yatatukuta kama Yanga walivyofanywa na David Mwakalebela...

Hoja kubwa inayozunguzwa ni kwamba watanzania hawana uwezo wa kuwekeza kwenye sekta hii.

Tuko watanzania zaidi ya milioni 45. Watu milioni 45 tunashindwa vipi kuwekeza kwenye uchimbaji mafuta na gesi?

Jibu ni kwamba hatushindwi. Ila maamuzi ya haraka haraka yanafanya ionekane kama vile tunashindwa.

Kuna hoja zinaongelewa kama vile tunalazimika kuchimba mafuta mwaka huu, mara moja. Kama vile mafuta yatakimbia.

Mafuta yalikuwepo, yapo na yataendelea kuwepo. Tunachohitaji sisi ni mkakati wa jinsi ya kuyavuna kwa faida zaidi.

Ingefaa tuwe na mkakati wa miaka kumi (10) wa kujijengea uwezo wa kuchimba mafuta na gesi.

Katika kipindi hicho cha miaka 10 tupeleke vijana wakasome ujuzi wa kiufundi, kisheria, kiuchumi, kibiashara na kimazingira wa uchimbaji mafuta na gesi. Vijana 60 katika ufundi na wengine 10 katika fani nyingine, jumla vijana 100. Vijana hawa wangesoma kwa wastani wa miaka mitatu degree ya kwanza.

Baada ya hapo, tukawapeleka vijana hawa miaka miwili internship kwenye makampuni ya uchimbaji mafuta na gesi katika fani walizosomea. Paid intenship.

Baada ya miaka hiyo miwili tukawapeleka kusoma masters degree katika fani zitakazowekewa malengo maalum. Masters itakuwa kwa wastani wa muda wa miaka miwili.

hapo itakuwa imeisha miaka saba (7). Tutakuwa na wataalam wenye uelewa wa kutosha kuhusu uchimbaji mafuta na gesi, tuliowaandaa kwa malengo maalum. Wapo ambao hawatamaliza masomo lakini iwapo uchaguzi utafanyika vizuri, ambao hawatamaliza watakuwa wachache sana.

Wataalam hawa baada ya kumaliza masters degree warudi nyumbani kwa ajili ya kuanzisha masomo ya elimu ya uchimbaji mafuta na gesi kwa ngazi ya diploma na degree. At the same time watumiwe katika uwekezaji huu.

Je, pesa zitatoka wapi?

Miaka kumi inatosha kubuni mfuko wa kukusanya pesa za mtaji wa kuwekeza kwenye uchimbaji toka kwa wananchi.

Ili nchi za Africa ziendelee, kwanza kabisa inabidi zitambue kuwa haziwezi kufanikiwa iwapo zitakuwa zinaiga jinsi nchi zilizoendelea zinavyotatua masuala yao. Nchi zilizoendelea zina mifumo inayoziwezesha kutabili matokeo ya maamuzi wanayofanya. Sisi mifumo hiyo hatuna. Maamuzi yetu mengi ni trial and error.

Kwahiyo, inabidi tubuni utaratibu ambao uko customised kulingana na mazingira yetu.

Serikali inaweza kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa ukusanyaji mitaji. Kwa kipindi cha miaka saba nchi ifanye kazi ya kukusanya mitaji tu na kuhifandhi fedha hizo. Ukiangalia pesa zinazochangwa kwenye harusi, utakuwa shahidi wa kuwa uwezo tunao - kinachokosekana ni organisation tu. Ndio maana hata kwenye familia inayofanya harusi ya shilingi milioni tano si ajabu kukuta kuna mtoto anayekosa ada ya shilingi laki mbili!

Wakati haya yakifanyika serikali inaendelea na uboreshaji wa TPDC kimfumo, kisera na kimiundombinu ili iwe tayari kwa kazi hii. Hii ni pamoja na kuanzicha chuo cha TPDC chenye lengo la kuzalisha wataalam wa ngazi mbalimbali za ujuzi katika sekta ya mafuta na gesi.

Kwa utaratibu huu, katika kipindi cha miaka saba nchi inakuwa na wataalam pamoja na pesa na TPDC inakuwa standby. Inabaki miaka mitatu ya wataalam hao kushirikiana na wale wachache ambao tayari wapo na watendaji wa serikali kutengeneza utaratibu rasmi wa uchimbaji kutokana na utaalam waliojifunza. Pale tunapopungukiwa tunaweza kuajiri washauri wenye uzoefu zaidi, lakini wanakuja kama waajiriwa wanaosikiliza mahitaji ya mwajiri ambaye ni sisi.

Haraka ya nini? Mbona kama kuna kitu kinakimbiliwa kabla jambo fulani halijatokea? Je, ni nini future ya miradi hii baada ya jambo hilo kutokea? - kwa sababu ni lazima litokee.

Nchi yetu imejiendesha zaidi ya miaka 50 bila mafuta na gesi, inaweza kuvumilia miaka mingine kumi bila mafuta na gesi wakati tukijiandaa.

Tufikirie vizazi vijavyo. Hakuna mwingine wa kuwaandalia mazingira bora watanzania wa kesho ila ni sisi.

Kupanga ni kuchagua...

Mawazo yaku mazuri sana mkuu na yanajenga, Tatizo ni kuwa mara nyingi Serikali yetu imekuwa inapanga mipango yake au kufanya kazi zake kwa kuangalia Uchaguzi mkuu ujao sasa hili ni tatizo, inaamana uchaguzi ukimalizika akiingia mtu mwengine naye anaanza mipango yake huku kipaumbele kikiwa ni Uchaguzi unaofuata.
Kwa misingi hiyo wakati wenzetu wanapanga mipango kwa miaka 50 au zaidi ijayo sisi mipango yetu ni ya miaka 5 tu.
 
wazo Zuri na ukita kujifunza ufanisi w akujiandaa na kusomesha wakwako nenda IRAN kajifunze wnavyo tengeneza NYUKLIA maana wamesomesha watu wao na Mpaka maprofesa wao, na Israel kila siku anwaua hao wataalamu lakini ngoma ipo pale pale kwa kuwa Iran aliwekeza kwenye elimu basi manpower ipo kubw ana ya kutosha na hatetereki.
 
wazo Zuri na ukita kujifunza ufanisi w akujiandaa na kusomesha wakwako nenda IRAN kajifunze wnavyo tengeneza NYUKLIA maana wamesomesha watu wao na Mpaka maprofesa wao, na Israel kila siku anwaua hao wataalamu lakini ngoma ipo pale pale kwa kuwa Iran aliwekeza kwenye elimu basi manpower ipo kubw ana ya kutosha na hatetereki.

Kwa hiyo mifano ipo na ni juu yetu kuchagua njia sahihi.
 
Mawazo yaku mazuri sana mkuu na yanajenga, Tatizo ni kuwa mara nyingi Serikali yetu imekuwa inapanga mipango yake au kufanya kazi zake kwa kuangalia Uchaguzi mkuu ujao sasa hili ni tatizo, inaamana uchaguzi ukimalizika akiingia mtu mwengine naye anaanza mipango yake huku kipaumbele kikiwa ni Uchaguzi unaofuata.
Kwa misingi hiyo wakati wenzetu wanapanga mipango kwa miaka 50 au zaidi ijayo sisi mipango yetu ni ya miaka 5 tu.

Na haya ndio madhara ya kuacha mambo ya kitaalam mikononi mwa wanasiasa...
 
ZeMarcopolo tuna haraka kugawa maeneo hayo ya visima vya gesi na mafuta kwa kuwa watawala wetu hawataki kupoteza nafasi hii adimu ya kujilimbikizia mali na wanataka wakimaliza ngwe yao wajikute washatengeneza mfumo ambao utawahakikishia kuendeela kula kwa miaka kadhaa ijayo
Tuna haraka kwa kuwa washagawiwa chao na hawataki kuwaangusha wale waliowapa hicho chao wajikute hawajawagawia kile walichowaahidi
Shangaa uharaka huo wakati bado hatujajitengeneza huku nyumbani kujua kama nyumba ni safi wageni wanaweza kuja na kuingia kwa maana ya sera na sheria ambazo zinaweza kutupa mwanga ni asilimia ngapi na namna mwananchi wa kawaida atakavyofaidika kwenye uwekezaji huo

Mkuu Mr. Rocky nisome vizuri hapo kwenye red kwenye thread post.
 
Last edited by a moderator:
Kwa mara ya kwanza tangu nikufahamu , Sikumbuki kama uliwahi kuandika kama hivi ! umeandika kitu kizuri mno ! Japo bila shaka jibu la swali ulilouliza UNALO ( unajua kwanini wanafanya haraka, ila umeamua kutushirikisha tu ) ASANTE SANA !
 
Back
Top Bottom